THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY' Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.

  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 2647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 2647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com






DC MAKETE ASOMA TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA SERIKALI WILAYANI MWAKE

 Mkuu wa wilaya ya makete Mh. Josephine Matiro akisoma taarifa ya utekelezaji wa shughuli za serikali wilayani hapo kwa kipindi cha Januari-Aprili 2013 katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Makete.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA


Mjadala wa waTanzania UK Kufanyika University of Reading

Siku ya Jumamosi tarehe 01/06/2013, waTanzania waishio UK watakutana kwa ajili ya mjadala mkubwa utakaohusu maswala yafuatayo: Elimu; Katiba;Muungano; na Utaifa. Mjadala utafanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa University of Reading


Hii ni nafasi ya kipekee kwa waTanzania kuzungumzia mambo muhimu yanayoihusu jamii yetu bila kujali itikadi, imani, rangi au kitu kingine chochote. Vikundi mbali mbali vya kidini, kisiasa na kijamii vitakuwepo.

Japokuwa mjadala unafanyikia UK, waTanzania wote wenye nia ya kushiriki kutoka mahali popote pale duniani wanaweza na wanakaribishwa kushiriki. Kama ungependa kushiriki kutoka sehemu yoyote ulipo, unaweza kufanya hivyo kwa kupitia tweeter account itakayotolewa hivi karibuni.

Mjadala utarushwa kwenye YouTube channel. Pia kwa hisani ya Funguka Forums mjadala utakuwa unarushwa live kwenye fungukaforums.com. Pia updates zitakuwa zikitolewa kwa kupitia facebook na twitter.

Karibuni wote tushiriki kwa mapenzi ya nchi yetu.

“Usiulize Tanzania imekufanyia nini. 
Jiulize wewe umeifanyia nini nchi yako. “


john mashaka on Tanzania's Agriculture & the Balance of Payment

Agriculture has bankrolled Tanzanian economy for a long time, contributing as much as 27.8 per cent of the gross domestic product (GDP).It remains potentially the most lucrative sector of the economy. The lingering question is whether the sector can alleviate Tanzania’s economic burden by offsetting the current negative balance of payment. 
 With the nation at Sh22 trillion in debt, offsetting balance of payments (BoP) could be a tricky one, unless each and every able individual engages in productivity. The agricultural sector seems to be the only viable option that can employ every able bodied individual. Tanzania has vast arable land, which is rapidly falling in the hands of foreigners engaged in farming not for the benefit of the local economy, but rather, to provide raw material for their industries and food security for their people.
After independence, Tanzania became a manufacturing hub. Cotton farmers had a ready market for their produce. Textile mills - Mwatex, Sunguratex and the like - created thousands of jobs to urban dwellers and were a source of steady income for farmers in rural areas. The surplus raw material was processed and exported to foreign markets. 
 Today, all the textiles and cotton processing factories are literally gone while large-scale cotton farming has been abandoned because farmers have no motivation to work. In the sixties and seventies, Tanzania’s economic potential was much higher than that of many nations in the red-hot economies in Asia such as South Korea, Singapore, Vietnam, Malaysia and others. 
 In contrast, Tanzania is three times the size of Vietnam with only 45 million people while the Vietnam population stands in excess of 88 million. Vietnam recorded a current account surplus of $246 million in 2012 while Tanzania recorded $250 million deficit in the same year. Why such a huge contrast when Tanzania has much more potential than Vietnam? Beginning in the 1990s, the Vietnamese government launched a special program, which elevated the country’s agricultural standing to higher heights making it the world’s leading rice producer and exporter. In 2010, Vietnam broke the barrier and became the largest rice producer. 
 The new policy became so successful that Vietnam eliminated internal food scarcity and today has plenty to export. Agriculture contributes 22 per cent into Vietnamese GDP. Agriculture has revolutionized the country’s economy, following the footsteps of giants such as South Korea in becoming a global manufacturing hub.
 Vietnam processes its own agricultural produce, and only exports finished products, a move that has kept unemployment at 4.3 per cent and inflation at 4.5 per cent. In Tanzania, rural farmers are suffering extreme bouts of apathy and are no-longer motivated to carry on large scale farming. This is because they lack sufficient and organized markets for their produce. They lack capital, farm inputs, and an infrastructural base that would enable them access both domestic and foreign markets. 
 Elsewhere, tiny Netherlands is racking-in $79 billion annually from agriculture. Ironically, Tanzania’s agricultural potential is well over $90 billion, dwarfing both the Netherlands and Brazil.Tanzania has the potential to feed itself, the entire sub-Saharan Africa, and parts of Europe Sadly, Tanzania is importing tainted rice, receiving spoilt maize as humanitarian assistance when it has millions of hectors either idle or leased to foreign entities. 
 The country is also importing contaminated fish from Japan, yet cargo-planes are loading tonnes of fresh fish from Mwanza to Eastern Europe at a throw away price. Tanzania dairy farmers are selling milk cheaply to some neighboring countries that process it and then bring it back into our domestic market as processed dairy products at a higher price.
 Tanzania need an agricultural revolution that will ensure only processed and finished agricultural-products are exported. Not raw-products that fetches almost nothing in the world market. The revolution must provide tax incentives to farmers and companies that engage in export To correct the current balance of payment through agriculture, the government must design a revolutionary blueprint, by providing research, technical, financial and farming input assistance to farmers. 
It must help agricultural traders secure entry into the global market. Quarter System is needed on importation of food and agricultural products to boost local innovation and productivity. 

Mungu Ibariki Tanzania 
 John Mashaka
 mashaka.john@yahoo.com


MKATAA KWAO MTUMWA

Leo tuburudike na ngoma ya asili ya Wanyanyusa wa Mbeya


ngoma azipendazo ankal

LEKA DUTIGITE NA KIGOMA ALL STARS NI NOMA!


JIANDAE NA KIJIWE CHA UGHAIBUNI BAADAYE LEO JUMANNE MAY 21


 Leo Jumanne May 21, 2013 kipindi chako ukipendacho KIJIWE CHA UGHAIBUNI kitakuwa hewani kama kawaida. Pichani  wanakijiwe wakiwa kwenye kipindi kwa ajili ya kurekodi. kutoka kushoto ni Benja Mwaipaja, msanii wakucheza na nyoka, Salma Moshi, Eliza Luhanga na Yasin Randi.
 Eliza na Yasin wakichangia jambo kwenye Kijiwe kitakachorusha baadaye leo Jumanne.
Benja na Salma Moshi wakilumbana kwenye Kijiwe Leo ndio Leo wakina baba wamekabwa koo na akina mama wameshindwa kufurukuta imebidi wakimbie kipindi USIKOSE


shukurani


Familia ya Bw. Thomas Martin Kiama wa Bongoyo, Oysterbay, Dar es salaam  tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwenu ndugu, jamaa, marafiki, wachungaji, madaktari, wauguzi na wote wenye mapenzi mema kwa moyo wa upendo na kujitoa kwa hali na mali katika kipindi chote cha kumuuguza hadi pale Mungu alipoamua kumtwaa Mama yetu kipenzi, Victoria Thomas Kiama tarehe 11.05.2013 na tukampumzisha tarehe 14.05.2013 katika Makaburi ya  Kinondoni.
Ni vigumu kumshukuru kila mmoja binafsi, hivyo kwa moyo mkunjufu tunawaomba mpokee shukrani zetu za dhati. Mungu wa Mbinguni awabariki.
Tunamshukuru Mungu kwa muda wote aliotupatia wa kuishi naye hapa duniani. Bwana Mungu alitoa, naye ametwaa, Jina lake libarikiwe milele na milele. 

Amina.




WAREMBO WA REDD'S MISS KIGAMBONI 2013 WAJIANDAA


Warembo wanaoshiriki shindano la Redd's Miss Kigamboni wakiwa kwenye mazoezi kwa ajili ya kujiandaa na kinyang'anyiro hicho kitakachofanyika Ijumaa Juni 7 mwaka huu kwenye ukumbi wa Navy Beach ulioko Kigamboni jijini Dar es salaam. 


RAIS KIKWETE AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KATIKA MAZISHI YA MZEE ALLY KLEIST SYKES JIJINI DAR LEO

  Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Makamu wa Rais Dkt Mohamed Ghalib Bilal, Marais wastaafu Alhaj Ali Hassan Mwinyi na Mzee Benjamin William Mkapa,  Mawaziri Wakuu wastaafu Jaji Joseph Sinde Warioba na Dkt Salim Ahmed Salim, Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana, Mzee Kingunge Ngombale Mwiru na viongozi wengine wakiungana na mamia ya waombolezaji katika mazishi ya Mzee Ally Kleist Sykes, mmoja wa waasisi wa chama cha TANU katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam leo Mei 20, 2013.
  Rais Jakaya Mrisho Kikwet akiongoza mamia ya waombolezaji katika mazishi ya Mzee Ally Kleist Sykes, mmoja wa waasisi wa chama cha TANU, leo katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam leo Mei 20, 2013.PICHA NA IKULU


Maalim Seif na Fatma Fereji wakutana na mkuu wa brigedi ya nyuki Zanzibar leo

Na Hassan Haamd
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, amevitaka vyombo vya ulinzi nchini kusimamia vyema majukumu yake ili kuhakikisha kuwa bahari na mipaka ya nchi inakuwa salama. Amesema Zanzibar ikiwa nchi ya visiwa, inakabiliwa na changamoto moto nyingi za kiulinzi na usalama kuhakikisha kuwa magaidi hawaingii nchini, sambamba na kukabiliana na vitendo vya uharamia na usafirishaji wa dawa za kulevya. 
Maalim Seif ameeleza hayo ofisini kwake Migombani alipokuwa na mazungumzo na Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Brigedia Jenerali S S Othman. Amesema katika siku za hivi karibuni kumekuwa ni tishio la vitendo vya kigaidi katika Pembe ya Afrika, jambo ambalo linapaswa kuzingatiwa ili vitendo hivyo visije kuiathiri Zanzibar. 
“Suala la ulinzi halina mbadala, kitu cha msingi ni kwa vyombo vya ulinzi na dola kushirikiana kuhakikisha kuwa nchi iko salama kwa maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla”, alisisitiza Maalim Seif. 
Kuhusu vitendo vya uharamia vinavyofanywa katika bahari ya hindi, Maalim Seif amesema vinaathiri shughuli za kibiashara na uchumi na vinastahiki kupigwa vita kwa nguvu zote. 
Kwa upande wake, Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Brigedia Jenerali S S Othman, amesema suala la ulinzi ndio jukumu la msingi kwa vyombo vya ulinzi, na kuahidi kushirikiana na vyombo vya dola na wananchi katika kutekeleza jukumu hilo kwa ufanisi zaidi. 
Jererali Othman ambae pia ni Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na usalama Zanzibar, amesifu mashirikiano anayoyapata kutoka kwa viongozi wa nchi na watendaji wengine katika kufanikisha jukumu hilo la kiulinzi. Jererali Othman pia amekutana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, Fatma Abdulhabib Fereji na kubadilishana mawazo juu ya majumu ya ofisi hiyo. 
Waziri Fereji amesema katika kukabiliana na majukumu ya ofisi hiyo, wanahitaji mashirikiano ya karibu na vyombo vya ulinzi katika kukabiliana na na vitendo viovu vikiwemo udhalilishaji wa watu wenye ulemavu, uchafuzi wa mazingira na matumizi ya dawa za kulevya. Amevishauri vyombo vya ulinzi kujiimarisha zaidi ili kuweza kukabiliana na makundi ya kihalifu yakiwemo yale yanayojihusisha na uchimbaji wa mchanga kinyume na utaratibu.
 “Ukweli ni aibu kusema kuwa jeshi la polisi linashindwa kuwakamata wachimbaji wa mchanga kwa sababu wana pamanga na marungu au mawe, wakija wakiamua kuingia barabarani je mutawafanyaje?”, alihoji Waziri Fereji.
 Kuhusu UKIMWI, Waziri Fereji amesema licha ya kuwa kiwango cha maambukizi bado ni chini ya asilimia moja, lakini athari kubwa inajitokeza kwa makundi hatarishi likiwemo lile linalojihusisha na biashara haramu ya ukahaba.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akisalimiana na Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Brigedia Jenerali S S Othman, alipofika ofisini kwake Migombani.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Brigedia Jenerali S S Othman, alipofika ofisini kwake Migombani.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais  Zanzibar, Fatma Abdulhabib Ferej, akizungumza na Mkuu wa Brigedi ya Nyuki Zanzibar, Brigedia Jenerali S S Othman, alipofika ofisini kwake Migombani. Picha na Salmin Said, OMKR


NSSF YASHINDA KOMBE KATIKA MAONESHO YA KIBIASHARA YA KIMATAIFA JIJINI TANGA


Mrs Eunice Chiume, Meneja Kiongozi wa Uhusiano na huduma kwa Wateja mara baada ya kukabidhiwa Kikombe cha Ushindi wa Kwanza katika kundi la Utoaji Huduma Kwa Jamii, Kutoka kwa Mhe. Dr. Abdallah Kigoda, Waziri wa Viwanda na Biashara katika Maonyesho ya Kibiashara Ya Kimataifa ya Tanga, mjini Tanga.

 Baadhi ya watu waliofika katika banda la Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) wakipata huduma mbalimbali za zinazotolewa na Shirika hilo.
 Huduma za Afya zikitolewa.
Ofisa Mwandamizi Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Theopista Muheta akitoa maelezo kwa wakazi wa jiji la Tanga waliofika katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa kwenye viwanja vya Tangamano 
 Meneja Kiongozi Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Eunice Chiume, akitoa maelezo kuhusu shughuli za NSSF kwa Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dk. Abdallah Kigoda,alipotembelea banda la NSSF katika Maonyesho ya Kibiashara Ya Kimataifa yanayofanyika jijini Tanga.
Meneja  Kiongozi  Uhusiano na Huduma kwa Wateja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF),  Eunice Chiume (kushoto) akitoa maelezo juu ya huduma za shirika hilo wakati  wa maonesho ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika kwenye viwanja vya Tangamano jijini Tanga.


soma simulizi ya kusisimua kutoka kwa mtunzi Adela kavishe.

UKITAKA KUISOMA RIWAYA HIYO KWA KINA

 INGIA 


HADIJA SAID AIBUKA MSHINDI WA TAJI LA MISS UTALII TANZANIA 2012/13 KITAIFA

MSHINDI WA TAJI LA MISS UTALII TANZANIA 2012/13 HADIJA SAID MISS UTALII MOROGORO  KATIKATI AKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA LUCY NOEL MISS UTALII DAR ES SALAAM KUSHOTO NA MSHINDI WA TATU KULIA THELESIA KILOMO MISS UTALII VYUO VIKUU.
 MSHINDI WA TAJI LA MISS UTALII TANZANIA 2012/13 HADIJA SAID MISS UTALII MOROGORO AKISHWA TAJI LA USHINDI NA MGENI RASMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI KANALI MSTAAFU CHIKU GALAWA,MKUU WA WILAYA YA TANGA HALIMA BENDEGO

 KUTOKA KUSHOTO NI MISS UTALII KUTOKA MKOA WA KATAVI ASHA RAMADHANI ALIYE SHINDA NAFASI YA NNE, LUCY NOEL MISS UTALII DAR ES SALAAM ALIYESHINDA NAFASI YA PILI, MISS UTALII MOROGORO HADIJA SAID AMBAYE NDIYE MISS UTALII TANZANIA 2012/13, MISS UTALII VYUO VIKUU THERESIA KILOMO
 KUTOKA KUSHOTO NI MISS UTALII KUTOKA MKOA WA KATAVI ASHA RAMADHANI ALIYE SHINDA NAFASI YA NNE, LUCY NOEL MISS UTALII DAR ES SALAAM ALIYESHINDA NAFASI YA PILI, MISS UTALII MOROGORO HADIJA SAID AMBAYE NDIYE MISS UTALII TANZANIA 2012/13, MGENI RASMI KWA NIABA YA MKUU WA MKOA WA TANGA LUTENI KANALI MSTAAFU CHIKU GALAWA,MKUU WA WILAYA YA TANGA HALIMA BENDEGO ,MISS UTALII VYUO VIKUU THERESIA KILOMO NA MISS UTALII SINGIDA MWAKOMBO KESSY ALIYESHINDA NAFASI YA TANO



 WASHIDI WA TANO BORA WAKIWA KATIKA PICHA YA PAMOJA NA VIONGOZI WA SERIKALI MKOA WA TANGA.



haja ya hoja

Mshindi ni simba, mara ya mwisho alimfunga Yanga 5-0. Kwa kuwa mechi iliyofuatia baada ya ile ilikuwa 1-1, kwa matokeo ya Jumamosi matokeo ya jumla (aggregates) itakuwa 3-0. kama hujui mahesabu mjomba, pole


Shamim Mohamed anyakua taji la Redd's Miss Mzizima 2013

 Redd's Miss Mzizima 2013,Shamim Mohamed (kati) akipunga mkono muda mfupi baada ya kutangazwa kuwa mshindi wa taji hilo katika shindano lililofanyika kwenye Ukumbi wa Lamada jijini Dar es Salaam,mwishoni mwa wiki.Wengine pichani ni Mshindi wa Pili,Munira Mabrouk (kulia) pamoja na Mshindi wa Tatu,Rehema Mpanda.
 Warembo wa Redd's Miss Mzizima walioingia katika hatua ya tano bora,wakiwa wamejipanga kusubiri kupatikana kwa mshindi.
 Redd's Miss Mzizima 2013,Shamim Mohamed (kulia) akikabidhiwa hundi ya dola 450 kutoka kwa Mamaa wa Mitindo,Asia Idarous.
 Wacheza shoo wa Twanga Pepeta wakifanya mambo yao jukwaani. 
Waratibu wa Shindano la Redd's Miss Mzizima,Kushoto ni Sunday Mozzy pamoja na Osango wakipozi kwa picha.



news alert: MBUNGE MSIGWA NA WENZAKE 70 WAACHIWA KWA DHAMANA


Na Francis Godwin wa Matukio Daima Blog,Iringa

SAKATA la vurugu  za machinga na polisi mjini Iringa limechukua  sura  mpya  baada  ya  jeshi la  polisi mkoa wa Iringa  kumfikisha mahakamani mbunge  wa jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa pamoja na  watuhumiwa wengine zaidi ya 70

Huku mahakama   hiyo  ikitoa masharti nafuu ya dhamana kwa  watuhumiwa hao na  kuwaonya  kutofanya  kosa kwa  kipindi  chote  cha kesi  hiyo inapoendelea  kusikilizwa .
Watuhumiwa hao  walifikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi wa wilaya ya Iringa Mheshimiwa Godfrey Isaya  leo  majira ya saa 8 mchana  huku wakiwa  chini ya ulinzi mkali  wa askari  wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) waliokuwa na msafara  wa magari zaidi ya matatu  likiwemo  gari ya maji ya  kuwasha .

Mbali ya mbunge Msigwa  kupanda gari ndogo  ya  wazi ya  polisi pamoja na  watuhumiwa  wawili wanawake  waliokamatwa katika  vurugu  hizo bado  watuhumiwa  wengine zaidi ya 70  walitumia usafiri wa karandinga la polisi.

 Mbele  ya mahakama  hiyo  wakili  wa serikali  Adolph Maganda alisema  kuwa  watuhumiwa hao kwa pamoja  wanatuhumiwa kwa makosa matatu  likiwemo la kushiriki  mkutano na kufanya   vurugu ,uchochezi na kuharibu mali kinyume na sheria .

Huku mbunge  akisomewa mashitaka mawili likiwemo  kushawishi   na kufanya mkutano bila  kibali  .

Watuhumiwa  wote  wamekana  mashitaka  dhidi yao  huku  wakili  wa  serikali akidai  kuwa hana pingamizi na dhamana kwa  watuhumiwa hao wote ,hata  hivyo wote   wamekana  mashitaka  yote yaliyotolewa  dhidi  yao.

Hata  hivyo makimu anayesikiliza kesi  hiyo alisema kuwa dhamana kwa  washitakiwa  wote  ipo  wazi  kwa kila mmoja kuwa na mdhamini mmoja anayeaminika pamoja na kusaini hati ya dhamana  ya Tsh milioni moja .

 Hadi majira ya  saa 10 jioni mahakama  hiyo  ilikuwa ikiendelea na mchakato  wa  kupitia barua  za dhamana kwa  wadhamini  huku  mbunge akiwa  wa kwanza kudhaminiwa ,mbali ya  mbunge  watuhumiwa kati ya 74  waliokuwa  bado kupata  wadhamnini  ni  watuhumiwa  sita pekee.

 Katibu  wa chama cha Demokrasia na maendeleo (Chadema) wilaya ya Iringa mjini Suzana Mgonakulima alisema  kuwa  mchakato  wa  kuwadhamini  watuhumiwa  wote  waliosalia unaendelea kufanyika na kuwa wana uhakika wa  watuhumiwa  wote kudhaminiwa .

Hadi  majira  haya  ya saa 10 .40  jioni  wakati habari  hii inakwenda  mitamboni bado  mahakama  ilikuwa ikiendelea na umati wa wafuasi  wa Chadema  ukiwa nje  ya mahakama hiyo kusubiri watuhumiwa  hao kudhaminiwa .
 
Wakati  huo  huo  wananachi  waliofika  mahakamani hapo  kushuhudia mbunge  wao akifikishwa mahakamani  wamempongeza mkuu  wa  kikosi cha kutuliza ghasia mkoa  wa Iringa (FFU) Said Abdulah Mnunka  kwa kusimamia amani na utulivu katika  eneo hilo la mahakama na jinsi ambavyo alivyoweza  kupambana na machinga  pasipo kumwaga damu kwa  siku ya  jana wakati  wa vurugu  hizo


WAZIRI WA MAMBO YA NJE,MH. BERNAD MEMBE AKUTANA NA MABALOZI LEO JIJINI DAR LEO

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Benard Membe akiongea na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao nchini Tanzania leo jijini Dar es salaam alipokutana nao kujadili maandalizi ya mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano kwa manufaa ya Wote (Smart Pertinership) na mchango wao katika kuhamasisha ushiriki wa nchi wanazotoka katika mkutano huo utakaofanyika mwezi ujao. Kushoto kwake ni Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Juma - Alfani Mpango.
Meneja Mradi wa maandalizi ya mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano kwa manufaa ya Wote (Smart Pertinership) Rosemary Jairo akitoa ufafanuzi kwa mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao kuhusu maendeleo na maandalizi ya mkutano huo wa kimataifa utakaofanyika mwezi June jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo marais 10 kutoka nchi zilizoendelea.
Sehemu ya mabalozi wakifuatilia hatua mbalimbali za maandalizi ya mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano kwa manufaa ya Wote (Smart Pertinership) na mchango wao katika kuhamasisha ushiriki wa nchi wanazotoka katika mkutano huo. Zaidi ya washiriki 500 wanatarajiwa kwenye mkutano huo utakaojadili kwa kina matumizi ya Sayansi na Teknolojia katika kuleta Maendeleo kwa nchi zinazoendelea.
Meneja Mradi wa mkutano wa Kimataifa wa Majadiliano kwa manufaa ya Wote (Smart Pertinership) Rosemary Jairo akitoa ufafanuzi kwa mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao leo jijini Dar es salaam kuhusu maendeleo na maandalizi ya mkutano huo utakaohudhuriwa na wachumi, wanasayansi na viongozi mbalimbali wa serikali kutoka ndani na nje ya nchi.Picha na Aron Msigwa - MAELEZO.


MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHANI MSIBA WA MZEE ALLY SYKES JIJINI DAR LEO


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitia saini katika kitabu cha maombolezo ya msiba wa marehemu Ally Sykes, wakati alipofika kuhani msiba huo wa mwasisi wa TANU, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa leo jioni jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiaga na baadhi ya wazee waliohudhuria shughuli za msiba, wakati alipokuwa akiondoka baada ya kuhani msiba wa mwasisi wa TANU, Ally Sykes, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anatarajiwa kuzikwa leo jioni jijini Dar es Salaam.
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimfariji mjane wa marehemu Ally Sykes, Zainab Ally, wakati alipofika kuhani msiba huo wa mwasisi wa TANU, aliyefariki jana jijini Nairobi. Marehemu Sykes anazikwa leo jioni jijini Dar es Salaam.


baada ya kukipiga Azam na Simba,Mrisho Ngassa sasa arejea Jangwani

MSHAMBULIAJI Mrisho Ngasa amemwaga wino wa kuichezea klabu ya Yanga kwa dola 30,000 ikiwa ni mkataba wa miaka miwili. Habari zilizotufikia chumba cha habari cha Globu ya Jamii leo hii zimesema kuwa tayari uongozi wa Yanga umeshampa kitita cha dola 10,000 mshambuliaji huyo ambaye aliondoka kwa mbwembwe kwenda Azam kwa dau la milioni 50,000.

Chanzo hicho kimedai kuwa Ngasa bado anaidai klabu hiyo ya mtaa wa Jangwani kitita cha dola 20,000 ambacho aliahidiwa kukabidhiwa mara atakapotua rasmi ndani ya klabu hiyo.

Uongozi wa Yanga leo umemtambulisha rasmi Mrisho Ngasa kwa kurejea kundini baada ya kumaliza mkataba wake na Azam ambao walimpeleka kwa mkopo Simba ambako ametukimikia klabu hiyo ya wekundu wa Msimbazi kwa muda wa mwaka mmoja.

Akizungumza na waandishi wa habari Ngasa ambaye amekabidhiwa jezi iliyokuwa na jina lake na Katibu mkuu wa klabu hiyo Laurance Mwalusako alisema "Namshukuru Mungu kwa kuniwezesha kurudi tena Yanga, klabu ambayo nina mapenzi nayo toka utoto, nawashukuru viongozi wa Yanga waliofight hasa rais Kifukwe (Francis) kuhakikisha wananirudisha kundini.

"Nilipokuwa Azam, Simba nilicheza kwa uaminifu mkubwa lakini viongozi hawakuwa na imani na mimi kwa vile nina mapenzi na Yanga, ni kweli naipenda Yanga lakini hata siku moja sikucheza unazi, nilicheza kwa uaminifu kwa vile mpira ni ajira yangu, mapenzi yanafuata lakini viongozi hawakuliona hilo.

Kuhusu kusaini mkataba na Simba ambapo alipewa dola 25,000 pamoja na gari aina ya Verosa Ngasa alisema "Sina mkataba na Simba na sijawahi kusaini mkataba na Simba, mkataba wangu ni Azam na Azam walinipeleka Simba kwa mkopo.

Akifafanua jambo hilo, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga Abdallah Bin kreb alisema "Shilingi 25 milioni zilizotolewa na Simba ilikuwa ni ada ya kumtoa Azam kwenda Simba na gari alilopewa ilikuwa ni ushawishi tu ili akubali kucheza Simba klabu ambayo hakuwa na mapenzi nayo."

Alisema kama Yanga hawana kinyongo na mchezaji huyo ambaye aliitosa timu yao na kwenda kusaka maslahi Azam na kwa wapinzani wao na kwamba hata penati aliyoisababisha katika mechi dhidi ya wapinzani wao iliyochezwa Jumamosi na Yanga kuibuka na mabao 2-0 imedhihirisha uamifu wa Ngasa katika timu alizochezea.

Akizungumzia suala hilo, Mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba, Zakaria Hanspop alisema "Mkataba wetu na Ngasa upo wazi tena unasema wazi utaanza pale ambapo mkataba wake na Azam utakapomalizika, hatujaingia mkataba juu ya mkataba kama Yanga wanavyodhani.

"Yanga wamezoea fujo wanafanya mambo kama vile TFF ni mali yao wanajua watabebwa, kwanza wao ndio waliomwambia Ngasa sio mali kitu, ameshuka thamani wakati ule sisi tulitaka kutoa milioni 20 wao wakambiwa waongeze tano iwe 25,000 milioni ili wamchukue walikataa na kusema hana thamani ya hela hiyo imekuwaje sasa? alisema kwa kuhoji na kuongeza "Kuna watu wanampotosha Ngasa na tulishamwambia kabisa mchezaji mzuri lakini atajikuta anishia pabaya, sisi tutafuata sheria TFF ndio watakaoamua.


CRB yahamasisha makandarasi kushiriki mkutano mkuu

Msajili wa bodi ya makandarasi nchini (CRB), Eng. Boniface Muhegi (kulia) akisisitiza jambo alipokua akitangaza kuhusu mkutano mkuu wa majadiliano wa bodi hiyo unaotarajiwa kuanza alhamis ya wiki hii jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni msajili msaidizi, Utafiti na Maendeleo, Eng. Magesa Bairi (katikati) and msajili msaidizi wa bodi hiyo, Utawala na Fedha, Bw. Rhoben Nkori.

Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam

Bodi ya Usajili wa Makandarasi nchini (CRB) imewataka makandarasi hapa nchini kuhudhuria kwa wingi kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa majadiliano wa bodi hiyo unaotarajiwa kuanza alhamisi wiki hii jijini Dar es salaam.

Msajili wa Bodi hiyo injinia Boniface Muhegi ametoa wito huo mjini Dar es salaam jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maandalizi ya mkutano huo ambao kwa mwaka huu utaangalia kwa undani mafanikio na changamoto katika sekta ya ujenzi Tanzania miaka kumi na tano tangu kuanzishwa kwa bodi hiyo.

Amesema washiriki wa kada mbali mbali kutoka sekta ya ujenzi wanakaribishwa kwenye mkutano huo kwani mkutano huo utakuwa na manufaa makubwa kwao ikiwamo kusaidia kuwapandisha madaraja na kupata alama katika maendeleo ya fani yao.

Ameongeza kuwa washiriki kutoka nchi za Kenya,Uganda,na Rwanda wamealikwa ili kuweza kubadilishana uzoefu na washiriki wa ndani. “Tunahamasisha ushiriki wa wakandarasi toka sekta binafsi na umma,” alisemana kuongeza kuwa pia patakua na maonyesho ya huduma na vifaa mbalimbali vya sekta hiyo.

Amedokeza kuwa sekta ya ujenzi Tanzania imepiga hatua kubwa toka kuanzishwa kwa bodi hiyo miaka 15 iliyopita kwani kulikuwa na makandarasi wapatao 1000 kulinganisha na sasa ambapo kuna jumla ya makandarasi 7000.

Ametaja mafanikio mengine kuwa ni kuongezeka kwa ubora na uwingi wa kazi za ukandarasi wa ujenzi akitolea mfano ongezeko la minara ya mawasiliano ya simu za mkononi ambayo imetapakaa karibu nchi nzima, barabara na majengo ya kisasa. “Pamoja na vikwazo mbalimbali, tumepiga hatua kubwa,” alisema.

Pamoja na maendeleo hayo pia ametaja baadhi ya changamoto ambazo zitajadiliwa kwenye mkutano huo ikiwemo kujenga uwezo wa wakandarasi wazalendo, kutofuata kanuni na sheria mbalimbali.

Mada nne zitawasilishwa kutoka kwa wadau mbalimbali zote zikilenga changamoto na mafanikio katika sekta ya ujenzi Tanzania ndani ya miaka kumi na tano.

Mapendekezo ya mkutano huo yatapelekwa kwa wadau husika na baadae kufuatilia utekelezaji wake.

Pia mkutano huo utapitia utekelezaji wa maazimio ya mkutano uliopita ikiwepo la madeni ya makandarasi.

Takwimu zinaonyesha kwamba sekta ya ujenzi inachangia asilimia saba ya pato la taifa huku ukuaji wake kwa mwaka ikikadiliwa kuwa ni asilimia kumi na moja ikiwa ni sekta ya pili kwa kasi ya ukuaji huku sekta ya madini ikiongoza.

Asilimia sitini ya bajeti ya maendeleo nchini inakwenda kwenye sekta ya ujenzi huku asilimia themanini ya fedha hizo zikienda kwa wanachama wa bodi ya usajili wa mandarasi wa ujenzi.


CBE Dar na SAUT Mwanza mabingwa Safari Pool


  Nahodha wa timu ya Chuo cha St.Augustine (SAUT),Jimy Nikas akionyesha kitita cha sh.500,000 mara baada ya chuo hicho kutetea ubingwa wa mashindano ya Safari Lager Pool Higher Learning Pool Competitio 2013 Mwanza yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Villa Park.
Bingwa  wa mashindano ya Pool yajulikayo kama Safari Lager Pool Higher Learning Pool Competitio 2013 Mwanza,  Vitalis Bakilane akiwa amebebwa na mashabiki mara baada ya kutwaa ubingwa wa Mkoa wa Dar es Saalaam tena wakati wa mashindano hayo yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Villa Park jijini Mwanza.
  Mabingwa wa mchezo wa Pool Mkoa wa Dar es Salaam,CBE wakishangilia na kitita cha sh.500,000  mara baada ya kuibuka washidi katika mashindaano hayo yajulikanyo kama Safari Lager Pool Higher Learning Pool Competitio 2013 yaliyomalizika mwishoni mwa wiki Meeda Sinza jijini Dar es Salaam.
Bingwa Mtetezi wa mashindano ya Pool yajulikayo kama Safari Lager Pool Higher Learning Pool Competitio 2013 Mkoa wa Dar es Salaam na Taifa, Peter Patrick akiwa amebebwa na mashabiki mara baada ya kutwaa ubingwa wa Mkoa wa Dar es Saalaam tena wakati wa mashindano hayo yaliyomalizika mwishoni mwa wiki Meeda Sinza jijini Dar es Salaam.


ASKARI POLISI WAWILI WATIWA MBARONI KWA KUSINDIKIZA MADAWA YA KULEVYA

Mahmoud Ahmad Arusha.

Jeshi la polisi mkoani hapa limefanikiwa kukamata magunia 30 ya bangi huku askari wawili wa jeshi hilo mkoani hapa wakikamatwa wakati wakisindikiza magunia 18 ya madawa ya kulevya aina ya mirungi kwenye mpaka wa nchi na Kenya Holili mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza na vyombo vya habari Kamanda wa jeshi hilo mkoani hapa kamishna wa msaidizi wa polisi Liberatus Sabas alisema kuwa mnamo tarehe 19 mwezi huu huko mpakani mwa nchi ya Kenya na Tanzania Holili mkoani Kilimanjaro askari wawili wa Jeshi hilo mkoani hapa Koplo Edward na Mwenzake pc.George walikimatwa akisindikiza mirungi magunia kumi nane.

Kamanda Sabas alisema kuwa watuhumiwa hao wapo mkoani Kilimanjaro na taarifa zao anazo kamanda wa polisi mkoa wa Kilimanjaro Robert Boaz alibainisha kuwa jeshi hilo limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa watatu wakiwa na bangi magunia 30 katika msako mkali walioufanya kwenye kata ya Ngarenanyuki wilayani Meru.

Sabas alibainisha kuwa wengine wawili walikimbia na jeshi hilo linawatafuta katika hatua nyingine jeshi hilo limakamata gari lenye namba za usajili KBQ372V lililoibiwa nchi jirani ya Kenya majira ya saa 6:30 usiku huko wilayani Longido.

Kamanda Sabas alisema kuwa katika kupambana na mitandao ya madawa ya kulevya walifanikiwa kuwakamata askari hao na kuwataka watanzania na wakazi wa mkoa huu kutoa taarifa zitazosaidia kumaliza matukio ya kiuhalifu mkoani Arusha kwani Arusha bila ya madawa ya kulevya inawezekana na nchi vile vile pia