Na Mwandishi Wetu

Mbunge wa Jimbo la Babati Mjini, Mhe. Pauline Gekul, ametoa pongezi kwa Serikali ya Awamu wa Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa miradi mingi ya maendeleo jimboni hapo.

Mhe. Gekul ametoa pongezi hizo katika Mkutano wa Hadhara wa Rais, Mhe. Samia uliofanyika katika Uwanja wa Kwaraa mjini Babati leo Novemba 23, 2022 ambapo amesema kiasi cha Shilingi bilioni 1.7 unatekeleza mradi ya Vituo vya Afya, huku bilioni 1.5 zikitekeleza ujenzi wa Shule za msingi na sekondari ambapo kwa mwaka 2022 wanafunzi wameingia darasani katika madarasa ambayo yamekamilika kabisa.

Amesema kuwa, takriban Shilingi milioni 10 zimetumika katika ujenzi wa Ofisi ya Machinga Babati Mjini na wamachinga wanaendelea kufanya biashara zao kwa utulivu.

Mhe. Gekul amesema Jimbo hilo pia limenufaika na Mradi wa TASAF katika Mitaa yote kwa kutumia takriban Shilingi milioni 800.

Aidha, Mhe. Gekul amemshukuru Rais Mhe. Samia kwa kuzindua mradi wa barabara za lami wa takriban KM 8 katika Mji wa Babati. Aidha, amemshukuru kwa ahadi yake ya kuongeza KM 5 katika Mji huo.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...