


NB: Sehemu ambazo hazijatajwa, ikiwa hata mikoani na visiwani, msaada tutani wadau
Kikosi Kazi cha Voice of America (VOA) idhaa ya Kiswahili kinawatakia wadau wote wa Globu ya Jamii heri ya mwaka mpya. Ujumbe: Tuendeleze libeneke. Toka shoto ni Juma Nkamia, Mwamoyo Hamza (mkuu wa idhaa), Mkamiti Kibayasi,Khadija Riyami na Sunday Shomari na kwa upande wa nyuma Abdu shakura Aboud,Ester Ewart na Duane Collins.
banda letu maoneshoni athens

Mwaka mpya, na mambo mapya. CRDB inakuja na droo zitazotokana na Manunuzi ya Bidhaa na huduma kwa kutumia TemboCardVisa, ambapo walengwa ni wateja wote wa Benki ya CRDB na watumiaji POS za Benki ya CRDB.
Mabalozi mbalimbali wamejitokeza kutoa rambirambi na kuweka saini daftari la maombolezo ya kifo cha Mzee Rashid Mfaume Kawawa hapa Ubalozi wa Tanzania, London. Ubalozi huu umefungua kitabu hicho leo asubuhi kufuatia kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Pili wa Rais kilichotokea jijini Dar es Salaam tarehe 31 Desemba 2009.
Balozi wa Zambia, Profesa Royson Mukwewa akiweka sahihi yake. Yeye alimwelezea Mzee Kawawa kama "Shujaa Mkuu wa Tanzania na Afrika aliyejitolea muhanga kupigania ukombozi wa Bara zima." Alisema njia pekee ya kumuenzi Mzee Kawawa ni kuendeleza yale aliyoyapigania wakati wa uhai wake.
Balozi wa Papua New Guinea, Bi Jean L Kekedo, O.B.E. akiweka sahihi yake. Amesema "Tunatoa pole kwa kifo cha kiongozi huyu mkuu."
Balozi wa Ghana, Profesa Kwaku Danso-Boafo akiweka sahihi na kusema "Afrika imempoteza kiongozi wa kipekee. Bwana Kawawa alikuwa kiongozi aliyetutia hamasa wanasiasa wengi Afrika, wengi wetu tuliingia kwenye siasa kwa kufuata nyayo zake. Alichangia kiasi kikubwa kwa ukombozi wa Afrika."
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania waishio UK, Ndugu Abubakar Faraji akiweka sahihi yake. Kwa majonzi makubwa amesema jina la Simba wa Vita halikuja hivi hivi na kwamba ni kweli Mzee Rashidi Mfaume Kawawa alikuwa sima wa vita vyote vya Tanganyika na baadaye Tanzania, akisimama kidede katika shida na raha zote nchi ilipitia. Na kwamba endapo Mwalimu Nyerere alikuwa wino basi Mzee Kawawa alikuwa kalamu na kwa pamoja waliweza kuiandika historia ya kipekee ya Tanzania ambayo ni kisiwa cha upendo, amani na utulivu kutokana sio tu na busara zao bali pia kwa kuona mbali na kuunganisha matabaka yote.
Baadhi ya washiriki wa kongamano la watanzania Tamil Nadu wakiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi nje ya ukumbi wa mkutano wa Holy Cross brothers, Chennai.
Mashindano ya kuwania kombe la mapinduzi ya yanayodhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania yanatarajiwa kutimua vumbi kesho katika viwanja vya Mao Tsetung na Uwanja wa Karume Jijini Dar es Salaam.

nadir haroub canavaro alikuwa na kazi moja tu, kumkaba drogba asifurukute
kipa mwalami wa Taifa Stars akitahayari baada ya drogba kupiga bao, kisha kujiangusha na kujifanya kaumia. aliamka na kuendelea na gemu
mtangazaji mahiri wa mpira wa TBC 1 Chacha Maginga (kuumeni) akiwa na mchezaji wa Yanga wa zamani aliye masomoni kusaka nondozzz Ali mayai wakichambua mchezo kama karanga
Sensei Alfred Malekia akiwaelekeza watoto nini cha kufanya. Sensei Malekia, ambaye ni kiongozi wa dojo (shule ya karake) ya Tanzania Goju Ryu Karate-Do inayotumia mtindo wa Jundo Kan-Kuroobi Kai (badala ya Jundo Kan Shibu) ya Okinawa, Japan, inaendeleza libeneke la sanaa ya kujilinda kwa mikono mitupu katika ukumbi wa shule ya msingi ya Zanaki kila siku jioni. Leo hii wanafunzi watano wametunukiwa mikanda myeusi shahada ya kwanza na wawili wametunukiwa mikanda ya kahawia katika sherehe fupi zilizofanyika hapo dojo usiku huu. Sensei Malekia amesisitiza umuhimu wa vijana na watoto kujiunga na mazoezi hayo ambayo humlea mwanafunzi kuwa na nidhamu ya hali ya juu katika jamii.
watoto wakicheza kata ya kwanza ya Goju Ryu
Francis Kabika Sizya anaachana na mkanda wa kahawia na kuvalishwa mweusi baada ya kufuzu
Benki ya NMB ilileta burudani ya aina yake
promo za wafadhili kwa kwenda mbele
vuvuzella ndani ya nyumba
Tajania oyeeee!
Kocha wa makipa Juma Pondamali akiwa kazini
Ivory coast wakipiga jalamba
Marcio Maximo na vijana wake
Nahodha wa Taifa Stars Nsajigwa akibadilishana bendera na nahodha mwenzie Didier Drogba wa Ivory Coast
Shilingi inarushwa kuchagua upande wa kuanzia
waamuzi na manahodha na wasimamizi katika taswira ya pamoja ya kumbukumbu
Ivory Coast
Taifa StarsExclusive interview between Jamii Blog and Taifa Stars coach on Tanzania's soccer development plans
wachezaji wa ivory coast baada ya dina la mchana
kila mtu alikuwa anahamu na drogba
nyota wengine wa ivory coast
baadhi ya wachezaji wa taifa stars. toka shoto ni nizar khalfani, nsajiwa na mrisho ngasa
Kocha wa timu ya Ivory Coast, VahidHalihodzic akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mchezo wao dhidi ya timu ya Taifa stars utakaofanyika kwenye Uwanja wa Taifa leo
Mchezaji wa timu ya Taifa ya Ivory Coast na Chelsea Didier Drogba akitoka kupata dina la mchana Hoteli ya Kilimanjaro Kempinski jijini Dar ambako timu hiyo imefikia. Wacheaji wote isipokuwa mmoja tu, wanacheza soka la kulipwa nje ya nchi yao. Leo wameanza tizi neshno na kesho watakipiga na Taifa Stars. Leo askari walikuwa na adabu na kila mtu kafanya kazi yake bila zogo linalosababishwa na kutaka sifa kusiko msingi kwa badhi ya hawa askari wetu ambao wanapenda kutumia nguvu nyiiiingi na maarifa kiduchu..
Mchezaji wa timu ya Taifa ya Ivory Coast na Arsenal Emmanuel Eboue akisaini katika fulanazzz ya mtoto aliyefika kwenye Hoteli ya kilimanjaro Kempiski kuwaona wachezaji hao
Wachezaji wa timu ya taifa ya Ivory Coast kushoto Yaya Toure na kulia Bajari Kone.Lovely Gamble Soundtrack 'Hatakama' by Mkazuzu feat Spilla. the track was produced Josh @ Urban Pulse in conjunction with Mzuka label. the video was produced UrbanFilmz a B Magazine production studio. The movie features Steve Kanumba the Great and shot in London
naibu waziri wa habari, utamaduni na michezo mh. joel bendera akiwapoza wanahabari waliotaka kususia kukava ujio wa drogba na ivory coast usiku kuamkia leo uwanja wa ndege wa julius nyerere jijini dar baada ya askari kuwajia juu wanahabari na kuwazuia wasifanye kazi zao kwa sababu wanazozijua wenyewe.
huko nje ya fensi mashabiki walikuwa wanamsubiri drogba na wengie kwa hamu. waliambulia kumuona kiduuuuchu tena kwa mbali
wanahabari wakiwa wamesusia kukava ujio wa ivory coast baada ya kunyanyaswa na askari uwanja wa ndege
wanahabari wakiweka msimamo wa kususia baada ya askari kuwanyanyasa katika kukava ujio wa ivory coast. hakuna mpiga picha aliyepiga picha ujio huo.