Akiwa nchini Ufaransa, Rais Mstaafu Mheshimiwa Rais Mstaafu Kikwete amekutana pia na kufanya mazungumzo na Bi. Audrey Azoulay, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO). Katika mazungumzo ya viongozi hao, imekubaliwa kuwa UNESCO na GPE zitaendalea kushirikiana katika kupeleka ajenda ya elimu mbele.
Pembezoni mwa mikutano ya Bodi ya Taasisi ya Global Partnership for Education (GPE) Rais Mstaafu Mhe. Dkt Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye ni Mwenyekiti wa GPE, aamekutana na kufanya mazunguzo mafupi na Mheshimiwa Amadou Ba, Waziri Mkuu wa Senegal. Katika mazungumzo hayo, masuala ya elimu yaligusiwa, kati ya masuala mengine
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...