Sunday, September 05, 2010
EID PARTY RED CAPERT AFFAIR@FACE CLUB READING

SAT 11Th SEPT 2010
EID PARTY RED CAPERT AFFAIR
AT FACE CLUB READING RG1 7JE
DOOR OPEN 10PM-4.30AM
ENTRY £10 ALL NITE
MUSIC BY FINEST DEEJAYS RICHIE, FUGGAFLEX, AND GUEST
ON THE NITE WILL BE OFFERING YOU THE BEST & LATEST AFRO BEATS,RnB,FUNK HOUSE,DANCEHALL +OLD SKUL & MANY MORE......
SO GET YA SWAGGA ON!!! THIS IS A NIGHT TO SHINE WITH THE FRIENDS FROM ALL OVER GIRLS DRESS TO IMPRESS GUYS COME FULL LOADED COME AND BE PART OF IT,THIS IS TOTALY A NIGHT NOT TO BE MISSED!!!
HOSTED BY BONGO DEEJAYS AND GERATON PROMOTIONS
for more info visit
www.bongodeejays.blogspot.com
angalizo la mdau juu ya lugha gongana...
Kwanza nakupongeza kwa kutupasha habari mbali mbali ambazo nyingi ni za kutuburudisha na kuelimisha. Ni ukweli usiopingika kuwa blog yako inasomwa na watu wengi sana, hasa sisi watanzania tuishio nje ya nchi. Lakini pia tukumbuke kuwa blog yako ni kioo cha jamii, na baadhi ya vijana wetu wanaamini kila kinachoandikwa kwenye blog hii ni sahihi.
Hivyo basi ni changamoto kwako kuhakikisha lugha na taarifa zinazotumika katika blog yako ni sahihi kwa kiwango kikubwa. Mimi naomba nigusie matumizi ya lugha inayotumika hasa wakati tunapochanganya maneno ya kingereza na kiswahili. mfano:Chuo kikuu cha University of Dar es salaam, hapa maneno yamerudiwa, chuo kikuu maana yake kwa kingereza ni University.
Mfano mwingine ni barabara ya Ali Hassan Mwinyi road, hapa utaona barabara maana yake kwa kiingereza ni road. Lugha kama hizi zimekuwa zikitumika mara kwa mara na hivyo kuleta mkanganyo wa lugha ambao si sahihi.
Mdau Ruger wa Ughaibuni
maajabu ya makaburi kando ya barabara ya iringa
Saturday, September 04, 2010
msaada kwenye tuta
Ankal Michuzi Salamaleko,
Nimerejea tena, safari hii nna swali ambalo naomba msaada tutani ili wadau wa Globu yetu ya Jamii wanisaidie.
Ni hivi ankal, kila mara nabishana na dereva wetu aitwaye Saidi kuhusu huu mtindo wake na madereva kibao wa hapa Dar wanapofika sheli kutia mafuta garini. Yaani huwa wananishangaza pale wanapoanza kutingisha gari wakati mafuta yanakaribia full tenki wao hukitingisha gari ili mafuta yawe yanajaa vizuri, Jee hii ni kweli ama ni magumashi?
Mdau Tandamti
JK akubalika Morogoro

JK akimnadi mgombea ubunge wa CCM Morogoro mjini Abdulaziz Abood leo katika uwanja wa Jamhuri katika ziara yake ya kampeni ya siku mbili mkoani humo
.jpg)
Wananchi wa Ngerengere wakimshangilia JK wakati alipowahutubia leo

Mkaazi wa Matombo, Morogoro vijijnini Mashariki, akinadi CCM

Mpuliza vuvuzela la kiasili wa Matombo, Morogoro vijijini leo

wakaazi wa Matombo katika mkutano wa kampeni wa JK

JK akihutubia wananchi wa Morogoro uwanja wa Jamhuri leo

Wakereketwa wa Morogoro mjini wakimlaki JK leo

sehemu ya umati uwanja wa Jamhuri leo

maelfu ya wakaazi wa mji kasoro bahari uwanja wa jamhuri leo

palikuwa hapatoshi...
vodacom miss tanzania kuondoka na gari aina ya hyundai i10

Warembo 30 wanaoshiriki shindano ya Vodacom Miss Tanzania 2010 wakipozi kwa picha kwenye gari yao aina ya Hundai i10 lenye thamani ya shilingi Milioni 12 ambalo mshindi wa taji hilo ndiye atakaeondoka nalo pamoja na kitita cha shilingi milioni 10 fedha taslimu.

Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania,George Rwehumbiza akiongea wakati wa kuonyesha gari lenye thamani ya shilingi Milioni 12 kwa warembo wanaoshiriki shindano ya Vodacom miss Tanzania 2010,ambapo mshindi wa taji hilo ataondoka na gari hilo pamoja na kitita cha shilingi milioni 10 fedha taslimu.

Warembo 30 wanaoshiriki shindano la Vodacom Miss Tanzania 2010 wakifungua gari lao Aina ya Hundai I 10 lenye thamani ya shilingi Milioni 12,ambapo mshindi wa taji hilo ataondoka na gari hilo pamoja na kitita cha shilingi milioni 10 fedha taslimu.
msaada tutani
Hi bro Michuzi,
Ningependa kujua kiutalamu ukomo wa uzazi kwa akina baba na akina mama
kwa maana ya umri. Baadhi ya watu wanadai kuwa akina baba waweza kupata watoto ktk umri mkubwa, na akina mama hawawezi kupata ktk umri mkubwa.
Wadau mwasemaje kuhusiana na hilo?
Wisdom itumike kujibu pls.
Mdau muungwana.
Memorial Service in London
The late Mzee Richard J. Kasella-BantuMwezi uliopita 15-07-10 Familia ya Kasella-Bantu tulimpoteza mpendwa Baba yetu mzee Richard J.Kasella-Bantu.
On September 5, 2010 from 14.00pm to 16.00om will be our beloved Father's Arubaini. On behalf of the Kasella-Bantu family we would like to inform family and friends and all of those who knew Mr Richard to come to celebrate his life through prayer.
The mass will be held at:
St Annes and St Agnes Lutheran Church,
2 Gresham Street London EC2V 7BX.
Our Father was an intelligent, loving and a wonderful person to know, you have taught us life is precious and should be shared with loved ones. We thank God for his life and the moments we shared. You were a great man to many and a rock to your loving family, you will be deeply missed by your loving wife Florence Kasella, your son's Ray,Roy and Ronald and Henry. Your Brothers, sisters, Uncle's, Aunties, Grandchildren, family and Friends.
Lamentations 3:31-33
For men are not cast off by the Lord forever.Though he brings grief, he will show compassion, so great is his unfailing love.For he does not willingly bring affliction or grief to the children of men.
Thank you to all our family and friends and those who have grieved with us and continue to bring the family comfort through prayer.
balozi mwapachu afungua tovuti ya kongamano la uwekezaji litalofanyika desemba mwaka huu jijini mwanza

KATIBU MKUU WA AFRICA MASHARIKI,BALOZI JUMA MWAPACHU AKIZINDUA TOVUTI YA KONGAMANO LA UWEKEZAJI KATIKA ZIWA VICTORIA LINALOTARAJIWA KUFANYIKA KATIKA JIJI LA MWANZA MAPEMA MWEZI WA KUMI NA MBILI MWAKA HUU,KULIA KWAKE NI MHARIRI WA TOVUTI YA JUMUIYA YA AFRICA MASHARIKI BW. EDWARD SSEKALO.TOVUTI HII IMEPEWA JINA LA ZIWA VICTORIA.(PICHA NA WOINDE SHIZZA,ARUSHA).
MOHAMMED G. DEWJI AIPONGEZA TAIFA STARS
Mh. Mohamed G. DewjiMimi kama mwenyekiti wa kamati ya ushindi kwa timu yetu ya Taifa (Taifa Stars) ninayofuraha kubwa kuwapa pongezi uongozi mzima wa timu yetu ya Taifa pamoja na wachezaji wetu kwa ushujaa waliouonyesha katika mechi yao dhidi ya Timu ya Taifa ya Algeria iliyochezwa siku ya Ijumaa tarehe 3/9/2010 ikawa ni kampeni za kuelekea katika kombe la mataifa ya Afrika.
Kwa nini nasema ni ushujaa?
Ni kwa sababu ya kuweza kuonyesha mchezo safi ile hali kukiwa na uonevu ulioonekana wazi ukiwa na lengo la kukandamiza timu yetu isipate ushindi. Hakuna mtu yoyote ambaye aliyeshuhudia mechi hiyo atapingana nami eti kulikwa hakuna uonevu! Lakini matokeo tuliyoyapa yamedhihirisha ukomavu wetu katika soka la kimataifa, Pongezi zangu za dhati zimfikie kocha mkuu wa Jean Paulsen kwa kuweza kuwatayarisha wachezaji kiakili ili kukabiliana vilivyo na hali hiyo ya uonevu na pia nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sitampa pongezi nyingi Abdi Kassim (Babi) kwa goli zuri alilolifunga katika kipindi cha kwanza cha mchezo.
Vilevile tukumbuke haya yote ni matunda ya mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kuamua kuweka nguvu kubwa katika mchezo wa soka nchini naye pia nampa pongezi kubwa na ninafahamu naye anasheherekea pamoja nasi matokeo haya popote pale alipo.
Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki Taifa Stars Ahsanteni Sana.
Mwenyekiti - Kamati ya Operation Ushindi.
Saadane resigns as Algeria coach after Tanzania draw

Rabah Saadane has resigned as Algeria coach, a day after his team's 1-1 home draw with Tanzania in a 2012 Africa Cup of Nations qualifier.
The Algeria Football Federation confirmed that Saadane had tendered his resignation following the disappointing result and that it had been accepted.
Saadane took charge three years ago and steered Algeria to their first World Cup in 24 years in South Africa.
But they went home early after gaining just a point from three group games.
The federation said that Algeria's under-17 coach Abdelhak Ben Chikha will take charge on a caretaker basis.
The 64-year-old previously considered quitting after his team were eliminated from the World Cup at the first hurdle without scoring a goal, but decided to stay on after being awarded a two-year contract extension.
The North Africans finished bottom of Group C after losing to Slovenia and the United States and drawing with England.
However, his extended stay proved short-lived as the Algerians, who reached the semi-finals of the Cup of Nations in Angola in January, opened their 2012 campaign with a dispiriting home draw with the Taifa Stars in Algiers.
The visitors led the Group D favourites when Abdi Kassim fired home a free-kick from 30-yards after 33 minutes.
Adlene Guedioura's equaliser on the stroke of half-time was enough to save some of the Desert Foxes' blushes, but not enough for Saadane to remain as coach.
Saadane has had five stints in all in charge of the national side, including in 1986, when he also led the side to the World Cup finals, in Mexico.
nafasi ya kazi kinondoni
Nafasi ya kazi ya kuuza dukani-Boutique in Kinondoni area. Mdau wa New York anahitaji mtu muaminifu ambaye anaelewa masuala ya uuzajia, kazi ni kuuza na kuripoti kwangu na kwa meneja wako aliyeko hapo monday to friday, wkend ni makubaliano mengine. tafazali uwe mwaminifu, mtanashati, mwenye lugha nzuri kwa watu na mchapa kazi! Mimi ni bosi mzuri sitakusonga as long as u do ur job u will love working with me! Sijali umri wala jinsia.
wasiliana nami: subiraga5@yahoo.com
Thanxxxx.
Video ya mechi ya Taifa Stars Na Algeria
Notting Hill Carnival Funika bovu
Urban Pulse Inapenda Kuwaletea wadau wote video ya Notting Hill Carnival Iliyofanyika hapa Ukerewe katika siku kuu ya benki(Bank Holiday) jumatatu 30.8.10 Jijini London.
Sherehe hii hufanyika kila mwaka na huvutia watu mbalimbali kutoka pande zote za dunia, Pia hii ni sherehe kubwa kuliko zote zinazofanyika barani Ulaya.
Wadau zaidi ya million moja na ushee walijumuika kwa pamoja na kusherekea kwa vifijo na ndelemo. Sherehe hii ilijumuisha mdundiko, mchiruku na ngoma toka tamaduni mbalimbali.
asanteni sana
Urban Pulse Creative
Azania Bank Ltd yafutarisha

Mkurugenzi Mtendaji, Bw Singili (katikati) akiwa na Sheikh Ahmad Mussa (kushoto) na Sheikh Hamisi Milambo

Sheikh Hamis akihitimisha kwa dua

Mkurugenzi wa Bodi Bw. Kidula akipakua futari.

wafanyakazi wa Azania Bank wakiwa na wageni waalikwa katika futari
dr. shein aanza kutembelea matawi ya CCM zanzibar

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM, Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia Wanachama wa Chama cha Mapinduzi CCM wa Tawi la Mtoni mjini Zanzibar leo, wakati alipokuwa katika ziara ya kuyatembelea Matawi ya CCM ya Wilaya ya Magharibi Unguja na kuzungumza Wanachama hao.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CCM,Dk. Ali Mohamed Shein, akizungumza na Mtoto Fatuma Juma (9) wakati alipotembelea katika Tawi la CCM Mtoni Mjini Zanzibar leo.
taifa stars ilivyopokelewa kwa shangwe nchini algeria

kinogozi wa wanafunzi wa kitanzania nchini Algeria,Habibu H.Ruhombo (pili kishoto) akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Taifa Stars,Mrisho Ngasa (pili kulia) na nyanda namba 2 wa Stars,Jackson Chove (kushoto) pamoja na mdau wa huko Algeria walipokwenda kuwapokea airport.

Taifa stars ikiwasili uwanja wakimataifa wa Algiers taya kwa kuelekea kwenye usafiri maalumu walioandaliwa na wenyeji wao katika ulizi mkali wa viosi vya usalama.

mashabiki wakiimba nyimbo za hamasa wakati timu yetu ya Taifa ilipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Algiers kwa ajili ya mpambano wao na wenyeji Algeria uliopigwa usiku wa kuamkia leo na kutoka sare ya bao 1-1.
kinyang'anyiro cha kumsaka balozi wa redd's
TAMASHA LA MUZIKI NA INJILI WASHINGTON DC SEPTEMBA 4 HADI 6,2010
KUTAKUWA NA TAMASHA LA MUZIKI NA INJILI KATIKA KANISA LA CATHEDRAL OF PRAISE MJINI WASHINGTON DC, WAIMBAJI MAARUFU AKIWEMO MSHINDI WA KORA AWARD KWA AFRICA GEORGE OKUDI KUWEPO MHUBIRI WA KIMATAIFA ASKOFU WALTER SMITH ATAHUDUMUSIKU:JUMAOSI,JUMAPILI NA JUMATATUMUDA 1PM - 6PM KILA SIKUMAHALI10110 GREENBELT ROADLANHAM, MD 20706MAELEZO ZAIDI PIGA240 338 4917301 712 2572301 256 6018
Z ANTO YUKO WAPI SIKU HIZI BAADA YA KUTOKA NA BINTI KIZIWI?
TAIFA STARS VS ALGERIA NGOMA DROO 1-1
MPIRA UMEISHA NA TAIFA STARS IMETOKA DROO YA 1-1 NA ALGERIA KATIKA MCHEZO WA MGUU WA KWANZA KUTAFUTA KUFUZU KUCHEZA FAINALI ZA MATAIFA YA AFRIKA. TAIFA STARS IMECHEZA KUFA NA KUPONA NA KUTANDAZA KANDANDA SWAFI MBELE YA MASHABIKI WA ALGERIA AMBAO WANAJUTIA NAFASI KIBAO WASHAMBULIAJIA WAO WALIZOKOSA HASA KATIKA KIPINDI CHA PILI WALIPOFUNGA KAMBI NUSU YA UWANJA UPANDE WA TAIFA STARS - HUKU WAKIBEBWA NA REFA AMBAYE ALIONGEZA DAKIKA 7 NZIMA ZA MAJERUHI AMBAPO WAMANGA HAO WALIPATA KONA KAMA NANE HIVI MFULILIZO LAKINI WAPI...
JK atoa changamoto kwa halmashauri ya jiji la dar kuelimisha wananchi juu ya mpango wa ujenzi wa mji mpya kigamboni
swali la kizushi
Asalaam aleikum bro Michuzi,
pamoja swaum uliyonayo nina suali dogo la kizushi, eti katkika suala zima la kuibua miradi na ujasiriamali hii imekaaje? Halafu hapa kama bongo vile, hayo si maji ya uhai au?? Kina mama wanaonaje?
Mdau Umangani
TAIFA STARS VS ALGERIA
NI DAKIKA YA 34 SASA NA TAIFA STARS INAONGOZA KWA BAO MOJA LILILOFUNGWA DAKIKA MBILI ZILIZOPITA KWA FREE KICK YA MITA 30 NA ABDI KASSIM, KATIKA MCHEZO WA KUTAFUTA KUFUZU KUCHEZA FAINALI ZA KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA UWANJA WA MUSTAPHA TCHAKER MJINI BLIDA.
NI MAPUMZIKO SASA NA ALGERIA WAMERUDISHA BAO DAKIKA YA 45. TAIFA STARS WANAKIPIGA HASWA ILA TU UMALIZIAJI KIDOGO KUNAWAANGUSHA.
Friday, September 03, 2010
helikopta za kukodi zatua dar
Uzinduzi wa usafiri wa helikopta juu ya hoteli ya holiday inn jijini dar leo
Usafiri mpya umeanza jijini Dar leo katika harakati za kukwepa msongamano na foleni. Usafiri huo, ambao ni wa helikopta umezinduliwa kwa mbwembwe leo jijini ambapo vikwangua anga kadhaaa vitatumika kama viwanja kama ilivyo katika nchi zilizoendelea zenye msongamano mkubwa wa usafiri wa ardhini.
Uzinduzi huo umefanyika hoteli ya Holiday Inn saa 5 asubuhi na kushuhudiwa na waandishi wa habari. Kampuni ya kukodi ndege ya Everett Aviation ndio wamiliki wa helikopta hiz ambazo idadi yake haijaelezwa.
“Huu ni mlango mzuri wa kuboresha biashara. Tutakuwa tukiwatoa wateja hapa na kuwapeleka maeneo kama Zanzibar, Mtwara na hata Uwanja wa Ndege kama mtu au kampuni itataka kupatiwa huduma hiyo.
"Wageni watakapokuwa wakiwasili kutakuwa na mawasiliano na mamlaka ya anga hapa nchini, lakini pia hata hapa kwenye hoteli ghorofa ya 11 kutakuwepo na waongoza ndege kutoka kampuni binafsi na wale ambao watakuwa tayari kukabilina na dharura yoyote itakayojitokeza kama ajali au moto, ingawa hilo hatutegemei kutokea,” alisema Meneja Masoko na Mauzo wa hoteli hiyo, Ruan Schreuder.
Schreuder alisema kuwa bado wanafanya mazungumzo na Malaka ya Anga Tanzania ili kupewa kibali cha kutoa huduma hiyo katika paa la hoteli yao na kuwa wanatarajia kuanza kutoa huduma hiyo mwezi Desemba mwaka huu.
jumatatu na jumanne ijayo hakuna kupiga kampeni
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imesitisha kampenzi za uchaguzi Jumatatu na Jumanne ili kupisha mtihani wa Taifa wa kuhitimu darasa la saba ufanyike bila bughudha.
Taarifa ambayo imetolewa na NEC na kusainiwa na Mkurugenzi Mkuu, Mh. Rajabu Kiravu, inasema kuwa hatua hiyo ni kutaka mitihani kufanyika kwa utulivu.
“...kwa kuwa mikutano ya kampeni za uchaguzi mara kwa mara imekuwa ikifanyika karibu na maeneo ya shula za msingi, tume baada ya kushauriana na vyama vya siasa imeamua kwamba pasiwepo na kampeni za uchaguzi zozote siku ya Septemba 6 na 7 mwaka huu,” alisema.
Alisema kuwa ili kupisha mitihani hiyo, NEC imeagiza wasimamizi wa uchaguzi kuhakikisha hakuna kampeni zinazoendelea kwa siku hizo mbili.
Kampeni zitaendelea tena rasmi tarehe 8 Septemba hadi 30 Oktoba 2010, imesema taarifa hiyo ya NEC.
JK aiteka Kawe, Ubungo na Mbagala leo
Bango la Dk Faustine
JK akimnadi mgombea ubunge wa CCM jimbo la Kigamboni Dk. Faustine Ndugulile ambaye ni mwana libeneke mahiri.
tamko la mamlaka ya mawasiliano nchini kuhusu uvumi wa mawasiliano ya simu ulieneka kwa kasi hapa nchini
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA

UZUSHI KUHUSU MADHARA YA MAWASILIANO YA SIMU
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imepata malalamiko kutoka kwa watumiaji wa simu za mkononi kwamba kuna ujumbe unaosambazwa kwamba ukipokea simu utapata madhara.
Mamlaka ya Mawasiliano inapenda kuwahakikishia wananchi kwa ujum;a kwamba taarifa zinazoenezwa ni za uzushi na sio za kweli. Wananchi wanaombwa kupuuza uzushi huo kwa kua hauna ukweli wowote.
Kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia, kuna tafiti nyingi zimefanyika sehemu nyingi duniani, ambazo zimeonyesha kwamba kiwango cha mawimbi ya mawasiliano hakina madhara kwa afya ya binadamu. Mamlaka inashauri watumiaji wa huduma na wananchi wote kwa ujumla, kuendelea kuwa na imani na teknolojia mpya zikiwemo za mawasiliano ya simu, utangazaji na utumiaji wa kompyuta, ambazo hutumiwa ulimwenguni kote bila kuleta madhara yoyote.
Madhumuni ya Mamlaka ya Mawasiliano na watoa huduma za mawasiliano kwa ujumla ni kuwaletea wananchi wa Tanzania mawasiliano bora kwa kujenga miundombinu, kutoa huduma bora na matumizi mema.
Uzushi unaoenea upuuzwe kwa kuwa hauna ukweli wowote.
Imetolewa na:
Mkurugenzi Mkuu
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.
yanga na simba kukutana Octoba 16,CCM kirumba jijini mwanza

PAMBANO la watani wa jadi Simba na Yanga linatarajiwa kuchezwa Oktoba 16 kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Pambano hilo ambalo litakuwa ni la mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Tanzania bara iliyoanza kutimua vumbi Agosti 21 ikiwa ni siku mbili baada ya vigogo hao kuvunja utepe katika mchezo wa kuwania ngao ya hisani iliyochezwa Agosti 18 na timu ya Yanga kuibuka kidedea kwa kuinyuka Simba mabao 3-1, Mchezo huo utachezwa Kirumba baada ya uwanja wa Uhuru kufungwa kutokana na shughuli za kitaifa na hivyo klabu za Ligi Kuu za jijini kutakiwa kusaka viwanja nje ya Dar es Salaam.
Kufuatia hali hiyo Yanga ilipeleka maombi Wizarani kuomba kutumia uwanja wa taifa hali kadhalika kwa Simba.
Awali kulikuwa na taarifa kuwa Yanga wameruhusiwa kutumia uwanja huo kwa kukatwa asilimia 10 ya mapato ya mlangoni kama garama ya uwanja pia itakatwa shilingi milioni tatu za usafi iwapo watacheza na timu kubwa ambayo italazimika kutumia mageti yote ya uwanja na iwapo itatumia
mageti machache itakatwa shilingi milioni 1.8.
Hata hivyo kuna taarifa kuwa Simba ambao awali walitangaza kutumia uwanja wa CCM Kirumba waligeuka na kupeleka barua wizarani kuomba nao waruhusiwe kutumia uwanja huo kitu ambacho kiliiwia vigumu serikali ambao walidai haiwezekani kutumia uwanja huo kwa mechi
mfululizo.
Kaimu katibu mkuu wa TFF, Sunday Kayuni amesema leo kuwa "Baada ya mazungumzo ya muda mrefu Wizara ilikubali ichezwe michezo miwili kwa Simba na Yanga lakini kwa taratibu zetu haiwezekani kuwa na viwanja viwili vya nyumbani nje ya mkoa wake hivyo tuliviachia vilabu vikubaliane kuachiana jambo ambalo halikuwa rahisi."alisema Kayuni.
"Maamuzi ya mwisho Simba watatumia uwanja wa CCM Kirumba na tunaitaka Yanga itufahamishe uwanja watakaotumia ifikapo saa kumi na moja jioni hii, Simba pia wametuarifu pambano lao na Yanga litachezwa Kirumba kwa kuwa wao ndio wenyeji wa mchezo."alisema Kayuni.
kongamano la bonde la ziwa Victoria kufanyika jijini Mwanza mwezi desemba

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,Balozi Juma Mwapachu, akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu kongamano la bonde la ziwa Victoria litakalofanyika jijini Mwanza mapema mwezi Desemba mwaka huu,kwenye mkutano uliofanyika leo katika hoteli ya Naura Springs jijini Arusha.

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki,Balozi Juma Mwapachu, akiongea leo hukusu mipango ya kongamano la bonde la ziwa Victoria litakalofanyika mapema mwezi Desemba mwaka huu huko jijini Mwanza.mkutano huu umefanyika leo katika hoteli ya Naura Springs jijini Arusha.Picha na Woinde Shizza.