Na Andrew Chale,Dar es Salaam.


WIZARA ya Afya kupitia kwa Mganga Mkuu wa Serikali [CMO], Prof. Bi. Tumaini Nagu ametoa maagizo kwa Waganga na Madaktari nchini kutoa dawa kwa wagonjwa kulingana na majibu ya Kimaabara ilikutambua dawa gani sahihi ya kutibu ugonjwa husika kuepuka usugu wa vimelea vya magonjwa dhidi ya dawa.

Ametoa kauli hiyo Jijini Dar es Salaam wakati wa wiki ya kampeni ya kuzuia usugu wa vimelea dhidi ya dawa za Antibiotiki inayoadhimishwa kila mwaka 18-24 Novemba ambapo mwaka huu kauli mbiu ‘’Kwa pamoja tuzuie usugu wa vimelea dhidi ya dawa’’, ambapo Prof. Nagu amesema usugu wa dawa husababishwa na mambo mengi ikiwemo kutofuata usahihi wa matumizi na pia kukwepa kutumia wataalam wa hospitali.

‘’kwa sasa usugu wa vimelea vya dawa umeongezeka moja wapo ni kutotumia dawa kwa usahihi, mfano mtu unaambiwa utumie dawa kwa siku tano, wewe unatumia kwa siku mbili unapopata nafuu unaaacha hapa unajenga usugu kwa sababu havijaisha mwilini mwako.

Lakini pia pia kutumia madawa kabla ya hujapimwa,
Wapo wanaoenda duka la dawa hawajaonwa hata na Daktari, wao wanaenda kuchukua dawa bila kupimwa pindi wanapojisikia vibaya wanapewa hizi dawa za Antibiotiki.

...Na hapa naomba niwaase wananchi wote, unapojisikia vibaya tumia huduma zetu za afya.

Uende hospitali yoyote iliyopo jirani, umuone daktari akupime, na ukiwa umeonekana na vimelea vya ‘infection’ atachukua 'sample' atapeleka maabara vitapimwa, kwa hiyo katika hili niwaombe pia Waganga madaktari, watumie hizi huduma za maabara kuangalia kama mtu anaugonjwa ilikujua anatumia dawa gani katika kukabiliana na ugonjwa husika.’’ Alisema Prof. Nagu.

Aidha, ameongeza kuwa, Waganga watoe madawa sahihi kulingana na ugonjwa husika, na pia ameomba kuwa watoe dawa hizo kulingana na majibu ya Maabara akisistiza.

Aidha, Prof. Nagu amesema kwa sasa usugu kwa Tanzania unakadiriwa kuwa kati ya Asilimia 59.8 hadi 60 hii ni wastani ambapo amebainisha kuwa, vimelea vipo aina nyingi na dawa zipo za aina tofauti, hivyo ametoa raia dawa za Antibiotiki ziachwe kutumika kiholela na zaidi zitumike kulingana na ushauri wa kitaalam.

‘’Vimelea vikiwemo mwilini lazima tutumie Antibiotiki, lakini tutumie kwa uangalifu kulingana na wataalam, lakini pia tuweke mazingira ya usafi ya kujilinda ikiwemo kuosha mikono mara kwa mara, kusafisha Vyoo na usafi wa mwili ilikuepuka magonjwa,

Hivyo niwaombe watu wote wananchi, tujaribu kujikinga kwa kuboresha usafi wa mazingira, kuosha vyoo na vitu vingine vingi katika hali ya usafi.’’ Alisema Prof. Nagu.

Aidha, amesema usugu wa dawa unatofautiana kulinagana na utumiaji wa madawa,katika hospitali moja na nyingine kulingana na mpangilio kazi wao wa utoaji wa madawa kwa wagonjwa wao kulingana na matumizi ya hospitali husika.

Katika kongamano hilo ambalo linatarajiwa kufikia tamati leo, wadau mbalimbali wameweza kuwasilisha mada za kibobezi katika sekta ya afya ikiwemo ya madawa ya binadamu na mifugo dhidi ya kukabiliana na usugu wa vimelea dhidi ya dawa.


Mganga Mkuu wa Serikali (CMO),Prof. Bi. Tumaini Nagu akizungumza katika kongamano la wiki ya Kampeni ya Kuzuia Usugu wa Vimelea dhidi ya Dawa, Jijini Dar es Salaam ambapo lilianza 18-25 Novemba mwaka huu




 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...