Mdau mkuu wa Libeneke na nanihii
THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT "THE SMART CHOICE" Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Ila nawaomba tuweze kujieshimu kila mmoja wetu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya globu ya jamii, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoeleza vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.





 

Thursday, January 7, 2010
mambo ya ahmed viryala

 
© Michuzi | Thursday, January 07, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
mitaa nyeti jijini dar
Kijitonyama, Sinza na Mikocheni:
Mitaa ya Sayansi, Makumbusho na Maeneo ya Mikocheni Rose Garden ni hatari sana kwa kina dada na kina kaka ambao huninginiza mabegi ya laptop na mapochi makwapani mwao.

Kuna kundi la vijana linatumia magari kukwapua mabegi na mapochi hayo.
Wanachofanya ni kwamba dereva anapunguza mwendo na kukusogelea kisha abiria aliokuwa nao hukwapua mikoba hiyo na kukimbia.
Simu pia huibiwa kwa mtindo huo.

Mbagala:
Mitaa yote ya Mbagala Charambe, Hadi Kiburugwa hi hatari sana kwa kuwa kuna kundi la vibaka linaloitwa Mbwa Mwitu. Kundi hili hupora fedha, simu na kila ulichonacho hadi viatu. Ukikutana nao wanakushambulia kwa vipisi vya nondo na kukuibia huku wakikuacha huna fahamu.

Giraffe Hotel:

Kwenye maegesho ya hoteli hii ni hatari sana kwa wenye tabia ya kuacha mali za thamani ndani ya magari yao.
Kuna kundi la vijana likishirikiana na walinzi wa hoteli hiyo, huvunja vioo vidogo ya nyuma sehemu ya kiti cha abiria, hung'oa power windows na kuchukua kila wanachoweza.
Hoteli imekuwa ikijibu wanaoibiwa kuwa hapa kwetu Parking is at owners risk.

Posta ya zamani na mpya:

Maeneo haya ni hatari kwa wanaotumia daladala na wale wanaogesha magari sehemu mbalimbali za katikati ya jiji hili. Watumia daladala wa Posta huibiwa pesa na simu zao zilizomo kwenye mikoba na mifukoni wakati wakiwa wanagombania magari mida ambayo usafiri huwa mgumu. Wenye magari huibiwa vitu kama power windows na laptop ikiwa utaacha ndani ya gari. Na wezi wakubwa ni vijana wanaozagaa maeneo ya maegesho.

Bonde la Jangwani, Salenda Bridge na Bonde la Kigogo:
Maeneo haya ni hatari kwani hamna makazi, hivyo vibaka hutumia mwanya huo kufanya uhalifu mchana kweupe, na usiku maeneo haya ni hatari zaidi. Ukipata pancha maeneo ya jangwani nakushauri utembelee ringi hadi eitha Faya au Magomeni Mapipa ambapo pana watu na pana usalama. Vibaka hutokea kwa staili ya kukupa msaada na mwisho wa siku hukuacha ukiwa huna kitu na huku gari yako ikiwa skrepa.

Sea View, Ocean Road na Viwanja vya Golf Gymkhanna Club:

Maeneo haya kuna vibaka hatari sana ambao hushambulia kwa kikundi na kupora mali zote na kukuacha ukiwa majeruhi. Maeneo haya yametulia sana na yanaonekana ni salama sana kwani yako jirani na ikulu, lakini hayana usalama wowote na ni hatari kabisa.
Usipite maeneo hayo kwa miguu mida ya kuanzia saa kumi na mbili na nusu giza likiwa linaingi, maana utakumbwa na dhahama.
Daraja la Mlalakuwa, karibu na makao makuu JKT
Hapa watu wamesema weeeee wamechoka. Yaani watu wanavyoporwa kila siku kijua kikizama inaanza kuaminika kwamba wapiga loba ni askari wa hapo JKT ama wanashirikiana na hao vibaka. Wakazi wanajiuliza iweje sehemu nyeti kama hiyo pawe na vibaka? Wanatokea wapi?

TUTAFIKA kweli?
Afande Kova upooooooooo????

NB: Sehemu ambazo hazijatajwa, ikiwa hata mikoani na visiwani, msaada tutani wadau


 
© Michuzi | Thursday, January 07, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
kwa vijana wa zamani tu: tuwakumbuke Trio Madjesi

 
© Michuzi | Thursday, January 07, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
simba wa vita aombolezwa nairobi
Chumba maalumu kilichotengwa katika Ubalozi wa Tanzania, Nairobi Kenya, ambacho kinatumiwa na wageni kutia saini kitabu cha maombolezo kufuatia kifo cha Mzee ashidi Mfaume Kawawa, Simba wa Vita
Balozi wa Zambia, Mrs Charity K.M. Mutesha akitia saini kitabu cha Maombolezo katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Nairobi. Alimwelezea Mzee Kawawa kama shujaa na kwamba Taifa limepoteza kiungo muhimu.

Balozi wa Uganda nchini Kenya Mrs Angelina C. Wapakhabulo akitia saini kitabu cha Maombolezo katika ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Nairobi Kenya.
Balzozi wa Tanzania nchini Kenya Mh. Nyasugara P. Kadege (Kulia) akibadilishana mawazo na Balozi wa Uganda Nchini Kenya mara baada ya kutia saini kitabu cha maombolezo, wakitafakari juu ya kifo cha Simba wa Vita

Afisa Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya Mrs Mola (consular Affairs) akimkaribisha Balozi wa Russia nchini Kenya alipowasili ofisi za Ubalozi wa Tanzania Nairobi kutia saini kitabu cha Maombolezo
Balozi wa Iran nchini Kenya Mh. Mahmoud Zand akitia saini kitambu cha maombolezo
Afisa ubalozi wa tanzania Nairobi Bw. Stanley Ngozi akisalimiana na Balozi wa Iran Nchini Kenya mara baada ya Balozi huyo kutia saini Kitabu cha Maombolezo








 
© Michuzi | Thursday, January 07, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
UDSM yachangia shule ya sekondari mbagala
Makamu wa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandala (Mwenye suti) akikabidhi mfano wa hundi ya Shilingi Milioni nane kwa Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari Mbagala Dar es Salaam Mwl. Marcelina Kimario ikiwa ni michango ya wafanyakazi na wanafunzi wa Chuo hicho kwa shule hiyo ili zisaidie kukarabati sehemu ya madarasa iliyoharibika kufuatia ajali ya milipuko ya mabomu iliyotokea mwezi Februari mwaka jana.
Makabidhiano hayo yamefanyika shuleni hapo mbele ya viongozi akiwamo diwani Mh. Jerome Bwanausi wa kata ya Mbagala Kuu, waalimu na wanafunzi wa shule hiyo. Wengine waliofuatana na Prof. Mukandala ni Kaimu Mkurugenzi wa Huduma kwa Jamii Prof. Amandina Lihamba (wa Kwanza kushoto), Mkuu wa Shule ya Elimu Prof. E. Bhalalusesa(wa kwanza kulia) na Mkurugenzi wa Rasilimali watu na utawala Bw. Edward Jambo (hayuko pichani).
 
© Michuzi | Thursday, January 07, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
Aga Khan Mzizima Reunion 2010

 
© Michuzi | Thursday, January 07, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
rwanda on the run
Little known by the outside world until genocide tore the country apart 15 years ago, Rwanda has become the first nation to launch a wireless broadbandI Internet facility in Africa.

Unlike other countries in Africa, where mobile broadband Internet connection is restricted to a few buildings, Rwanda's capital city, Kigali, has become the first capital city in Africa broadly offering high-speed services, overtaking Nigeria and South Africa, Africa's biggest telecom markets in terms of both investment and users.

The launch of the wireless facility means that Rwandese will now be able to surf the Internet anywhere and anytime in the capital city using their laptops.
The US$7.7 million wireless internet facility has been built by Korea Telecom, South Korea's largest fixed line operator. Korea Telecom is a prominent South Korean integrated wired and wireless telecom service provider.
The contract to build the wireless Internet facility was awarded to Korea Telecom in 2007 by the Rwandan government. The service is based on WiBro technology, the South Korean version of the mobile WiMax IEEE 802.16e specification, and will offer 5.5Mbps and 2Mbps connection speeds.

The launch of the wireless internet facility also marks the entry of wireless broadband technology in Africa.

"By launching the wireless facility, Rwanda has become the ICT hub not just in east Africa but the whole Africa. Other countries must surely follow the footsteps of Rwanda," said Mwape Mutale, CEO of the center for ICT development in Africa.

In addition to the wireless broadband internet facility, Korea Telecom is also constructing a US$40 million Kigali Metropolitan Network project. The Kigali Metropolitan Network project is based on on a fiber-optic loop and will be the largest computer network in Rwanda, providing connectivity for local area networks. The Rwandan government claims over 45 government institutions have already been connected to the high-speed Internet facility.

The Rwanda Metropolitan Network will be completed next year, according to Rwanda Development Board (RDB) deputy chief executive in charge of information technology Patrick Nyirishema.

Rwanda's vision is to promote and facilitate modern infrastructure development by 2020.
In the next three years, the Rwandan government is aiming to provide access to high speed Internet to more than 4 million Rwandans through the wireless Internet facility and the Kigali Metropolitan Network project.
Until last year, Rwanda was also the first country in Africa to have a mobile phone assembling plant through a company called A-Link Technologies.
Early this year, the world Bank provided $24 million to Rwanda for the provision of broadband connectivity and access to low-cost international connectivity through the connection to the undersea cables in east Africa.
 
© Michuzi | Thursday, January 07, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 11
madhara ya mafuriko kilosa
Kundi la Waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali akiwemo mdau John Nditi (shoto chini ) pamoja na Nickson Mkilanya wa Star TV na Redio Free Afrka wakijiandaa kupanda kiberenge kuelekea kilometa zaidi ya 10 toka mjini Kilosa , njia ya reli ya kati kulekea eneo liliposombwa na maji darala la reli katika Mto Mkondoa , usiku wa mkesha wa mwaka mpya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais – Mazingira , Dk Batilda Burian , ( kulia) akiwa pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Miundombinu , Omary Chambo ( kati kati) na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo ( kushoto) wakitafakari hali halisi ya uharibifu wa mazingira na athari za mafuriko yaliyowakuba wakazi zaidi ya 24,000 wa mjini Kilosa kuanzia Desemba 26, mwaka jana.

Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkullo ( kushoto) akipita orodha ya vifaa vya misaada ya dawa za binadamu na mingine iliyotolewa na Mkurugenzi wa Hospitali ya Regencyu ya Dar es Salaam ( hayupo pichani) iliyowasilishwa kwa Mbunge wa Jimbo la Kilosa ikiwa ni kuwasaidia waathirika wa mafuriko yaliyotokea mjini Kilosa kuanzia mwishoni mwa mwaka jana.

wananchi wa Kilosa wakibeba misaada kupeleka kwa waathirika wenzao wa mafuriko hayo
wananchi wakivuka mto mkondoa
daraja la reli ya kati iliyokumbwa na madhara ya mafuriko hayo
sehemu ya uharibifu huo

daraja likiwa limebomoka kwa mafuriko










 
© Michuzi | Thursday, January 07, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
salamu za mwaka mpya toka VOA
Kikosi Kazi cha Voice of America (VOA) idhaa ya Kiswahili kinawatakia wadau wote wa Globu ya Jamii heri ya mwaka mpya. Ujumbe: Tuendeleze libeneke. Toka shoto ni Juma Nkamia, Mwamoyo Hamza (mkuu wa idhaa), Mkamiti Kibayasi,Khadija Riyami na Sunday Shomari na kwa upande wa nyuma Abdu shakura Aboud,Ester Ewart na Duane Collins.

 
© Michuzi | Thursday, January 07, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
Wednesday, January 6, 2010
ugiriki tambararezzzzz....
Katibu wa jumuiya wa Tanzania (mmatumbi pekee) akishiriki katika mada mbali mbali za wageni Ugirki. Sheria ambayo inatarajiwa kupitishwa bungeni tar 7 Jan.10 kuhalalisha kupatiwa uraia kwa mtu yoyote alokaa miaka mitano kihalali pamoja na watoto wao waliozaliwa Ugiriki au kama mtoto amekua anasoma shule Ugiriki kabla hajatimia miaka 18 at least awe amehudhuria miaka mitatu nyuma,kwa kusema awe ameanza kusoma tokea akiwa na umri wa miaka 15. banda letu maoneshoni athens

maandamano ya wageni kulilia sheria mpya ya uhamiaji

Mheshimiwa Ankal,
naomba tuwekee hili wazi. Kwa mara ya kwanza na katika historia wakaazi waliokaa ugiriki kwa atleast miaka mitano tu kisheria pamoja na watoto wao basi watakula nondo(Passport)za kigiriki.Ikiwa mzazi wa mtoto atakua anaishi kisheria kwa miaka mitatu basi akitimiza miaka mitano tu yeye na mtoto wake wanakula nondo kama kawa.

Sheria isharekebishwa na inapitishwa bungeni Tar 7 Jan.10 kwa kupigiwa kura,WADAU TUNAOMBA DUA ZENU,TUMEDATAA NA POPOTE ULIPO K AMA ULIKAA UGIRIKI RUDI HARAKA UWAHI KULA NONDO LAKO.
Habari zaidi pitia www.tanzaniansingreece.com KATIKA SITE YETU USOME
Mdau Nuramo

 
© Michuzi | Wednesday, January 06, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 21
maombolezo ya simba wa vita india

TAARIFA KWA WANAJUMUIA YA WATANZANIA WAISHIO DELHI


Ubalozi wa Tanzania Nchini India- New Delhi, unawakaribisha Watanzania wote kujumuika katika kusaini kitabu cha maombolezo ya Waziri Mkuu na Makamu wa Rais wa Awamu ya kwanza, Mpendwa wetu RASHID MFAUME KAWAWA maarufu SIMBA WA VITA aliyetutoka hivi karibuni.

Kitabu cha Maombolezo kitakuwepo Ubalozini eneo la Chanakyapuri EP 15 kwa ajili ya Watazania wote kuanzia saa Tano Asubuhi MPAKA Jioni kuanzia Kesho Alhamisi JANUARY 7TH Hadi Ijumaa JANUARY 8TH.

Wote Mnakaribishwa kutoa heshima hiyo Muhimu.
Mungu Ailaze Roho ya Marehemu RASHID MFAUME KAWAWA .AMEN.

Mwenyekiti wa Tasa - New Delhi
Jennifer Sumi.

 
© Michuzi | Wednesday, January 06, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
daktari bingwa...

video

 
© Michuzi | Wednesday, January 06, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
JK apata dina la mchana na ivory coast, rwanda na taifa stars leo
JK akimzawadia jezi ya TAifa Stars nyota wa Ivory Coast na Chelsea Didier Drogba katika dina la mchana alilowaandalia wachezaji na viongozi wa Taifa Stars, Rwanda na Ivory Coas mchana huu hoteli ya Golden Tulip jijini Dar.
JK katika picha ya pamoja na timu ya Ivory Coast
JK na Ivory Coast
JK katika picha na timu ya Taifa ya Rwanda ambayo imedhatua nchini kucheza na Ivory Coast kesho neshno
Kocha wa Taifa Stars Marcio Maximo na vijana wake
Baadhi ya wachezaji wa Rwanda

JK akoshwa na ziara ya Ivory Coast
*Awaandalia chakula maalumu Golden Tulip
*Amwagia sifa Drogba, amkabidhi uzi wa Stars
Awaombea watwae taji, aahidi Watz kuwashangilia
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, ameelezea kufurahishwa na ujio wa timu ya taifa ya Ivory Coast ‚The Elephant’ kwani umeutangaza nchi kutokana na wachezaji wake nyota wa kimataifa kujulikana akiwemo mshambuliaji wa klabu ya Chelsea Didier Drogba.
Akizungumza katika hafla maalumu ya chakula cha mchana aliyoiandaa kuwakaribisha Ivory Coast, kwenye Hoteli ya Golden Tulip jijini Dar leo JK kasema Tanzania imepata sifa kubwa duniani baada ya kutangazwa kwa mara ya kwanza katika kituo cha televisheni cha Sky News, kuhusiana na ziara ya The Elephant katika habari za michezo, sambamba na kuonyesha picha.
Kikwete alisema, kutangazwa kwa mechi kati ya Tanzania na Ivory Coast ni sifa kubwa kwa nchi, hasa ukizingatia Taifa Stars iliweza kuwamudu The Elephant ambao walikuwa wamesheheni nyota wa kulipwa na kutoka na ushindi mwembamba wa bao 1-0, lililofungwa na Drogba.

Rais alimpa pongezi kubwa mshambuliaji huyo ambaye pia ni tegemeo wa klabu ya Chelsea ya England, kwa kuitangaza Tanzania alipokuwa akihojiwa na Sky News Sports, ambako hakusita kusifu kiwango cha wachezaji wa Stars, kuwa ni kikubwa.

"Jana nilifurahi sana nilipokuwa nikiangalia kituo cha Sky News Sport, kwa mara ya kwanza kuona wakitangaza timu ya Ivory Coast ikiwa nchini, ambapo mchezaji nyota wa kimataifa Drogba alikiri kwamba, Tanzania soka lipo huku akisifu kiwango cha Stars," alisema Kikwete.

Kikwete alisema, kutokana na Drogba kuwa mchezaji maarufu duniani, kwa kupitia umaarufu wake, Tanzania imeweza kujitangaza duniani kote na hiyo itasaidia kuwavutia nyota wengine kufanya ziara hapa nchini.
"Hivi sasa Dunia nzima inatambua kiwango cha soka la Tanzania, natoa shukrani nyingi kwa Ivory Coast kuichagua nchi yetu kupiga kambi ya kujiandaa na fainali hizo za Angola," alisema Kikwete.

Aidha alisema, alipanga kuandaa hafla hiyo na kuwaalika wachezaji wa Ivory Coast, lakini baadaye akaona ni bora ajumuike na timu zote tatu, ambazo ni wenyeji Tanzania, Rwanda na Ivory Coast.

Katika hatua nyingine, Kikwete aliwataka wachezaji wa Rwanda ‚Amavubi’, kucheza kwa kujituma na ushirikiano mkubwa ili kuwafunga Ivory Coast, baada ya Stars kufungwa 1-0 licha ya kuwa, angalau wangeweza kutoka sare, lakini bahati haikuwa yao.

Aliongeza kuwa, Tanzania itajivunia hivi sasa katika Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, kutokana na Ivory Coast kuichagua pekee kwa ajili ya kuweka kambi ya kujiandaa na fainali za Angola, pamoja na Kombe la Dunia litakalofanyika Afrika Kusini.

"Ninaamini kuwa, Bara hili la Afrika lina timu nyingi huku Ivory Coast ikiwa inaongoza kwa ubora, hivyo kwa kuchagua kuja nchini kwetu kufanya mazoezi ya mwisho ya kujiandaa kwenda Angola katika Fainali za Afrika, ni jambo la kujivunia kwa kila Mtanzania," alisema Kikwete.

Wakati huohuo, Kikwete alisema, anawaombea kwa Mungu na Miungu mingine kutwaa ubingwa wa Afrika, ili kurejea na Kombe hilo kama walivyopanga kulileta na kulipeleka Mlima Kilimanjaro na kuongeza kuwa, ana imani watashinda.

Aidha alisema, Tembo hao wa Ivory Coast watakapotinga hatua ya fainali, Watanzania watakwenda kuipa sapoti ili kutwaa taji hilo.

Mwisho wa hafla hiyo, Rais Kikwete aliwakabidhi jezi ya Taifa Stars, wachezaji nyota wa kimataifa wa Ivory Coast, Didier Drogba, Kolo Toure, Emmanuel Eboue, Solomon Kalou na Yaya Toure.

Fainali za Mataifa ya Afrika zinatarajiwa kuanza kutimua vumbi Januari 10 hadi 30, mwaka huu nchini Angola.




 
© Michuzi | Wednesday, January 06, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 37
mwaka mpya na mambo mapya CRDB Bank
Mwaka mpya, na mambo mapya. CRDB inakuja na droo zitazotokana na Manunuzi ya Bidhaa na huduma kwa kutumia TemboCardVisa, ambapo walengwa ni wateja wote wa Benki ya CRDB na watumiaji POS za Benki ya CRDB.

Benki ya CRDB Imeendelea kukusikiliza wewe mteja wake kwa kukupa huduma bora na za kiwango cha juu kabisa.
Kama hilo halitoshi, Benki ya CRDB sasa inakupa nafasi ya kutimiza ndoto yako ya kujishindia safari ya kwenda Afrika Kusini kushuhudia Fainali za Kombe la Dunia live na Zawadi nyingine kem kem kama Luninga plasma ilionginishwa na DSTV, Fulana, miamvuli, kofia n.k

Unachotakiwa kufanya ni
kutumia kadi yako ya TemboCardVisa kufanya malipo ya zaidi ya Shilingi 50,000/= kupitia mashine za malipo za Benki ya CRDB (Point of sales)
kila ununuapo bidhaa au kupata huduma kwenye Maduka, Migahawa, Supermarket, Malls, Maduka ya Dawa, Vituo vya mafuta, ulipiapo mbuga za wanyama (TANAPA) au ukilipa kodi (TRA) ili uweze kuingia kwenye draw na kujitengenezea nafasi ya kushinda.

Zawadi zote zitapatikana katika draw kubwa mbili ambapo:

Draw ya mwezi wa kwanza na wa pili:

Mshindi mmoja, atajishindia safari, chakula, malazi na Ticket ya kushuhudia live mechi ya kombe la Dunia Afrika kusini

Mshindi wa Pili na Watatu watajishindia Luninga ya SONY bapa (Plasma) inchi 32 zilizounganishwa na kulipiwa DSTV kwa mwezi mzima wa mashindano!

Wasindi wengine watano watajishindia zawadi kem kem ikiwamo T-shirts, Mipira, miamvuli nk.

Draw ya mwezi wa tatu:

Washindi watatu wa mwanzo, kila mmoja atajishindia safari, chakula, malazi na Ticket ya kushuhudia live mechi ya kombe la Dunia Afrika kusini.

Mshindi wa nne na watano,watajishindia Luninga za SONY bapa (Plasma) inchi 32 zilizounganishwa na kulipiwa DSTV kwa mwezi mzima wa mashindano!

Mfanyabiashara ambaye POS zake zitakuwa na miamala mingi nae atajishindia tiketi ya kwenda kushuhudia fainali hizi. Pia, wafanyakazi wa sehemu za biashara zenye miamala mingi pia watajishindia pesa taslimu kuanzia shilingi 100,000 mpaka shilingi 250,000

Anza sasa kufanya malipo kwa kutumia kadi yako ya TemboCardVisa na uwe mshindi!

CRDB Bank
Benki inayomsikiliza mteja


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Membe akikata utepe kuzindua huduma za ATM za kwenye magari wakati wa sherehe hizo.

Mh. Membe akibofya kwenye moja ya kompyuta za kwenye magari ya ATM baada ya kuzindua. Nyuma yake ni Mkurugenzi Mkuu wa CRDB Dr. Charles Kimei na maafisa wengine.

Mh. Membe akiwa na Mwenyekiti wa Bodi ya CRDB Bw. Martin Mmari, Mkurugenzi Mkuu wa , CDRB Bank Dk. Charles Kimei na Mkurugenzi wa Masoko na Utafuti wa CRDB Bi. Tully Esther Mwambapa wakati wa uzinduzi wa huduma ya matumizi ya TemboCardVisa
Mh. Membe akiwa na viongozi wakuu wa CRDB pamoja na mwakilishi toka ubalozi wa Afrika Kusini Carol Rath wakati wa uzinduzi huo.
Mh. Membe akiwa na uongozi wa CRDB Bank na watendaji kitengo cha TemboCardVisa
 
© Michuzi | Wednesday, January 06, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 7
bei ya madafu leo

 
© Michuzi | Wednesday, January 06, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
The Details For Julius Nyerere Master's Scholarships - Deadline April 1, 2010
Please apply if this interests you otherwise send this to any Tanzanian who is currently ordinarily residing in Tanzania and wants to apply. (Note that there are other scholarships from the University for other African candidates from other countries).

Simple 7 Useful Points For Those Who Are Seriously Interested in Getting Their Scholarship at the University of Edinburgh, in Scotland:


*Apply directly to the University of Edinburgh for Admission in Your Chosen School, Your Chosen Course. You MUST get admission into your chosen course for you to be considered for the scholarship.

*Apply for the scholarship directly via online as explained here - http://www.scholarships.ed.ac.uk/postgraduate/internat/nyerere.htm. Completed application forms must be returned to the Scholarships and Student Finance Office no later than 1 April 2010.

*Do not waste time sending queries to the University or TzECA members. All the required information is on this email and the link given.

*Follow the instructions to the last word, and do not make any assumptions. Read all the links in this email and pay attention to all the details.

*Apply more than one scholarship using the check boxes BUT ensure you have read the eligibility criteria for each award.

*For someone who has never applied before to such scholarships, don't shy from getting a trusted and perhaps senior to you as second pair of eyes to go through your application, spell check, etc, just make it the best quality you can, then you can leave the rest to the process, but you MUST do your part as perfect as you can. *Don't think of competition as something to discourage you, just think that your application is the best ever and BELIEVE that is the case and deliver the Quality to the Best Standard Ever

*Don't wait to the last minute, give it plenty of time and start working on it NOW.

Feedback from last round of applications : (remember two Tanzanians were awarded their scholarships and are now attending their courses)

Applications for the 2010-2011
Julius Nyerere Master's Scholarship:

Last year there were cases of Tanzanian students applying for scholarships other than the Julius Nyerere Master's Scholarship (such as the Southern African scholarship: http://www.scholarships.ed.ac.uk/postgraduate/internat/sas.htm
but who were also eligible for the Julius Nyerere Master's Scholarship and, unfortunately, didn't apply for it. I am reliably informed that as of September applications can be made on a generic scholarship application form that will simplify the process by offering tick boxes for each of the different scholarships that applicants would like to apply for. This will help ensure that those Tanzanians who are eligible for the Julius Nyerere Master's Scholarship consider applying for it, and can do so more easily.

Another improvement for Tanzanians is that the Julius Nyerere Master's Scholarship will also be advertised through the British Council on their website and in the Dar es Salaam office.

University of Edinburgh also now have a Desmond Tutu Scholarship for anybody who wants to study an M.Sc. on 'emancipatory' topics such as Politics or Religion. I don't know much about this Scholarship at the moment but I hope that more details will be available on the UoE Scholarships website soon.

Please note that TzECA (http://www.tzeca.org.uk) does NOT offer any scholarship - so no need to send anything to anyone in TzECA. All applications must be directed to the University of Edinburgh as per online instructions.

If This Is NOT For You, Please Send To Someone Else You Know Who May Benefit From This Opportunity And Let Him/Her Have The Information And Allow Him/Her To Make Up His/Her Own Mind. Do Not Simply Delete or Hide It In Your Own Mailbox. Just Take Two Minutes To Think And You Will Definitely Find Someone Who Potentially Qualifies And May Want To Apply.

All the best and happy new year 2010.

Regards

Apollo Temu
Chairman
Tanzania Edinburgh Community Association (TzECA)

Additional Details:

Web: http://www.tzeca.org.uk -
Tanzania Edinburgh Community Association (TzECA)
f: http://www.facebook.com/group.php?gid=29100921417 - Tanzania Edinburgh Community Association (TzECA) on Facebook


Links and Some Photos, Courtesy of the University of Edinburgh. The University of Edinburgh is a charitable body, registered in Scotland, with registration number SC005336:

The following link on the celebration of the life of Julius Nyerere features on the front page of the University of Edinburgh's website, complete with a short film clip:
http://www.ed.ac.uk/news/all-news/021209-nyerere
 
© Michuzi | Wednesday, January 06, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
Tuesday, January 5, 2010
mario

 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 12
mwanaume wake wengi ati...
Rais Jacob Zuma akiwa na mai waifu zake wote watatu, mpya ni wa pili shoto

 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 68
MAOMBOLEZO YA SIMBA WA VITA LONDON
bendera ya Tanzania ikipepea nusu mlingoti ubalozi wetu London
mtoto wa mdogo wa Sima wa Vita ambaye pia ni wajina wake, Rashidi Kawawa, akiweka sahihi kwenye kitabu cha maombolezo. Hitma imeandaliwa siku ya Jumamosi kuomboleza kifo cha mpendwa wetu
Mabalozi mbalimbali wamejitokeza kutoa rambirambi na kuweka saini daftari la maombolezo ya kifo cha Mzee Rashid Mfaume Kawawa hapa Ubalozi wa Tanzania, London. Ubalozi huu umefungua kitabu hicho leo asubuhi kufuatia kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Pili wa Rais kilichotokea jijini Dar es Salaam tarehe 31 Desemba 2009.
Mabalozi na wawakilishi wa nchi mbalimbali waliopo hapa London wamemuelezea Mzee Kawawa kama nguzo muhimu ya historia ya Tanzania na Kiongozi aliyeacha mfano wa unaminifu.

Balozi wa Zimbabwe, Mhe. Gabriel Machinga (Picha ya juu) amesema "Tunashukuru kwamba Mzee Kawawa ameacha historia iliyovuka mipaka ya nchi yake na bara zima la Afrika. Atakumbukwa sana na wengi tunamshukuru kwa kazi aliyoifanya."
Balozi wa Zambia, Profesa Royson Mukwewa akiweka sahihi yake. Yeye alimwelezea Mzee Kawawa kama "Shujaa Mkuu wa Tanzania na Afrika aliyejitolea muhanga kupigania ukombozi wa Bara zima." Alisema njia pekee ya kumuenzi Mzee Kawawa ni kuendeleza yale aliyoyapigania wakati wa uhai wake.
Balozi wa Papua New Guinea, Bi Jean L Kekedo, O.B.E. akiweka sahihi yake. Amesema "Tunatoa pole kwa kifo cha kiongozi huyu mkuu." Balozi wa Ghana, Profesa Kwaku Danso-Boafo akiweka sahihi na kusema "Afrika imempoteza kiongozi wa kipekee. Bwana Kawawa alikuwa kiongozi aliyetutia hamasa wanasiasa wengi Afrika, wengi wetu tuliingia kwenye siasa kwa kufuata nyayo zake. Alichangia kiasi kikubwa kwa ukombozi wa Afrika." Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania waishio UK, Ndugu Abubakar Faraji akiweka sahihi yake. Kwa majonzi makubwa amesema jina la Simba wa Vita halikuja hivi hivi na kwamba ni kweli Mzee Rashidi Mfaume Kawawa alikuwa sima wa vita vyote vya Tanganyika na baadaye Tanzania, akisimama kidede katika shida na raha zote nchi ilipitia. Na kwamba endapo Mwalimu Nyerere alikuwa wino basi Mzee Kawawa alikuwa kalamu na kwa pamoja waliweza kuiandika historia ya kipekee ya Tanzania ambayo ni kisiwa cha upendo, amani na utulivu kutokana sio tu na busara zao bali pia kwa kuona mbali na kuunganisha matabaka yote.
BURIANI SIMBA WA VITA
RASHIDI MFAUME KAWAWA
By Ayoub Mzee
Today the Tanzania community, Diplomats and friends of Tanzania gathered at the Tanzania High Commission to Pay their respect by signing the condolences book that was opened at the High Commission on 3 Stratford Place, London.
This book will be opened till Friday this week for all to come and sign.

Rashid kawawa who was the first Prime Minister of Tanzania died in the morning of 31 december 2009 in Dar es salaam. A seven- day mourning period has been declared by President Jakaya Kikwete.

The Tanzania community in the diaspora in conjunction with the Tanzania High commission in London will hold a memmorial service for the late on the 9th January 210 at
St Annes Mosque -St Annes Road,
Tottenham ,
London,
N15 5GJ

You are all welcome
 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
SAMRA NA NASSOR WAMEREMETA DUBAI
Bibi Samra Abdulrahaman Khatib na mai hazbandi wake Bwana Nassor Humud Nassor wakimeremeta katika mnuso wa nguvu uliofanyika jioni ya siku ya kwanza ya muongo wa pili wa karne ya 21, kwenye Hotel ya Intercontinental, Festival City Dubai. Bwana na Bibi Harusi wote ni Watanzania, wakazi wa Dubai.
maharusi wakilishana keki wakati wa mnuso huo
ngoma za utamaduni kutoka nyumbani zilikuwepo
wageni waalikwa, ndugu, jamaa na marafiki walikuwapo kibao




 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 3
msaada kwenye tuta
NIMEOKOTA MILIONI 4.6 NIPELEKE WAPI?

Brother Michuzi,

Habari za kazi. Mimi ni mama Mkristu mlokole na nimempokea Yesu miaka minne iliyopita. Nimeajiriwa kama mwalimu wa English Medium School hapa mjini Arusha.

Wiki iliyopita nikitokea wilayani Monduli ambako nilienda kwa sherehe za Krismasi nilipanda basi na nikawa nimeketi na mzee mmoja wa kimasai. Alipofika maeneo ya Burka alishuka, na akawa amesahau mfuko wake wa rambo pale chini ya kiti alipokuwa amekaa. Sikuwa nimeuona mpaka nilipokuwa nateremka kwenye basi hapa Arusha mjini.

Ilinibidi kuangalia ndani ya ulie mfuko na nikaona kuna pesa za ajabu.

Sikumwambia mtu na nikazichukua nikashuka ndani ya basi na kungoja kama yule baba atakuja pale stendi ili nimpatie. Nilikaa pale stendi kwa masaa 7 (kuanzia saa 5 asubuhi mpaka saa 12 jioni)na sikumwona kabisa yule bana japo kweli nilijitahidi kumtafuta.

Ilibidi niende nazo nyumbani. Kufungua nikaanza kuzihesabu. Zipo shilingi milioni 4 na laki sita taslim. Sasa yule baba simjui na tayari mimeshatoa matangazo kwenye redio nikisema aliyepotewa na pesa aje kwangu. So far sijamwona yule baba. Wanakuja matapeli tuu.

Nawaomba wadau wako wanishauri hizi fedha nifanyeje nazo? NIZITUMIE MIMI, NIPELEKE KWA MCHUNGAJI au NIPELEKE POLISI? Dhamiri yangu bado inanisuta.

Ni mimi
LAIZER M.J.D,
ARUSHA
 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 56
MKUTANO WA WATANZANIA TAMIL NADU, INDIA.
Mheshimiwa Col. Saleh Farrah (MB- Raha Leo) aliyekuwa mgeni rasmi akitoa hotuba ya ufunguzi rasmi wa kongamano la watanzania Tamil Nadu.
Baadhi ya washiriki wa kongamano la watanzania Tamil Nadu wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi nje ya ukumbi wa mkutano wa Holy Cross brothers, Chennai.
Kama ilivyo ada watanzania wanaoishi katika miji mbalimbali ya jimbo la Tamil Nadu, India walikutana kuanzia tarehe 26 mpaka 27 disemba 2009 katika mji mkuu wa jimbo hili, Chennai. Watanzania hao walipata nafasi ya kufanya kongamano la siku moja kujadili mustakabali wa jumuiya na hasa zaidi kujadili mikakati ya kuiimarisha jumuiya hii. Moja ya mafanikio makubwa ya kongamano hili ilikuwa kupatikana kwa fedha kiasi cha USD 200 kuchangia gharama za hosting za website ya jumuiya inayotarajiwa kuwa hewani kufikia tarehe 30 januari.

Konagamano hilo la siku moja lilizinduliwa rasmi na Mh.Col. Saleh Farah (Mb – Rahaleo). Katika hotuba yake ya ufunguzi Mh. Farrah alisisitiza umuhimu wa malengo yanayotuweka pamoja na kujifunza kuitumia jumuiya kama chombo cha kusaidia wakati wa shida. Aliwahimiza wajumbe kutokatishwa tamaa na uchache wao bali kujenga misingi imara ya jumuiya ili watakaokuja kuirithi waelewe malengo ya waasisi wa jumuiya.

Mwenyekiti aliyemaliza muda wake Ndg. Deus Valentine alimshukuru Mh. Farrah kwa moyo wake wa utayari kushirikiana na wanajumuiya hata pale alipopata taarifa ndani ya muda mfupi. Mwenyekiti alimshukuru zaidi Mheshimiwa kwa utayari wake na ukarimu kwa kujitolea kugharamia gharama zote za kuanzishwa kwa tovuti ya jumuiynzia inayotarajiwa kurushwa hewani kuanzia mwezi wa Januari, 2010. Hatahivo alimuomba mgeni rasmi ashirikiane na wanajumuiya kutangaza mema mengi aliyojionea katika jimbo la Tamil Nadu hasa zaidi nafasi za kimasomo ambazo gharama zimethibitika kuwa ndogo kuliko kusoma nyumbani.

Kongamano la siku moja lilifuatiwa na mkuatano mkuu wa mwaka ambao ulihusisha pamoja na mambo mengine mjadala juu ya mabadiliko ya katiba na uchaguzi wa viongozi wapya. Mabadiliko ya katiba yameidhinisha kuundwa kwa mfumo mpya wa uongozi ambapo kamati tendaji itabadilishwa na kuwekwa sekretariati itakayoongoza utendaji wa jumuiya. Utendaji wa jumuiya utaongozwa na mtendaji mkuu ambaye ni katibu mkuu atakeyeshirikiana na mweka hazina kuunda sekretariati. Nafasi ya mwenyekiti itakuwa ya muda itakayokuwa ikishikiliwa na Mwakilishi wa mji ambapo vikao rasmi vya jumuiya vitafanyika. Mabadiliko haya yanalenga kuongeza ufanisi na kupunguza gharama za uendeshaji wa jumuiya.

Jumuiya ya watanzania Tamil Nadu inawashukuru wote waliochangia kufanikisha kongamano na mkutano mkuu. Kwa namna ya pekee inamshukuru Mh. Saleh Farrah kwa mchango wake. Inawakaribisha wazazi na wanafunzi ambao wangependa kusoma katika jimbo la Tamil Nadu kwa elimu ya juu kuwasiliana na uongozi wa jumuiya ili kupata habari za uhakika kuhusu vyuo bora. Nafasi zilizopo ni nyingi na elimu ni ya hali ya juu kwa gharama nafuu kabisa.

Mungu ibariki Tanzania.

Imetolewa na Sekretariati ya Jumuiya ya Watanzania Tamil Nadu
Watanzania.tamilnadu@yahoo.com
+919840543985

 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
kumbukumbu

BADO NAKUMBUKA ni salam ambazo babatau amezitoa kufuatia msiba wa Vumi Urasa aliyewahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya The Guardian... Soma salamu hizo kupitia blogu yake ya
babataublog.wordpress.com
 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 0
kombe la mapinduzi cup kuanza zenji na dar kesho
Mashindano ya kuwania kombe la mapinduzi ya yanayodhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania yanatarajiwa kutimua vumbi kesho katika viwanja vya Mao Tsetung na Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam.

Mratibu wa Mashindano hayo ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Soka Cha Zanzibar (ZFA), Nassoro Salim Eljazeera alisema kwamba kila kitu kiko tayari kwa mapambano hayo.

Katika mashindano hayo, timu za Miembeni na Zanzibar View zitapambana katika uwanja wa Mao Tsetung wakati Simba na na Malindi zitachuana Jijini Dar es Salaam katika uwanja wa Karume.

Aljazeera alisema Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Dk Mwinyi Haji Makame ndiye atakayekuwa mgeni rasmi katika mchezo wa ufunguzi katika uwanja wa Mao Tsetung.

Mkuu wa Udhamini na Mawasiliano wa Vodacom Tanzania George Rwehumbiza alisema kampuni yake imedhamini mashindano hayo kwa zaidi ya Shilingi milioni 68.

Alifafanua kuwa udhamini huo unajumuisha vifaa vya michezo na fedha taslim.
Rwehumbiza alisema mashindano haya yanajumuisha timu za Tanzania bara na visiwani na kushindana kama ligi zikiwa katika kundi moja, alizitaja timu hizo kuwa Simba,Yanga,Mtibwa zikitokea Tanzania bara,na Tanzania Visiwani ni Malindi,Miembeni,Mafunzo na Ocean View.

Kwa mujibu wa Aljazeera fainali ya mashindano hayo ambayo yanalenga katika kuadhimisha siku ya mapinduzi zitafanyika tarehe 12 mwezi huu katika Uwanja wa Gombani huko Pemba na mgeni rasmi ni Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Aman Karume.


 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
wadau wa VOA waomwomboleza Simba wa Vita marekiani
kitabu cha maombolezo ya kifo cha Simba wa Vita kikiwa katika ubalozi wetu huko Washington
kocha mtangazaji wa Voice of America Alhaj Juma Nkamia akiweka sahihi ya maombolezo
Sunday Simba Shomary wa VOA akiweka sahihi yake
kocha na sunday wakiwa na balozi wetu Marekati, Mh. Ombeni Sefue
Sunday akiwa na afisa wa ubalozini Suleiman Saleh baada ya kutoa rambi





 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 6
HAPPY NEW YEAR FROM DOLPHINS
LET'S GIVE DOLPHINS SEA AND AIR LTD A BIG TOAST
A NEW YEAR WITH NEW PRIDE
IN AN AGENT WHO SERVES YOU WITHIN YOUR TIME AND BUDGET
dolphinstz@yahoo.com
www.dolphinstz.com
 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
SHUKURANI

MAJ. PERFECT ANTHONY SHAYO
25/08/1955 – 23/11/2009

Sisi Familia ya Shayo, tunapenda kuwashukuruni nyote kwa upendo wenu, kwa kushirikiana nasi tangu mlipopokea taarifa ya kifor cha baba yetu mpendwa, Maj. Perfect Anthony Shayo kilichotokea Hospitali ya Muhimbili tarehe 23/11/2009 na kuzikwa (Kimaroroni – Kilema) Moshi, Mkoani Kilimanjaro tarehe 27/11/2009.

Tunawashukuru kwa kutukimbilia nyumbani na kutoa salam zenu za rambirambi na kushiriki kwa hali na mali katika maandalizi na mazishi yake.

Tunamshukuru Dr. Kisanga na Wafanyakazi wote wa Hospitali ya Muhimbili. Dr. Green wa Hospitali ya Temeke. Uongozi wote na Wafanyakazi wa JWTZ. Viongozi, wafanyakazi na waumini wote wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) – Kurasini. Uongozi na waumini wa Parokia ya Mtakatifu Maurusi – Kurasini. Parokia ya Mtakatifu Bernadeta Kilema – Moshi. Viongozi na wanajumuiya wote wa Jumuiya za mtaa wa Mtoni na Sabasaba, Jumuiya ya Mtakatifu Benedict. Majirani zetu wote wa Mtoni Dsm na Kilema Moshi. Ndugu jamaa na marafiki zetu wote ambao mlishiriki nasi kikamilifu katika kuomboleza, kuandaa na kushiriki katika kufanikisha mipango ya mazishi ya Baba yetu mpendwa hapa Dar es Salaam na Moshi – Kilema.

Tunapenda kumshukuru kila mtu na kumtambua binafsi. Hatuna maneno zaidi ya kuelezea vya kutosha jinsi tulivyoguswa na upendo wenu mioyoni mwetu, tunachoweza kusema ni Asanteni Sana. Tulifarijika sana kwa upendo wenu na kushiriki nasi katika kipindi hicho kigumu tulichopita.
Mungu awabariki nyote.

Misa ya Kumuombea Marehemu Baba yetu mpendwa itafanyika Jumamosi tarehe 9/01/2010. Saa nne Asubuhi, Nyumbani kwake Mtoni kwa Azizi Ally.

TUNAMUOMBA MWENYEZI MUNGU AIWEKE ROHO YA MAREHEMU PERFECT ANTHONY SHAYO MAHALI PEMA PEPONI.
AMINA.
 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 1
video ya gemu la ivory coast na taifa stars jana
Ankal Mechoodhe,
Kuna video mbili japo kiduuuchu hivi zinazoweza kuwapa watu ladha ya ulivyokuwa mtanange wa kabumbu la jana. Linki hii hapa:
http://bit.ly/5zSvt4
Tunamshukuru Dk. Tonny aka Spika, kwa kuturekodia.
Subi
 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 9
tafsiri ya wimbo mamou wa franco lwanzo makiadi

 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 7
hitma ya simba wa vita london

FAMILIA , NDUGU , JAMAA NA MARAFIKI, WANA WAALIKA WATU WOTE KUHUDHURIA KISOMO CHA HITIMA YA BABA YETU SIMBA WA VITA , HAYATI RASHID MFAUME KAWAWA.

ITAFANYIKA :ST ANNES MOSQUE-ST ANNES ROAD

TOTTENHAM,
LONDON N15 5QG
JUMAMOSI JANUARI 9, 2010
SAA: 9 JIONI
KWA TAARIFA ZAIDI WASILIANA NA :
SHABANI KAWAWA
TEL: +44 07731802787
AHSANTE

NEAREST STATION : SEVEN SISTERS STATION
BUSES:341,29,141,341,67
 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
Taifa Stars yafungwa nusu bila??




nadir haroub canavaro alikuwa na kazi moja tu, kumkaba drogba asifurukute
kipa mwalami wa Taifa Stars akitahayari baada ya drogba kupiga bao, kisha kujiangusha na kujifanya kaumia. aliamka na kuendelea na gemu mtangazaji mahiri wa mpira wa TBC 1 Chacha Maginga (kuumeni) akiwa na mchezaji wa Yanga wa zamani aliye masomoni kusaka nondozzz Ali mayai wakichambua mchezo kama karanga

Ankal,
Hii taarifa ya Globu ya Jamii juu ya gemu la leo haiko sahihi. Ukweli ni kwamba Taifa Stars leo imefungwa nusu bila.

Kituko cha leo ni kwamba Taifa Stars imecheza na timu mbili tofauti
zote zikijiita timu ya taifa ya Cote d'Ivoire. Kikosi cha kwanza
(akiwemo Drogba) kilishinda 1-0, halafu ngwe ya pili kikaja kikosi
kingine kipya kabisa cha ma-underground kikatoka kapa.

Naomba kuwakilisha.
Mdau FM

 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 11
kamala na vaileth wameremeta kiaina
Vijana wa Agape Evangelical Singers wikiendi ilopita walikuwa na harusi moja ya kitamaduni ya mwenzao mdau Kamala James Lutatisinibwa na mai waifu wake Vaileth Ajuna Magezi.
Kwa kuwa vijana wengi wanadhani harusi ni lazima uwe na ma milioni, tunataka waone mfano huu. Harusi hii ilikuwa ni ya kipekee sana haijawahi kutokea na gharama yake ilikuwa chini ya laki tisa.

mchungaji Ernest Kadiva akiwameremetesha maharusi katika kanisa la Azania front

maharusi na wapambe pamoja na wasindikizaji
maharusi na wapambe wao
waalikwa wakifurahia champeni ya asili ya madafu
bendi ya agape ilitumbuiza
mchungaji Kadiva na maharusi wakiwa meza kuu iliyokuwa ya vigoda na jamvi

 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 28
saba wapanda daraja goju ryu karate dar usiku huu
Sensei Alfred Malekia akiwaelekeza watoto nini cha kufanya. Sensei Malekia, ambaye ni kiongozi wa dojo (shule ya karake) ya Tanzania Goju Ryu Karate-Do inayotumia mtindo wa Jundo Kan-Kuroobi Kai (badala ya Jundo Kan Shibu) ya Okinawa, Japan, inaendeleza libeneke la sanaa ya kujilinda kwa mikono mitupu katika ukumbi wa shule ya msingi ya Zanaki kila siku jioni. Leo hii wanafunzi watano wametunukiwa mikanda myeusi shahada ya kwanza na wawili wametunukiwa mikanda ya kahawia katika sherehe fupi zilizofanyika hapo dojo usiku huu. Sensei Malekia amesisitiza umuhimu wa vijana na watoto kujiunga na mazoezi hayo ambayo humlea mwanafunzi kuwa na nidhamu ya hali ya juu katika jamii.
watoto wakicheza kata ya kwanza ya Goju Ryu
Francis Kabika Sizya anaachana na mkanda wa kahawia na kuvalishwa mweusi baada ya kufuzu
Said Seleman Saleh akivishwa mkanda wa kahawia na kuachana na wa kijani baada ya kufuzu
Sensei Mbezi akimvisha Gaston Peter Minja mkanda wa kahawia
Sensei Rashidi Almasi akimtunuku Nicolaus Melkior Kalambo mkanda mweusi
Omary Emily Gregory akivalishwa mkanda mweusi
wahitimu ya mkanda mweuzi wakicheza kata
wahitimu wa mkanda mweuzi wakijifua na 'mae geri katika squatting position'
vingunge wa dojo la zanaki hivi sasa
wahitimu wa mikanda myeusi na kahawia wakipozi na viongozi wa dojo
wahitimu wa mikanda myeusi katika posi na viongozi wa dojo












 
© Michuzi | Tuesday, January 05, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 6
Monday, January 4, 2010
Tanga kunani paleeee???
Michuzi,
Heri ya Mwaka Mpya ankal,
Nakutumia taswira ya kiota kipya cha maraha cha Tanga, al-maarufu kama Tanga Beach Resort. Kipo maeneo ya Raskazone, mjini Tanga. Yaani usipime!

Mdau Lilly
 
© Michuzi | Monday, January 04, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 9
Rais Zuma ameremeta kwa mara ya tatu, mke wa tano
Rais Jacob Zuma akiwa na mai waifu wake mpya Tobeka Madiba wakilisakata javu la Kizulu leo huko jimbo la Kwazulu Natal
Bi harusi na wapambwe wakiwasili sehemu ya tukio

bwana harusi akijimwayamwaya kwa furaha ya kupata kitu kipya. bahati mbaya alijikwa na kula mweleka. ila mzee mzima hakuumia


maharusi wakiimba nyimbo za kizulu










 
© Michuzi | Monday, January 04, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 74
libeneke la youtube: Kunradhi kwa kwikwi...
Kunradhi wadau watukufu wa Globu ya Jamii,
Pamoja na hamu na jitihada ya kuendeleza libeneke la video lakini kwikwi ya spidi ya mtandao bado inafanya kazi iwe na changamoto kubwa kiasi hata inalazimu tupunguze ukubwa wa saizi ya video na kuambulia chenga-chenga.
Video ya Ivory Coast na Taifa Stars iko tayari lakini inapanda taratiiiiiiiibu hadi inakera. Hivyo wadau na tuvumiliane, nia ni nzuri tu lakini vitendea kazi iko jaa kwikwi dani yake.
Fibre Optic inaendelea kusambazwa kila sehemu ila haijakamilika kiiiivyo hivyo bado mtandao sehemu nyingi ni mwendo wa jongoo. Ukikaa sawa tu libeneke litanoga na inshaalla sio mbali sana toka leo!
 
© Michuzi | Monday, January 04, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
IVORY COAST YAISHINDA TAIFA STARS 1-0 KWA SHIIIDA

Benki ya NMB ilileta burudani ya aina yake
promo za wafadhili kwa kwenda mbele
vuvuzella ndani ya nyumba
Tajania oyeeee!

Kocha wa makipa Juma Pondamali akiwa kazini
Ivory coast wakipiga jalamba
Marcio Maximo na vijana wake
Nahodha wa Taifa Stars Nsajigwa akibadilishana bendera na nahodha mwenzie Didier Drogba wa Ivory Coast
Shilingi inarushwa kuchagua upande wa kuanzia
waamuzi na manahodha na wasimamizi katika taswira ya pamoja ya kumbukumbu
Ivory Coast
Taifa Stars
Juu na chini ni mlinzi wa Taifa Stars Nadir Haroub 'Canavaro' akimdhibiti Didier Drogba wa Ivory Coast wakati wa mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliomalizika muda mfupi uliopita. Ivory Coast walishinda kwa bao lile lile moja lilofungwa na Drogba dakika ya 39. Hata hivyo Taifa Stars, iliyokuwa ikishangiliwa kwa nguvu na mamia ya washabiki wakiongozwa na JK aliyekuwapo uwanjani, wanastahili kila aina ya sifa kwa kuweza kuwamudu Ivory Coast. Canavaro alimzima kabisa Drogba sema walijipanga vibaya wakati Emerse Fae alipochoropoka na kuporomosha majalo
















 
© Michuzi | Monday, January 04, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 27
mpaka sasa ivory coast yaongoza kwa bao moja
Timu ya Taifa ya Ivory Coast mnamo dakika ya 39 imezitikisa nyavu za timu ya Taifa Stars, mfungaji akiwa ni Didier Drogba wa Chelsea kwa kichwa baada ya kuunganisha majalo ya Emerse Fae.
Kwa uhondo zaidi wa picha na video vuta subra kidoogo.
 
© Michuzi | Monday, January 04, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 6
marcio maximo talks to us

Exclusive interview between Jamii Blog and Taifa Stars coach on Tanzania's soccer development plans

 
© Michuzi | Monday, January 04, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 21
Msaada kwenye tuta: skuli ya English Medium inasakwa
Ankal,

Heri ya mwaka mupya? Salaam kwa wadau wote wa globu ya jamii pia.

Naomba msaada kwenye tuta. Natafuta shule ya msingi ya English Medium
kwa ajili ya mwanangu. Ni mtoto wa kike, ana miaka 8, mwaka huu wa
2010 anaingia darasa la tatu.

Shule iwe Dar, Arusha, Mbeya, Morogoro, Dodoma, Bagamoyo au Kilimanjaro.

Hivi sasa yuko kwenye shule moja ya English medium hapa Dar sema
kinachoniuzi ni kwamba kila baada ya miezi mitatu wana likizo hivyo
mtoto anarudi nyumbani (ambako huwa hasomi). Nataka shule ambayo mtoto
akienda kurudi ni baada ya miezi sita.

Wadau mnaojua shule za English medium katika maeneo yaliyotajwa hapo
juu naomba mnisaidie majina na namba za simu. Kama namba ya simu huna
basi jina tu sio mbaya.

Asanteni.

Wenu mdau.
 
© Michuzi | Monday, January 04, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 41
kero bin karaha
Brother Michuzi,
Naomba niwekee kilio changu kwenye Blog yetu tukufu, please. Asante

Ilikuwa majira ya asubuhi wakati vijana wa shirika la maji Dares salaam walipokuja kwetu kwa madai ya kusafisha mita ya maji. Tupo Magomeni mapipa barabarani katika kituo cha daladala cha kuendea Kariakoo, tunalitumikia taifa kwa kazi ya kulisha chakula , SEABOYS FAST FOOD sehemu nadhifu inayopendwa na wengi na ni pasafi kiasi cha kwamba hatujapata malalamiko kutoka kwa ma-bwana afya.
Vijana wa dawasco baada ya kufika na supana zao waling'oa mita yetu ya maji na kuondoka nayo. Muda si mrefu walikuja na mita ingine (ambayo kumbe siyo ile yetu ya zamani ) na kuipachika pale na mda huo huo wakadai kwamba tunatakiwa tulipe bili ya maji ya LAKI 7 wakati bili yetu ya maji ya mwezi huo ilikuwa laki 180 na ambayo tayari computer zao zinaonyesha ya kwamba tumekwisha lipa.
Uzuri ni kwamba risiti zote za maji za miaka kadhaa ya nyuma tunazo na daima tuko mbele kulipa bili zetu.Hiyo mita waliyotupachikia ilikuwa tayari inasoma unit zilizotumika kibao.
Hatukusita kuwauliza, jamani hii bili ya laki 7 ni ya mwezi gani ??. mpaka hivi sasa naandika barua hii, hatuna maji,yaani walitukatia pale pale. Tuna endesha restaurant katika mazingira magumu.
Ndugu zangu na binadamu wenzangu tunaompenda Mungu na tunaokwenda misikitini na makanisani kusali, swali langu kwenu ni hili JE ?? HUU NI UUNGWANA ?? naomba barua yangu hii iwafikie wapenzi wote wa haki za binadamu.
Tusaidiane kuukemea unyama huu ambao sisi kwa sisi tunaweza kila raia ana majukumu ya kuisaidia jamii. Namaliza kwa kuwatakia mwaka mpya wenye amani na furaha.
Mdau Ezekiel Zebedayo.
 
© Michuzi | Monday, January 04, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 33
didier drogba ni changamoto kwa wachezaji wetu
achilia mbali nidhamu ya hali ya juu pamoja na kutojiskia, didier drogba amekuwa changamoto kubwa kwa wachezaji wetu ya namna ya kuwa mweledi. hapa analindwa na ulinzi wake binafsi na alioandaliwa na wenyeji wakati wote.

 
© Michuzi | Monday, January 04, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
Sunday, January 3, 2010
ivory coast waanza kambi dar
wachezaji wa ivory coast baada ya dina la mchana
kila mtu alikuwa anahamu na drogba
nyota wengine wa ivory coast
baadhi ya wachezaji wa taifa stars. toka shoto ni nizar khalfani, nsajiwa na mrisho ngasa
Kocha wa timu ya Ivory Coast, VahidHalihodzic akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mchezo wao dhidi ya timu ya Taifa stars utakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa leo




Mchezaji wa timu ya Taifa ya Ivory Coast na Chelsea Didier Drogba akitoka kupata dina la mchana Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski jijini Dar ambako timu hiyo imefikia. Wacheaji wote isipokuwa mmoja tu, wanacheza soka la kulipwa nje ya nchi yao. Leo wameanza tizi neshno na kesho watakipiga na Taifa Stars. Leo askari walikuwa na adabu na kila mtu kafanya kazi yake bila zogo linalosababishwa na kutaka sifa kusiko msingi kwa badhi ya hawa askari wetu ambao wanapenda kutumia nguvu nyiiiingi na maarifa kiduchu..
Mchezaji wa timu ya Taifa ya Ivory Coast na Arsenal Emmanuel Eboue akisaini katika fulanazzz ya mtoto aliyefika kwenye Hoteli ya kilimanjaro Kempiski kuwaona wachezaji hao
Wachezaji wa timu ya taifa ya Ivory Coast kushoto Yaya Toure na kulia Bajari Kone.







 
© Michuzi | Sunday, January 03, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 25
lovely gamble's soundtrack

Lovely Gamble Soundtrack 'Hatakama' by Mkazuzu feat Spilla. the track was produced Josh @ Urban Pulse in conjunction with Mzuka label. the video was produced UrbanFilmz a B Magazine production studio. The movie features Steve Kanumba the Great and shot in London

 
© Michuzi | Sunday, January 03, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 5
nani wa kulaumiwa?
Mfanyabiashara ndogondogo akiuza ndizi katika eneo linalokatazwa kandokando ya barabara ya kuelekea hospitali kuu ya Mkoa wa Dodoma. Lakini kwa nyuma askari nao wakipita na hamsini zao, ingawa bango linalokataza biashara limeandikwa kuwa na amri halali..... Hapo sasa....

 
© Michuzi | Sunday, January 03, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 15
ajali dabo dabo mikese na ubena leo
dereva wa hii semi-trela alitaka kugeuza gari na kujikuta anakwama kwenye tifutifu na kuziba barabara sehemu za mikese mizani leo hii
lori la azania likiwa limeacha njia maeneo ya ubena nzomonzi mkoani morogoro jioni hii. hakuna aliyepoteza maisha na chanzo cha ajali hiyo haikuelezwa kwani dereva na wasaidizi wake walikuwa wakali walipohojiwa na mdau KAM wa Globu ya Jamii aliyeleta taswira hizi sasa hivi
mbele kidogo maeneo ya mikese mizani mdau KAM amekuta ajali ingine wakati magari ya mafuta kuvaana uso kwa uso. madereva na wasaidizi wao wote wamenusurika na wanauguza majeraha madogo madogo. chanzo cha ajali hakijajulikana







 
© Michuzi | Sunday, January 03, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 4
ujio wa drogba na ivory coast kero kwa wanahabari
naibu waziri wa habari, utamaduni na michezo mh. joel bendera akiwapoza wanahabari waliotaka kususia kukava ujio wa drogba na ivory coast usiku kuamkia leo uwanja wa ndege wa julius nyerere jijini dar baada ya askari kuwajia juu wanahabari na kuwazuia wasifanye kazi zao kwa sababu wanazozijua wenyewe.
huko nje ya fensi mashabiki walikuwa wanamsubiri drogba na wengie kwa hamu. waliambulia kumuona kiduuuuchu tena kwa mbali
wanahabari wakiwa wamesusia kukava ujio wa ivory coast baada ya kunyanyaswa na askari uwanja wa ndege
wanahabari wakiweka msimamo wa kususia baada ya askari kuwanyanyasa katika kukava ujio wa ivory coast. hakuna mpiga picha aliyepiga picha ujio huo.
katibu mkuu wa chama cha wapiga picha nchini, bw. selemani mpochi, alieleza masikitiko yake ka vitendo vya askari kunyanyasa wanahabari wawapo kazini kwenye ujio wa aina hiyo, na kuhoji kwa nini inakuwa hivyo wakati Rais Kikwete amekuwa mstari wa mbele kuhakikisha ujio wa timu hiyo unapewa uzito unaostahili ili kuitangaza Tanzania vyema.
habari kamili





 
© Michuzi | Sunday, January 03, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 2
mapacha walioungana wazaliwa zenji
Watoto Mapacha walioungana wakiwa na uzito wa kilo3 waliozaliwa katika mkesha wa Mwaka Mpya katika hospitali ya Taifa Mnazi Mmoja Unguja wakipelekwa kuhifadhiwa katika chumba maalum. Bahati mbaya mapacha hawa walifariki dunia leo katika hospitali hiyo. Mama yao yu buheri wa afya. Picha na mdau Othman Maulid Mapara
 
© Michuzi | Sunday, January 03, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 7
kutana na MC chitanda
MC Chitanda ni mmoja wa waendesha shughuli maarufu jijini Dar akiwa na staili ya peke ya viatu ambavyo anasema huagiza toka ureno maalum kwa kufanyia kazi
mambo ya 'abdul'
MC Chitanda kuwa karibu sana na ma-DJ ili shughuli iwe mswano
Yeye na wenzie unaweza kuwapata katika libeneke la harusi




 
© Michuzi | Sunday, January 03, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 8
KUMBUKUMBU
MUTARAGARA CHIRANGI – ‘RUBHOJA BHANU’

Tarehe 03, Januari, 2010 inakamilisha takribani miaka mitatu tangu ututoke ghafla. Familia yako na Wanahistoria tunaendelea kukukumbuka kwa mengi uliyotufundisha kwenye njanja mbalimbali katika Uongozi, Uadilifu na Wema wako.

Katika kumbukumbu hii, dhamira zetu leo zinaguswa zaidi na tabia yako isiyokifani ya

UKARIMU ULIOKUWA NAO KWA WATU WOTE PASI KUJALI MAKABILA, ITIKADI ZA KISIASA, IMANI, JINSI, UMRI WALA HALI ZAO ZA KIUCHUMI.

Aidha haikuwa ajali Wanadamu wakati wa ujana wako wakakupa majina ya utani kama vile Rubhoja Bhanu na pia Nyamulila Mwirango utambulisho ulioashiria tabia hii ya kukarimu watu uliyoionyesha kwa vitendo pasipo uzandiki wala masharti kwa manufaa binafsi.

Tunamuomba Mola azidi kutukumbusha nasi leo kuwakarimu wageni na wahitaji kwa jinsi tunavyoweza kuwasaidia maana kwa kufanya hivyo si tu kuwa tutakuwa tunaenzi kauli mbiu

uliyoipenda ya Haki Huinua Taifa bali pia tutakuwa tunawajibika kuwasaidia wenzetu wenye mahitaji mbalimbali kama tunavyotakiwa katika kujali utu na haki za kila Binadamu.

KWA HESHIMA NA SHUKRANI,
FAMILIA YA CHIRANGI INAWASILISHA.
http://hakihuinuataifa.blogspot.com/
 
© Michuzi | Sunday, January 03, 2010 | Permalink | Mtumie Rafiki Yako | Maoni 13


Idadi ya watu
Idadi ya watu
eXTReMe Tracker