Rais Mstaafu Mheshimiwa Dkt. Jakaya Kikwete, ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya  Taasisi ya Kimataifa inayoshughulikia Masuala ya Elimu Duniani (Global Partnership for Education - GPE) akingoza Vikao vya Bodi ya Taasisi hiyo vinavyofanyika Jijini Paris,  nchini Ufaransa kuanzia tarehe 5 - 7 Disemba, 2022.  

Vikao hivyo ni vya kwanza vya ana kwa ana tangu dunia ilivyokumbwa na ugonjwa wa COVID-19 mwishoni mwa mwaka 2019.  Katika vikao hivyo, Taasisi ya GPE inapitia na kuazimia masuala mbalimbali yatakayolenga kuboresha mifumo ya elimu katika nchi zinazoendelea ikiwemo kuongeza idadi ya wanafunzi wanaopata elimu, wakiwemo watoto wa kike, na matumizi ya teknolojia katika utoaji wa elimu.






 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...