Na Mwandishi Wetu
WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kushiriki kwenda kwenye vivutio vya utalii lengo likiwa ni kumuunga mkono Rais Mama Samia Suluhu Hassan kupitia filam ya Royal Tour ambayo imeitangaza Tanzania.

Wito umetolewa Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Kata ya Mabwepande Jimbo la Kinondoni (UVCCM), Andrew Mashimba, wakati akizungumza na vyombo vya habari kuhusiana na mafanikio ya Serikali ya awamu ya Sita ikiwemo ukuzazaji wa sekta ya Utalii nchini.

Kiongozi huyo alisema lengo la kuandaa matembezi hayo ya kwenda Sadaan ni kwa lengo la kumuunga mkono mama Samia katika jitihada zake za kutangaza utalii wa Nchi yetu na kutengeneza desturi ya kutembelea vitu vyetu wenyewe.

Alisema ni vyema watanzania tukapenda vya kwetu kuliko kunyamaza kimya na kuishia kulalamika wakati vivutio vyetu vipo na ni bora.

Katibu wa UVCCM Mabwepande Ramadhani Kindamba alisema kuwa wamejipanga vizuri katika kuhakikisha jambo hili linatimia.

"Sisi tukiwa vijana lazima tumuunge mkono mama na kuhakikisha kila kitu kinaenda sawa hivyo uchaguzi umeisha na sasa kazi 'Iendelee'.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...