Na Mwandishi Wetu, Michuzi TV

MAONESHO ya Kitaifa ya YST 2022 ambayo ni Maalum kwa kuonesha kazi za kisayansi na Teknolojia yatafanyika  Desemba 8 mwaka huu jijini Dar es Salaam huku Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof.Adolf Mkenda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam kuhusu Maonesho hayo Mwanzilishi Mwenza wa Young Scientists Tanzania (YST)  Dkt.Gozibert Kamugisha ameeleza maandalizi yamekamilika na kwenye maonesho hayo  kazi zitaoneshwa ni zile ambazo zimejikita zaidi katika masuala ya njia salama  za utunzaji  wa mazao  ya kilimo na utunzaji wa mazingira 

Pia matumizi endelevu ya rasilimali  ya maji,  dawa za asili na uboreshaji afya za binadamu,  upatikanaji na  uzalishaji wa nishati  ya umeme,  matumizi ya muziki katika  ufundishaji  wa somo hesabu mashuleni,  matumizi ya mimea ya asili katika kuboresha uzalishaji  wa maziwa ya ng’ombe na kutatua tatizo la udumavu wa ukuaji wa kuku.

"Mwaka huu idadi ya wanafunzi waliowasilisha maombi  ya kufanya kazi za ugunduzi imeongezeka kwa kiasi kikubwa hadi kufikia 1,143, kati ya idadi hiyo jumla  ya kazi  za utafiti  na kisayansi 530  zimepatiwa  usaidizi ambapo  wanafunzi  walioziandaa wamepatiwa mafunzo ya namna ya kuziboresha na hatimaye kazi za kisayansi  na ugunduzi 380 zimekamilika,"amesema.

Pia mesema mpango huu wa kuimarisha sayansi na ugunduzi kwa vijana unawezeshwa na wadhamini wakuu wa YST ambaoni Karimjee Jivanjee Foundation/Toyota Tanzania huku akitumia nafasi hiyo kutoa shukrani kwa wadhamini ambao wamekuwa wakifanikishamaonesho hayo.

“Tunatoa shukrani kwa wadhamini wetu wengine kama Shell Exploration and Production Tanzania Limited (Shell  Tanzania), Institute of Physics,  Speedy Print,  Exim Bank Tanzania Ltd, Concern Worldwide na COSTECH,” amesema Dk.Kamugisha alipokuwa akielezea Maonesho hayo ya kisayansi.

Wakati huo huo Ofisa Mtendaji wa Taasisi ya Karimjee Jivanjee Foundation Caren Rowland ameleeza namna ambavyo wamekuwa wakitoa ufadhili  kwa wanafunzi ambao wanaibuka washindi wa YST pindi wanapomaliza masomo yao ya elimu ya juu "Hivyo  mpaka sasa tumeshafadhili wanafunzi 37 na tunatarajia tena kuwadhamini wanafunzi wanne kwa mwaka huu wa 2022."Tutaendelea  kuwa bega kwa bega na YST."

 Aidha amesema kwamba wanafunzi ambao wamepata udhamini wamekuwa na mafanikio makubwa ikiwemo kuwa madaktari, wahandisi, wanasayansi na wameonesha mabadiliko makubwa hapa nchini na hilo ni jambo ambalo hata wao wanalifurahia kuona jitihada wanazofanya zinakuwa na tija kwa Taifa la Tanzania.
Mwanzilishi Mwenza wa Young Scientists Tanzania (YST)  Dkt.Gozibert Kamugisha akisoma hotuba yake  kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) leo Desemba 4,2022 Jijini Dar es Salaam kuelekea Maonesho ya YST yatakayofanyika Desemba 8,2022 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam. (kulia) Afisa Mtendaji wa Taasisi ya Karimjee Jivanjee Foundation Bi.Caren Rowland. 
Afisa Mtendaji wa Taasisi ya Karimjee Jivanjee Foundation Bi.Caren Rowland akisoma hotuba yake kwa  waandishi wa habari  (hawapo pichani) leo Desemba 4,2022 Jijini Dar es Salaam kuelekea Maonesho ya YST yatakayofanyika Desemba 8,2022 kwenye hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam.
Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mwanzilishi Mwenza wa Young Scientists Tanzania (YST)  Dkt.Gozibert Kamugisha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...