Na Mwandishi Wetu,Same

MKUU wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro Kasilda Mgeni amewahimiza  wananchi kuhakikisha wanatunza vyanzo vya maji kwa kutunza mazingira na kupanda miti pembezoni mwa vyanzo vya maji 

Mgeni ametoa ushauri huo wakati wa  kilele  cha Wiki ya Maji kitaifa yaliyofanyika katika Kata ya Hedaru mbapo pia amepanda mti huku akihimiza kila kaya  kupanda mti kwenye maeneo ya nyumba zao,

Pia  amesisitiza wananchi kuepuka kulima ndani ya mita 60 kutoka kwenye chanzo cha maji. Aidha amewaelekeza wataalamu wa maji kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi kuhusiana na suala zima la mita 60.

Aidha amewaomba wananchi wote kumuunga mkono Rais Dk.Samiha Suluhu Hassani kwa kazi kubwa anayoifanya kuleta maendeleo katika jamii.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...