* TUZO za KPMG kwa mwaka 2022
*Ni
kutoka kundi la Taasisi za Umma
*Kashimba: Tuzo hii ni zawadi kwa Wanachama wa PSSSF
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
Mkurugenzi
Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), CPA. Hosea
Kashimba, amepata tuzo ya kuwa Mtendaji Mkuu Bora wa mwaka 2022 kwa upande wa
Taasisi za Umma nchini.
Utoaji
wa tuzo hizo uliratibiwa na taasisi ya kimataifa ya KPMG yenye uzoefi wa miaka
35 katika masuala ya Bima, Fedha, Sheria na Kodi. Tuzo hizo zilitolewa katika
ukumbi wa mikutano wa Mlimani City Novemba, 2022 jijini Dar es Salaam na
kuhudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo watendaji wa taasisi mbalimbali.
Akizumgumza
baada ya kupokea tuzo hiyo, CPA. Kashimba alisema, “Naelekeza tuzo hii kwa
wanachama wa PSSSF, hii ni zawadi yao ya kufungia mwaka, hakika tuzo hii
inanipa nguvu ya kuwatumia vyema zaidi wanachama mwaka 2023”.
CPA. Kashimba ni mhitimu wa Chuo Kikuu Mzumbe
ambako alitunukiwa Shahada ya Uzamili katika Uongozi wa Biashara (MBA
Corporate), pia amesomea uhasibu katika Chuo cha Maendeleo ya Uongozi (IDM
Mzumbe) na kuhitimu Stashahada ya Juu ya Uhasibu. Pia CPA. Kashimba amehudhuria
mafunzo mbalimbali ndani na nje ya nchi.
CPA. Kashimba ni mwanachama wa Institute of
Directors Tanzania (IoDT) na mjumbe wa Bodi kwenye taasisi mbalimbali ikiwa
pamoja na Benki ya CRBD. Kabla ya kuteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, Bw.
Kashimba ameshakuwa Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Ndani katika uliokuwa Mfuko wa
Pensheni wa PPF. Bw.
Kashimba aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John
Pombe Magufuli kuwa Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF kuazia tarehe 19 Februari, 2019.
KPMG hutumia vigezo vingi ikiwemo uongozi bora na unaoacha alama katika sehemu unayoongoza na kwa jamii kwa jumla ili kuweza kumpata mtendaji bora.
CPA. Hosea Kashimba akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Watendaji wa Mfuko huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...