THIS BLOG IS PROUDLY SPONSORED BY VODACOM, TANZANIA'S LEADING CELLULAR NETWORK. | NDOVU SPECIAL MALT - BEYOND THE ORDINARY - NATURALLY' Karibu katika hii Globu ya jamii. Una karibishwa kutoa maoni yako yoyote yatakayo jenga taifa letu. Nawasihi kila mmoja wetu ajiheshimu kwa kutumia lugha zisizochafua hali ya hewa. Yaliyomo humu hayahusiani kwa vyovyote vile na hariri za magazeti ya Daily News, HabariLeo na Sunday News. Maoni yanayotolewa na wasomaji si ya GLOBU YA JAMII, ni ya mtoa maoni isipokuwa pale itavyoelezwa vinginevyo. Akhsanteni sana na tuendeleze Libeneke.




  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com
  • P. O. Box 33909, Dar es Salaam, Tanzania.  Tel: +255 22 26647870/1/3  Fax: +255 22 2647872. www.giraffeoceanviewhotel.com














waziri mkuchika ziarani newala

 Mh Mkuchika akiwahutubia kwa nyakati tofauti wanavijiji wa Mtopwa, Idamnole, na mtongwele (hawapo pichani) jana katika siku ya tatu ya ziara yake ya siku saba ya kutembelea wilaya hiyo ambapo atahutubia vijiji 22
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais utawala bora, George Mkuchika ambaye pia ni mbunge wa Newala, akipokea zawadi kutoka kwa mwakilishi wa wazee wa kijiji cha Mtopwa Yusufu Livata kumpongeza kwa kuteuliwa tena kuingia katika baraza la mawaziri., mkuchika yupo katika ziara ya siku saba ya kutembelea wilaya hiyo (Picha na Hassan Simba).


ATCL yaanza mchakato wa kupata ndege nyingine

 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la ndege la Tanzania (ATCL) Paul Chizi (katikati) akikata  utepe kuzindua rasmi safari za ndege hiyo kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza wikendi hii.
 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la ndege la Tanzania (ATCL) Paul Chizi akiongea na waandishi wa habari kwenye uwanja wa ndege wa Mwanza mara bada ya kuzindua safari za ndege mpya ya Shirika hilo aina ya Boeing 733-500 wikendi hii.
 Mhudumu wa Ndege wa ATCL ambaye hakufahamika jina mara moja akimhudumia mmoja wa abiria wakati wa uzinduzi wa safari za ndege ya ATCL aina ya Boeing 737-500.
 Ndege ya ATCL  aina ya  Boeing 737-500 inavyoonekana kwa mbele
 Wahudumu wa ndege wa Shirika la ATCL wakipozi mbele ya Kamera ya blogu hii.
Abiria wakishuka kwenye ndege aina ya  Boeing 737-500 ya ATCL kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) wakati wa uzinduzi wa safari za ndege hiyo wikendi hii. Ndege hiyo itafanya safari za kila siku za Dar es Salaam-Kilimanjaro-Mwanza mara mbili kwa siku.

Na Mwandishi wetu.

MARA baada ya wiki moja tu baada ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) kupata ndege aina ya Boeing 737-500 iliyoanza rasmi safari za Dar es Salaam-Kilimaanjaro-Mwanza wikendi hii, Shirika hilo limeanza mchakato utakayoliwezesha kupata ndege nyingine kati ya wiki tatu au sita zijazo.

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya safari hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa ATCL Paul Chizi alisema shirika lake linatarajia kupata ndege nyingine aina ya Boeing ambayo italiwezesha shirika hilo kufanya safari za nje zikiwemo Dar es Salaam-Lusaka, Dar es Salaam-Harare and badae Dar es Salaam-Dubai.

“Tumeanza utekelezaji wa mpango kazi wetu wa muda mrefu ambao utatuwezesha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi.
“Katika mpango wetu ,tunatarajia kupata ndege nyingi na bora zaidi. Kwakuanzia,tunarajia kupata ndege nyingine katika kipindi cha wiki tatu mpaka sita na ndege hiyo itatuwezesha kuanza safari za kimataifa,’ alisema Chizi.

Chizi aliwataka wananchi pamoja na mashirika mbalimbali kuunga mkono jitihada za Shirika lake na kuahidi kuwa shirika hilo litazingatia utoaji wa huduma bora kwa bei nafuu. “Mafanikio ya shirika yatategemea mchango wa wadau mbali mbali. Tunaomba wananchi watuunge mkono ilituweze kupata mafanikio zaidi,” alisema.

Chizi alisema kuwa katika wiki chache zilizopita kampuni yake ilizindua tovuti ambayo itasaidia katika kuboresha huduma ya ukataji tiketi kwa wateja kwa wakati wao na kuboresha utoaji huduma wa kampuni.

 “Kitu cha kujivunia ni kuwa wateja sasa wanaweza kutaka tiketi kupitia mtandao bila kufika katika ofisi zetu au kupitia mawakala wetu kama ilivyo zamani,” alisema.

Nae Jaji Mstafu wa Mahakama Kuu ambaye alipata nafasi ya kusafiri kwa kutumia ndege mpya ya shirika hilo aliomba Serikali kutoa ruzuku kwa Shirika hilo na kusisitiza kuwa uboreshaji wa shirika hilio utaongeza pato la taifa kupitia sekta ya Utalii.


President Kikwete attends working lunch hosted by President Obama at Camp David





President Jakaya Kikwete, Prime Minister Meles Zenawi of Ethiopia, Ghana's President John Atta Millls and President Yayi Boni of Benin, chairman of the African Union, on Saturday May 19, 2012 went down  history books as the first African leaders to attend a G-8 summit at Camp David in Maryland, USA.

The event, whose host US President Barak Obama hailed as remarkable, saw the world leaders devoting the working lunch to food security.

Held in the Laurel Lodge, the session was a follow-up to President Obama's Friday announcement of a ten-year, $3 billion partnership plan for public-private agricultural investments in Africa.

In addition to the G8 leaders and the four African leaders, there were also six executives from some of the 45 US and African corporations that have partnered for the New Alliance for Food and Nutrition.

President Obama said he believes it is the first time private sector representatives - who included PepsiCo chief Indra Nooyi - have attended a session at any G8 Summit.

Seated at a long rectangular table between Ghana's President John Atta Millls and President Yayi Boni of Benin, Chairman of the African Union, President Obama, in  shirtsleeves, said the group will be "looking for a range of innovative ideas”.

President Jakaya Kikwete of Tanzania and Prime Minister Meles Zenawi of Ethiopia sat across them. 

Other leaders present were Stephen Harper, the Prime Ministerof Canada, President François Hollande of France and Germany's Chancellor Angela Merkel.

Others were Italy's Prime minister Mario Monti, the Prime Minister of Japan Yoshihiko Noda, Prime Minister of Russia Dmitry Medvedev and the Prime Minister United Kingdom David Cameron

"What makes this remarkable is this is probably the first time at a G8 Summit where in addition to having the leaders involved, we also have leaders of NGOs and business leaders involved," President Obama said.

"My goal is to have a very open conversation...and my hope is that coming out of this meeting, we are then going to be able to then each of us have assignments that we have to execute before the next G8 Summit."

The New Alliance builds on the L'Aquila Food Security Initiative, a $22.billion effort created in 2009 by G8 leaders, led by President Obama.

According to the the White House, attendees from the US private sector included Nooyi, Chair and CEO of PepsiCo and Mr. Michael Mack, CEO of Syngenta International AG.

From Africa: Tidjane Thiam, Cote d'Ivoire group CEO of Prudential; Dr. Donald Kaberuka, President of African Development Bank Group; Dr. Eleni Gabre-Madhin, Ethiopia, CEO and founder of Ethiopia and Commodity Exchange.


WORLD HYPERTENSION DAY 2012

 Members of the TANZANIA MEDICAL STUDENTS’ ASSOCIATION (TAMSA)-KCMC in collaboration with the MEDICAL ASSOCIATION OF TANZANIA (MAT) NORTHERN ZONE this week marked the international Hypertension day by conducting   free hypertension and diabetes screening to over 300 at the KCMC hospital in Moshi.
 
 Souvenir photo of the day
Relaxing after a job well done.


Hongera Chelsea kwa kupeleka kombe la ubingwa wa ulaya darajani



Innocent Nganyangwa awakuna mashabiki tamasha la carribean beat viwanja vya posta usiku huu,jijini dar

 Innocent Nganyangwa akiimba kwa hisi jukwaani usiku huu,kwenye tamasha la kumuenzi hayati Bob Marley.
Mwanamuziki mkongwe wa reggae nchini Tanzania  Innocent Nganyagwa akikamua usiku huu kwenye tamasha la carribean beat,lililoandaliwa kwa ajili ya kumkumbuka muasisi wa muziki wa reggae Ulimwenguni,Hayati Bob Marley,tamasha hilo linafanyika ndani ya viwanja vya posta,Kijitonyama jijini Dar.Picha zaidi ingia Hapa


THE INTERNATIONAL CONFERENCE ON THE GREAT LAKES (ICGLR) REGION FIRMILY CONDEM THE RESUMING VIOLENCE IN THE NORTH-KIVU PROVINCE OF THE DEMOCRATIC REPUBLIC OF CONGO (DRC)

The Executive Secretariat of the International Conference on the Great Lakes Regions (ICGLR) is deeply concerned about the resuming of the violence related to the negatives forces in the North-Kivu province in the Eastern part of the Democratic Republic of Congo (DRC), specifically in the districts of Masisi and Rutshuru since April 2012.

Several elements of the ex-rebel movement, the People’s Defense National Congress (CNDP) which has been integrated into the National Army of the DRC (FARDC) following the 2009 Goma Peace Agreement had decided to mutinate from the FARDC and since then, they are conducting several attacks in the North-Kivu province, raping, killing, stilling, burning villages and recruiting children in schools and send them at the frontlines.

In the night of 13 to 14 May 2012, following a deadly attack attributed to the Democratic Alliance for the Liberation of Rwanda (FDLR), one of the prominent negative forces in the region, against the population of Kamaniga village, in the Sector of Bunyakiri (Kalehe district), South Kivu province. This attack against the village had caused severe casualties among the local communities. The survivals of the tragedy, very frustrated and disappointed for being totally left without any protection against the various armed groups operating in the region, had conducted a punitive attack against a UN peacekeeping position stationed in Kanamiga, wounding 11 among whom, 7 in are in a critical condition.

The ICGLR Secretariat firmly condemns the massive human rights committed by all negative forces in the North Kivu province by the various illegal armed groups. The insecurity generated by the military operations related to these armed groups had caused deaths, massive rape cases, Internally Displaced Persons (IDP), Refugees, etc. Several villages had been burnt, and children abducted and sent by force on the frontlines.
During his official visit to Uganda and Rwanda the last week, the ICGLR Executive Secretary met with Senior political and military officials of both countries, both countries having being the signing members of the ICGLR Pact on Peace, Security, Stability, Development and Regional Integration in the Great Lakes Regions.

He highly appreciated the efforts deployed by the DRC and Rwanda in collaborating to ensure that peace and security prevail in both countries. He encouraged all ICGLR member states to act commonly in the spirit and the framework of the Pact.

The ICGLR Executive Secretariat encourages the countries of the Great Lakes Regions as well as the International community to strengthen their support to all the victims of the political instability in the North-Kivu province, especially for the vulnerable groups including the Victims of Rape and Sexual and Gender-Based Violence, IDPs, Refugees, etc.

In the same perspective, the ICGLR Executive Secretariat had highly appreciated the outcomes of the joint meeting between DRC-Rwanda on the Security issues in the North-Kivu province which took place in Rubavu (Gisenyi/Rwanda) on 12 May 2012.

The meeting, chaired by the Ministers of Defense of the two countries, issued a statement indicating the commitments of both countries to immediately conduct joint verifications at their common borders, but also, within each one of the countries. The two countries also decided to develop a common operational plan against the negatives forces in the region, among which the FDLR. During the meeting, the Government of Rwanda also committed to continue providing support to the DRC’s efforts in rehabilitating and maintaining Peace and Security in the Eastern part of its territory.

The ICGLR Executive Secretariat recalls that the renegate General Bosco Ntaganda, who is re-engaged in massive Human rights abuses in the DRC North-Kivu province has been a subject to an warrant for War Crimes and Crimes Against Humanity including Rape, recruitment and used of child soldiers in Ituri by the Movement of the Congolese Patriots (UPC) which was headed by Thomas Lubanga, since then detained at The Internal Criminal Court (ICC) in The Hague, and who’s indictment has recently been confirmed on the same charges.

The Executive Secretariat strongly believes that arrest of Bosco Ntaganda and other criminals who are still committing massive human rights abuses in the Eastern part of the DRC would send a very strong message to the entire region. Such a move could strengthen the existing efforts in fighting impunity, in rehabilitating the Victims of Rape and Sexual and Gender-Based Violence (SGBV). It could also assist in implementing and strengthening the Zero Tolerence against the perpetrators of the Human Rights violations and concretize the Fight against the Illegal Exploitation of Natural Resources in the Great Lakes Region.

The ICGLR Executive Secretariat seize this opportunity to reiterate its commitment to work in close collaboration with all existing actors in order to ensure that the 2006 ICGLR Pact on Peace, Security, Stability, Development and Regional Integration is fully implemented in the Great Lakes Region.


Bonanza la Ufunguzi wa Mashindano ya Excel With Grand Malt 2012 laendelea leo mjini moshi

 Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya,Joh Makini akiwaburudisha mashabiki wake kwa nyimbo zake mbali mbali wakati wa Bonanza la Ufunguzi wa Mashindano ya Excel With Grand Malt 2012,lililofanyika kwenye uwanja wa Chuo cha Ushirika,Moshi mkoani Kilimanjaro jioni ya leo.
 Mratibu wa Mashindano ya Excel With Grand Malt 2012,Victor Ndunguru (kushoto) akikabidhi zawadi ya Box la Grand Malt kwa washindi wa Mchezo wa Kuvuta Kamba wakati wa Bonanza la Ufunguzi wa Mashindano ya Excel With Grand Malt 2012,lililofanyika kwenye uwanja wa Chuo cha Ushirika,Moshi mkoani Kilimanjaro jioni ya leo.
 Baadhi ya wanafunzi wa Chuo cha Ushirika,Mjini Moshi wakishiriki kwenye mchezo wa kuvuta kamba. 


Mualiko wa Dua ya Kumrehemu Sheikh Yahya Hussein ikiwa ni Mwaka Mmoja toka Afariki Dunia

Alhajj Maalim Hassan Sheikh Yahya Hussein,anayo furaha kubwa kuwaalika nyote Katika Dua ya kumrehemu Sheikh Wetu Sheikh Yahya Hussein Itakayosomwa siku ya Jumapili 20/05/2012 (kesho) ikiwa ni Mwaka mmoja toka kufariki kwake.

Shughuli hiyo itafanyika kwenye Msikiti wa Manyema uliopo Mtaa wa Mafia na Lumumba jijini Dar es Salaam,kuanzia Saa Saba mchana baada ya Swala ya Adhuhuri.

Kufika kwako ndio ukamilifu wa Shughuli hiyo. 

Tunatanguliza Shukurani zetu za dhati kwa kufika mapema.

Maalim Hassan Yahya Hussein


mdau Oltesh Eliguard na Ssanyu Sylvia wakimeremeta mchana wa leo ndani ya azania front jijini dar

Maharusi,Bw.Oltesh Eliguard Metili na Ssanyu Sylvia Nyinondi wakiaga watu mbalimbali waliofika ndani ya kanisa la Azania Front,mara baada ya kufunga ndoa takatifu,mapema leo mchana jijini Dar.
Maharusi wakiwa na nyuso za furaha mara baada ya kufunga ndoa na kuwa mwili mmoja mapema leo ndani ya kanisa la Azania Front,jijini Dar.
Maharusi wakilishana kiapo cha ndoa mbele ya umati mkubwa (haupo pichani) uliofika kanisani hapo mapema leo mchana kuishuhudia ndoa hiyo ya Bw.Oltesh Eliguard Metili na Ssanyu Sylvia Nyinondi,iliyofanyika ndani ya kanisa la Azania Front.
Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dk Alex Malasusa akizibariki pete za ndoa za maharusi kabla ya maharusi hao kuvishana.
 Baadhi ya Wanakwaya kutoka mkoani Arusha wakiimba
Umati wa watu uliofika kuishuhudia ndoa ya Bw.Oltesh Eliguard Metili na Ssanyu Sylvia Nyinondi iliyofanyika mapema leo mchana ndani ya kanisa la Azania Front,jijini Dar.
Maharusi wakiingia ndani ya kanisa la Azania Front mapema leo mchana,tayari kwa kufunga ndoa takatifu.Kushoto ni Waziri Mkuu Mstaafu Mh Edward Lowassa na Mkewe, Mama Regina Lowassa wakishuhudia pia tukio hilo adhimu  na la kihistoria kwa Wanandoa.
Maharusi Bw.Oltesh Eliguard Metili na Ssanyu Sylvia Nyinondi wakiwa na wapambe wao wakielekea kanisani,tayari kwa kufunga ndoa takatifu,mapema leo mchana.


dkt kigoda amsimamisha kazi bosi wa tbs charles ekerege

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Abdallah Kigoda, amemsimamisha kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Charles Ekerege (pichani), kwa tuhuma za ubadhirifu.

Kusimamishwa kazi kwa Ekerege kumekuja baada ya kuwepo sintofahamu ya muda mrefu kuhusiana na kukabiliwa na tuhuma nzito za upotevu wa takriban sh bilioni 38 zinazotokana na ukaguzi wa magari nje ya nchi.

Kigoda alitangaza uamuzi huo jana, na kudai kuwa ni kwa ajili ya kutoa nafasi ya kufanyika kwa uchunguzi wa kina juu ya tuhuma hizo, ambapo ameunda kamati maalum ya uchunguzi. Hata hivyo, waziri huyo hakutaka kuingia kwa undani kuhusiana na suala la mtendaji huyo mkuu wa TBS.
Waziri huyo aliyeanza kazi wiki iliyopita, alisema ameamua kumsimamisha kazi Ekerege ili kulifanya shirika hilo lirudi katika hali yake ya kawaida ikiwemo kupisha bodi iliyoundwa kutimiza wajibu wake.

Tuhuma dhidi ya Ekerege ziliibuliwa na kamati mbili za kudumu za bunge, ya Mashirika ya Umma (POAC) na Hesabu za Serikali (PAC), ambapo wajumbe wa kamati hizo waliokwenda kufanya ukaguzi nje ya nchi walibaini madudu mengi, ikiwemo kutokuwepo kwa ofisi za ukaguzi kama ilivyodaiwa na shirika hilo, kiasi cha kusababisha upotevu wa sh bilioni 38.
Wajumbe wa kamati hizo walibaini malipo ya kampuni hewa za ukaguzi wa magari nje ya nchi.

Hatua ya kumsimamisha Ekerege, imekuja baada ya mtangulizi wake, Waziri Cyril Chami, kushindwa kumchukulia hatua ikiwemo kumsimamisha, jambo ambalo pamoja na tuhuma nyingine dhidi ya mawaziri kadhaa, lilizua mzozo mkubwa bungeni kiasi cha kuwalazimisha wabunge kutishia kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Chami pia inadaiwa alikataa ushauri wa aliyekuwa naibu wake, Lazaro Nyarandu, ambaye alitaka asimamishwe kazi kupisha uchunguzi, na akadiriki kuendelea na msimamo huo hadi alipoachishwa uwaziri wa viwanda na biashara.

Katika utetezi wake, Chami alidai kushindwa kumwondoa mkurugenzi huyo madarakani kwa kile alichodai kuwa mtendaji huyo ni mteule wa Rais kama alivyo yeye. Kauli hiyo, na kubaki madarakani kwa Ekerege, kuliwashangaza wengi ambao waliamini kuwa hakukuwa na sababu ya kutomwondoa kwa vile lengo lilikuwa kutaka tume ya uchunguzi ifanye kazi yake ikiwa huru.

Aidha inajulikana wazi kuwa kusimamishwa sio kufukuzwa, na hivyo angeweza kurudi kazini ikiwa ataonekana hana hatia.

Hata hivyo Dk. Kigoda ambaye ni Mbunge wa Handeni hakuwa tayari kuwataja wajumbe wa kamati hiyo ya muda waliopewa kumchunguza Ekerege.

Katika hatua nyingine waziri huyo alisema atainua sera ya kukuza viwanda na biashara ikiwemo kuinua wafanyabiashara wadogo na ushirikiano baina ya serikali na viwanda vidogo.

“Tumepanga kuwasaidia wajasiriamali na kuangalia maeneo ambayo watu wakiwezeshwa watainua uchumi wao na kuboresha utendaji kazi,” alisema.
Alisema kiwanda cha General Tyre kitahitaji kufufuliwa na viwanda vya Pamba na Korosho.

Pia alivisifu viwanda vinavyoiingizia serikali mapato kuwa ni kiwanda cha Saruji Twiga, Sigara (TCC) na viwanda vya bia kutaka viwanda vingine kuiga mfano ikiwemo kuongeza juhudi.

Akizungumzia uwekezaji katika nchi, waziri huyo alisema kuwa suala la kupunguza gharama za umeme halijapata ufumbuzi hivyo juhudi zinahitajika kukabiliana na changamoto hiyo.

Chanzo: Tanzania Daima


Tanzania kuwa moja ya nchi za mwanzo barani Afrika, kunufaika na mpango wa pamoja wa Kilimo

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania itakua moja ya nchi za mwanzo barani Afrika, kunufaika na mpango wa pamoja wa Kilimo kwa nia ya kuongeza na kulinda usalama wa chakula na lishe kwa watu wake.

Rais Barack Obama wa Marekani aliyasema hayo jana (18.5.12) katika hotuba yake ya ufunguzi wa kongamano kuhusu Kilimo na usalama wa chakula (Global Agriculture and Food Security) lililoandaliwa na kituo cha Masuala ya Kimataifa, Chicago Council on Global Affairs jijini Washington.

"Nimeona kuwa kuna umuhimu pia wa kuangalia changamoto zinazoikabili dunia, changamoto ya usalama wa chakula, tutatangaza ushirikiano mpya na nchi tatu zitakua za mwanzo kuanza ushirikiano huu ambao tutatangaza kwenye kushughulikia usalama wa chakula" Rais Obama amesema hayo mbele ya viongozi wa Afrika, ambao nchi zao zitakua za mwanzo kunufaika na uhusiano huo ambazo ni Ethiopia, Ghana naTanzania.

Rais Obama amesema ushirikiano huu mpya utatangazwa rasmi katika Kikao cha Nchi 8 tajiri zenye viwanda duniani maarufu kama G8 unaofanyika tarehe 19 May, 2012 katika makazi ya kupumzikia Rais wa Marekani na wageni wake maarufu kama Camp David.


Kikao hicho cha nchi tajiri duniani kimeweka katika agenda yake swala la chakula duniani kutokana na umuhimu wake katika kipindi hiki.

“Tumeliweka suala la kupiga vita njaa, Marekani ina wajibu wa kupiga vita njaa na pia suala la usalama wa chakula ni suala la kiuchumi" amesema na kuelezea kuwa Bara la Afrika linaweza kujitosheleza kwa chakula na pia katika kuuza nchi za nje.

Ushirikiano huu utakaotangazwa na Nchi 8 tajiri utahusisha serikali, watu binafsi na wafadhili ambapo mwito umetolewa kwa nchi tajiri kutimiza ahadi zao.

Kikao cha kila mwaka cha Nchi 8 tajiri zenye viwanda duniani ambazo ni Canada, ufaransa, Ujerumani, Italia, Japan na Urusi, zingine ni Uingereza na Marekani.

Katika kikao cha mwaka huu, Tanzania imealikwa kuhudhuria kikao hicho kutokana na mpango wake wa Kilimo Kwanza, ambapo nchi tajiri zimeuchukua kama mfano ambapo juhudi na mikakati iliyomo katika Kilimo Kwanza, itatumika na kuendeleza nchi zingine barani Afrika.

Rais Obama amesema nchi hizi tatu za kwanza zimechaguliwa kunufaika na ushirikiano huu kwa vile zimeonyesha kufikia katika Kilimo na usalama wa chakula.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete, tayari yuko jijini Washington kuhudhuria kikao hicho ambapo anategemewa kuelezea matarajio na muelekeo wa Tanzania katika ushirikiano huu.

Akizungumza katika kongamano hilo la siku moja, Rais Kikwete ameelezea umuhimu wa ushirikiano huu unaohusisha serikali, wafanya biasharabinafsi na wafadhili.

"Tunahitaji msaada zaidi katika Kilimo na pia Kilimo hakiwezi kuachwa kwenye mikono ya serikali na wafadhili peke yake, hata Sekta binafsi ina mchango mkubwa" amesema na kuelezea kuwa amefarijika sana, ana matumaini na anategemea yanayozungumzwa yatatimizwa"

Mkutano wa G8 pia utahudhuriwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika, ambapo Mwenyekiti wake, Rais Yayi Boni wa Benin anatarajia kuhudhuria pamoja na Rais John Mills wa Ghana na Waziri Mkuu wa Ethiopia Meles Zenawi.

Rais Kikwete ataondoka Marekani Jumapili usiku kurudi Dar-es-Salaam.

Imetolewa na Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi.
Washington.


HALFA YA CHAKULA KUCHANGIA UNUNUZI WA JENGO LA MSIKITI NA MADRASA NCHINI UINGEREZA

An Noor Community Centre ikishirikisha Madrassatul Noor Leicester ya UK inafuraha kuwaalika Waislamu wote nchini UK

Katika HAFLA (Fundraising Dinner) kwa ajili ya chakula cha kuchangia ununuzi wa jengo kwa ajili ya Msikiti, Madrasa na Maktaba ya Kiislamu

Hafla hiyo itafanyika kwa utaratibu ufuatao:

SIKU NA TAREHE:                Jumapili 20 Mei 2012
PAHALA:                                            Leicester Exhibition Centre, 203 Belgrave Road,LE1 3HT
MUDA:                                                Saa kumi na moja jioni hadi saa Nne usiku (5.00pm-10.00pm)

Kadi zinapatikana mlangoni siku ya hafla
Wanawake na watoto £15, Wanaume £25
Kama unapenda kuchangia ila hutaweza kuhudhuria, tafadhali waweza kutuma mchango wako kwa akaunti ifuatayo:

Bank: LLOYDS TSB
Account Name: Madrassatul Noor Leicester
Account Number: 45127768
Sort Code:                  30-94-97

Kwa walio nje ya nchi:

International Account Details:

LOYDGB21029

Iban:  GB27LOYD30949745127768

Shime tushirikiane kufanikisha mradi huu wa kheri. Kumbuka, Mwenye kuchangia ujenzi wa nyumba ya Allah, Allah atamjengea nyumba ndani ya pepo yake adhimu.

Kwa maelezo zaidi juu ya project hii, tafadhali wasiliana na:

MWENYEKITI WA JUMUIA            -Mohammed OMAR +44 790 397 8481
MAKAMU MWENYEKITI                -Abdul DAU                +44 779 210 4495

AN NOOR COMMUNITY CENTRE
CHARITY NUMBER 1146906


Omy Dimpoz kutoka na Kitu Kipya Jumapili hii jijini Dar

BAADA ya kutamba na wimbo wake wa Nai Nai Msanii anaekuja juu kwa kasi na mshindi wa Tuzo mbili za Kili Music Award 2012, Omy Dimpoz anataraji kuzindua Single yake mpya ya Baadae katika ukumbi wa Club Bilcanas jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na mtandao huu wa Kijamii, Meneja wa Msanii huyo, Mbaruku Issa ‘Mubenga’ alisema kuwa maandalizi yote yamekamilika na show itakuwa ya uhakika nay a kuvutia.

Mubenga amesema Ommy Dimpozy anataraji kuzindua wimbo huo aliofanyiwa kazi na Mwandaaji wa muziki Man Water huku spoting ya wimbo huo ikifanywa na mwanadada Angel.

Aidha Mubenga amesema Dimpoz atasindikizwa na wakali wa Bongo Fleva, Diamond, Ben Pol pamoja na msanii Alawi Jr pamoja na Ma DJ wakali wa Bongo kutoka kundi la Super Deejayz.

Tayari Dimpoz ameshaanza kuwasikilizisha wimbo huo baadi ya mashabiki wake wa mikoa ya Mwanza na Moshi wakati wa Ziara ya Wakali wa Kili Music Awartd 2012 inayoendelea ambapo leo atakuwa Mbeya chini ya Bia ya Kilimanjaro.

“Wimbo ni mkali na mashabiki wanaukubali vilivyo na tunaomba mashabiki wa Bongo Fleva make tayari kwa singo hiyo mpya itakayoanza sasa kuchezwa katika vituo vya redio na kumbi za burudani nchini kote baada ya uzinduzi huo,” alisema Mubenga.

Mungenga amewakata wakazi wa jiji la Dar es Salaam ambao ni mashabiki na wapenzi wa muziki wa kizazi kipya kujitokeza kwa wingi kumpa support Dimpoz katika uzinduzi huo wa aina yake katika Club ya Bilcanaz katikati ya jiji la Dar es Salaam jumapili.


Msama Akabidhi Baiskeli ya Walemavu kwa mkazi wa Buguruni Jijini Dar

Mkurugenzi wa Msama Promotons, Alex Msama akimkabidhi msaada wa baiskeli ya watu wenye ulemavu, mkazi wa Buguruni jijini Dar es Salaam, Mohamed Komu kwa ajili ya kumsaidia katika kazi zake. Msaada huo ni sehemu ya mapato yaliyotokana na tamasha la Pasaka lililofanyika hivi karibuni kwenye Uwanja wa Taifa na mjini Dodoma kati ya Aprili 8-9.
Mkurugenzi wa Msama Promotons, Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kukabidhi msaada wa baiskeli ya watu wenye ulemevu kwa mkazi wa Buguruni jijini Dar es Salaam, Mohamed Komu (hayupo pichani).
mkazi wa Buguruni jijini Dar es Salaam, Mohamed Komu ambaye ni mlemavu wa miguu akitoa shukrani baada ya kukabidhiwa baiskeli yake hiyo.


watendaji wakuu wa sekta binafsi wakunwa na ahadi za MAADILI


Mh. Zitto Kabwe akutana na Spika wa zamani wa Marekani Nancy Pelosi na Mbunge Dennis Kucinich

Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini,Mh. Zitto Kabwe (kati) akiwa katika picha ya pamoja na Spika wa zamani wa Bunge la Marekani,Mh. Nancy Pelosi (kushoto) na Mbunge Dennis Kucinich mara baada ya kukutana nao na kufanya nao mazungumzo.


MASHINDANO YA SAFARI LAGAR POOLTABLE KWA VYUO VYA ELIMU YA JUU YANAENDELEA LEO MKOANI IRINGA

Mchezaji wa Mchezo wa Pool kutoka Timu ya Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCO) Mkoani Iringa ,Alen Masebo akijitayarisha kupiga mpira wakati wa mashindano ya mchezo huo kwa Vyuo vya Elimu ya Juu yanayoendelea hivi sasa katika vyuo mbali mbali nchini.Mashindano haya yanadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania kupitia bia yake ya Safari Lager.
Mchezaji wa Mchezo wa Pool kutoka Timu ya Chuo Kikuu cha Tumaini Mkoani Iringa,Raphael John akipiga mpira wakati wa mashindano ya mchezo huo kwa Vyuo vya Elimu ya Juu yanayoendelea hivi sasa katika vyuo mbali mbali nchini.Mashindano haya yanadhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania kupitia bia yake ya Safari Lager.
Baadhi ya Viongozi wa mchezo wa Pool Mkoa wa Iringa pamoja na wahamasishaji wa mchezo huo katika Mkoa huo wakiwa kwenye picha ya pamoja.
Naibu Meya wa Mkoa wa Iringa,Mh. Gervas Ndaki (kulia) akisalimiana na washiriki wa mchezo wa pool kabla ya kuanza kwa mashindano hayo yanayodhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania kupitia bia yake ya Safari Lager.


Wilfred Moshi awa Mtanzania wa Kwanza kufika kileleni mwa Mlima Everest ambao ni mlima mrefu kuliko yote Duniani

Wilfred Moshi amekuwa Mtanzania wa Kwanza katika historia ya Dunia,kupanda Mlima Mrefu kuliko yote Duniani,Mlima Everest uliopo kule nchini China.Pichani ni Mtanzania Wilfred Moshi akiwa kileleni kabisa mwa Mlima huo huku akiipeperusha vilivyo Bendera yetu ya Taifa.

kwa kusoma zaidi juu safari nzima ya Mtanzania Mwenzetu,Wilfred Moshi kwenda huko mlimani.
AU 


DIFFERENT ACTIVITIES OF PRESIDENT KIKWETE IN WASHINGTON DC

President Jakaya Kikwete speaks at the Centre for Strategic and International Studies (CSIS) during a Stateman's forum on development themed "A country Transformed: A New Agenda for Tanzania".
President Barak Obama of the United States of America mingles with the crowd after delivering his Keynote Speech at the opening of the symposium themed "Food Security at the G-8: Changing the development landscape" at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.
President Jakaya Kikwete meets UK's Secretary of State for International Cooperation Hon Andrew Mitchel in the sidelines of the symposium themed "Food Security at the G-8: Changing the development landscape" at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.
US Secretary of State Hillary Clinton for a souvenir wraps up the symposium themed "Food Security at the G-8: Changing the development landscape" at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.
President Barak Obama of the United States of America introduces President Jakaya Kikwete as he acknowledges the presence of four African leaders present symposium themed "Food Security at the G-8: Changing the development landscape" at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC. The session outlined key components of the G8 deliverables for food and nutrition security. Others were HE Meles Zenawi, Prime Minister of Ethiopia, Prof. John Evans Atta Mills, President of Ghana and African Union Chairman and President of Benin, HE Dr Boni Yayi.
Tanzania's envoy to the US Ambassador Mwanaidi Sinare Maajar with the Permanent Representative of the African Union to the UN. Ambassador Amina Salum Ali and Senior advisor to the President of Tanzania (Diplomacy) Ambassador Liberata Mulamula take a break after a consultation meeting of leadership on the follow-up of G-8 commitments on the sidelines of the symposium themed "Food Security at the G-8: Changing the development landscape" at the Ronald Reagan building and International Trade Centre in Washington DC.


TANZANIA YAWASILISHA MAONI YAKE KUHUSU KILIMO KATIKA KUHIMILI MABADILIKO YA TABIA NCHI

Washiriki Kutoka Tanzania kulia Bi Fauzia Haji kutoka Idara ya Mazingira Zanzibar,Katikati Bi Imelda Adam Afisa Mazingira mwandamizi Ofisi ya Makamu wa Rais na Bw. Ladslaus Kyaruzi Afisa Mazingira Mwandamizi kutoka Ofisi ya Makamo wa Rais wakijiandaa kuwasilisha mada kwa niaba ya nchi za Africa katika mkutano wa Sayansi na Taaluma ya Mabadiliko ya Tabia Nchi unaendelea Mjini Bonn Ujerumani kuhusu Madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabia nchi.

NA EVELYN MKOKOI

Tanzania kama nchi nyingine zinazoendelea imepata fursa ya kuwasilisha maoni yake kuhusu kilimo katika kuhimli mabadiliko ya Tabia nchi katika mkutano kimataifa wa 36 wa sayansi na taaluma ya mabadiliko ya tabia nchi, unaendelea mjini Bonn Ujeremani.

Akiwasilisha maoni hayo, katika Mkutano huo Afisa Mazingira Mwandamizi kutoka Ofisi ya makamu wa Rais Bi Emelda Taikwa Adam ameeleza kuwa, nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania zinatakiwa kuangalia zaidi katika kuhimili mabadiliko ya tabia nchi ili kuweza kuongeza uzalishaji na kuhakikisha usalama wa chakula kupitia sekta ya kilimo kwani ndo uti wa mgongo wa Taifa.

Bi Emelda aliongeza kuwa, katika kuhimili mabadiliko ya Tabia nchi Tanzania kupitia sekta ya kilimo na tafiti zilizokwisha fanyika kuonyesha kuwa kuna matumizi salama ya mbegu zinazohimili ukame, pamoja na matumizi sahihi ya kilimo cha umwagiliaji, na kuna kila sababu ya matumizi ya teknolojia zaidi ya kisasa na kujenga uwezo kwa wakulima wa kawaida ili kuweza kuhakikisha usalama wa chakula.

“Tafiti zinaonyesha kuwa kilimo huchangia 13% katika kuzalisha gesi joto hivyo basi kuna umuhimu mkubwa wa kuingiza masuala ya kilimo katika kuhimili mabadiliko ya tabia nchi, kwa sababu nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania hutegemea kilimo alisisitiza.”

Akizungumzia athari za mabadiliko ya Tabia nchi katika sekta ya kilimo bi Emelda amesema kuwa, kupungua kwa mvua kunakopelekea ukame nchini na kuongezeka kwa gesi joto kumeathiri kwa kiasi kikubwa sana sekta ya kilimo, na katika kupunguza gas joto katika kilimo kunahatarisha usalama wa chakula na kupoteza ardhi kwa wenyeji.

Aliongeza kuwa pamoja na kwamba sekta ya kilimo imekuwa na mikakati mbalimbali inayotekelezeka katika kuhimili mabadiliko ya tabia nchi, Tanzani inatakiwa kuwa na mfumo ambao utahakikisha kuwa upunguzaji wa gesi joto katika kilimo unatokana na jitihada za kuhimili mbadiliko ya tabia nchi.


JK and U2's Bono talk curbing hunger with NBC's Andrea Mitchell



WATANZANIA MJINI ROMA ITALIA WAUAGA MWILI WA MAREHEMU FR. JAMES A. MBWANA

     Jeneza la Marehemu Fr. James Mbwana likiwa kanisani wakati wa misa.

Watanzania kutoka kila kona ya Roma nchini Italia, wakiongozwa na balozi wa Tanzania nchini Italia, Mheshimiwa James Msekela, pamoja na marafiki mbalimbali wa marehemu James A. Mbwana, walikusanyika kwenye misa takatifu ya kuuaga mwili wa  marehemu aliyefariki gafla jumatano tarehe 16 mei 2012 maeneo ya Termini mjini Roma akiwa njiani kuelekea Chuoni kama ilivyokuwa kawaida yake. 

Misa hii imefanyika katika parokia ya Mtakatifu Francisco jimboni Palestrina mjini Roma ambako marehemu alikuwa akitumikia na kuishi sambamba na kufuatilia masomo yake katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino kilichopo mjini Roma.  Misa iliongozwa na Mhasham Askofu Dominic, Askofu wa Jimbo la Palestrina.

Habari zaidi juu ya lini mwili wa marehemu utaondoka tutawapatieni kadri tutakapo zipata. Kwa niaba ya Jumuiya ya Watanzania Roma tunawapa pole sana ndugu, jamaa na marafiki kwa msiba huu mkubwa ambao unatukumbusha kuwa sisi binadamu hapa duniani ni wapita njia tu. Siku yoyote mwenyezi Mungu anaweza kutuchukua. Kwa hiyo hatuna budi kujiandaa kwa kusali na kutenda mema mbele ya mwenyezi Mungu.
 Bwana ametoa, bwana ametwaa jina lake liidimiwe milele amina! 

Kwa habari zaidi tafadhali tembeleeni www.watanzania-roma.blogspot.com
   Kutoka Kushoto ni Balozi wa Tanzania nchini Italia, Mh. James Msekela pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Roma Mh. Leonce Uwandameno wakati wa ibada takatifu.
   Ibada ikiendelea.
Mwili wa Marehemu James Mbwana Ukitolewa kanisani na mapadri wakitanzania.
Baada ya misa kuisha.


Idadi ya watu
Idadi ya watu
eXTReMe Tracker