video ya sehemu ya maneno yaliyotamkwa na spika wa Jamhuri ya Muungano Mh. Samwel Sitta muda si mrefu uliopita. kunradhi picha si ya ubora wa juu ila sauti ni mswano

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 35 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 30, 2009

    Huyu sasa anasahau majukumu yake yeye ni spika wa wabunge sio wa wananchi sio kila kinachooandikwa kwenye internet ni uzushi mengine ya kweli.asisahau ule uhuru wa vyombo vya habari na wala asije kutunga sheria zake
    Habari ndio hiyo ndugu spika

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 30, 2009

    huo ndio uwazi na uwajibishaji. ukiwa msafi uhandamwi. mbona hawajamsema Pinda au Shein? kwa nini wakuseme wewe? tujibu. Pikipiki wapi na wapi na uchaguzi? Ya richmond na epa yalianza hivi hivi na ukayabeza eti yanatoka kwenye internet. matokeo yake kila mtu anajua sina haja ya kuelezea. Bunge likuundie TUME.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 30, 2009

    Jamani, kama speaker yuko terrorised kiasi hicho, nani yuko salama? Usalama wa taifa wako wapi mpaka mkuu wa muhimili wa pili wa serikali anakuwa na woga kiasi hicho?

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 30, 2009

    Kaka Asante kwa kutupa hint hii muhimu. Nafikiri ni habari njema sana hasa kwa watanzania wa leo, kupata maelezo yenye usahihi kuhusu maneno ambayo yanavumishwa hasa kipindi hiki. Kwa wale wana-blog ambao wako nje ya Tz wanaweza wasielewe sana hali halisi kwa sasa, ila kwa wazoefu wanaweza kufahamu kuwa tunakaribia kipindi cha uchaguzi mkuu mwakani (2010). Kwa kawaida wanasiasa ambao hawajatulia huwa wanatumia muda mwingi kuchafua wenzao ili yeye aonekane safi... Lakini ukweli anayemchafua mwenzake kwa uongo, huyo ndio mchafu zaidi... Ombi langu tuwe macho sana... Watanzania tuna akili sana ya kuona na kuamua..tuzitumie hizo kuweza kuchagua mchele safi na chuya tutupe shimoni...

    Nsa

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 30, 2009

    Hongera sana muheshimiwa, sasa mambo yameiva, si uwataje tu au uwapeleke polisi, kwa nini ulinde hivyo , si kuna vyombo husika, jamani viongozi wetu, tunawaomba muwe wazi; kama wanakuonea wivu we kuwa wazi na wawajibishe badala ya kutoa vitisho. Watanzania tuwe macho kwa kila kinachosemwa mwaka kesho ni uchaguzi. AU unasemaje? lazima tuwapige maswali kuhusu hizo habari wanazo toa, Il tujue ukweli.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 30, 2009

    Michuzi sikujua nilitolee wapi dukuduku langu. ila nadhani sasa kuna baadhi ya mambo inabidi kama ni ushamba basi tupunguze kidogo. Hivi kumkabidhi Waziri Mkuu ripoti ya hujuma za Ubungo ikiwa imefungwa kama zawadi ya harusi ni ulimbukeni au ndio fasheni? Manake nimebaki hoi, kwa tafsiri ya harakaharka ni kwamba wamempa Waziri Mkuu zawadi akajipongeze! Huu ni uhuni na haswa ofisi inayoshughulikia masuala ya matumizi ya umma huu ni ubadhirifu usio wa lazima (kama kuna wa lazima)

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 30, 2009

    hongera ziwafikie wana vyombo vya habari kwakutuhabarisha, mtambue kama alivyosema unonymous wa mwisho watanganyika sasa ni watanzania waliofunua ubongo, vyovyote watakavyo jitetea, shughuli palepale tumechoka na danganya toto. politcs! 2010 kazi kweli kweli!!!

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 30, 2009

    ANONY WA 12:40, WATZ WALIONJE WAPO INFORMED SANA KULIKO WALIO TZ HASA ISHU HIZO ZA SIASA. WANAFUATILIA SANA KWANI WANAVYANZO VINGI SANA, NA WANAKATISHWA TAMAA NA TABIA ZA VIONGOZI WETU KUUMA NA KUPULIZA. KWA NINI SPIKA ASISEME SIO KWELI, NA AJITETEE KWA USHAHIDI. MSUMARI WA MOTO UMEINGIA KUMOYO HASAAAA.
    NAOMBA KUWASILISHA MITHUPU,HII IMETULIA, HATA YA RAIA MWEMA NAYO YA MEREMETA WATASEMA NI INTERNET STORY. MITHUPU NAWE JIANGALIE KWANI NAWE UNAMILIKI CHO CHA UTOAJI MAONI NA UPASHANAJI HABARI.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 30, 2009

    Mmmh! Mzee mzima mambo yamemfika mpaka anasema ulinzi alionao hautoshi?
    Pambana usitumie jukwaa hilo kwa maslahi binafsi.

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 30, 2009

    Huu ni uhuni. Ana uhakika gani kwamba atakuwa spika? Je anajua kama chama chake kitashinda? Mimi kwa kweli naona hii ni kuwakejeli watanzania wote!! Demokrasia ya kweli iko wapi iwapo hata spika atakuwa kama dikiteta? Naomba kutoa hoja!!!

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 30, 2009

    Michu,

    Weka hiyo atiko ya mwananchi iliyotoka ikisema "JK akana RICHMOND". Ningependa tuijadili.
    Naomba kutoa hoja

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 30, 2009

    six anaomba aongezewe ulinzi kwa pesa za nani? walipakodi? jamani hivi jasho la mtamzania limekuwa la kuchezewa hivi? cha msingi hapo ajibu shutuma juu jake na ajibu kwa vithibitisho na mamlaka husika zichukue hatua sio tu kukaa kimywa ama kushabikia. inafikia sasa watanzania tuache kuteteana na kuweka ukewli bayana na tutafute jia sahihi za kutatua matatizo yetu! kama tutaendelea kuleana na kuteteana na kuona kama hayatuhusu kunasiku tutalia na kusaga meno na kukumbuka nyakati hizi. jamani tubadili tanzania kwa kizazi kijacho bila kujali hadhi ya kiongozi wala mali. mzee six sema ukweli usiwe na jaziba na kutumia mic zinazolipiwa kodi na walala hoi kutishia watu na kujigamba! ni wakati wa ukweli sasa

    chief oderee
    mfalme wa kitaa

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 30, 2009

    Nachoweza kusema huyu,Spika Mnafiki,wakati anaandikwa Lowasa na wengine na m,agazei hayo hayo makini yalionekana mazuri sasa yanamgusa yeye anayapa sura ya uadui ili Watanzania wasiyaamini,wote viongozi wa CCM wachafu na X PM alisema wakati anaachngia nagi hatobaki mtu na hakika mtakwisha na mtamalizana wenyewe.Watanzania tukumbuke Spika huyo huyo alimbambika mtu tuhuma za uongo za uchawi Bungeni.mimi nasema waende zao na hafai kuwa Spika ni mroho wa madaraka na mtaka sifa tu.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 30, 2009

    kuongezewa ulinzi pia ni ufisadi,watu waachekufanya kazi za kujenga taifa wakae wakikulinda wewe mtu mmoja ndani ya watanzania wangapi,na inaonekana wewe tu ndo una maadui siyo,wataje basi hao maadui wako ili uwe na ulinzi wa kutosha kwa kuwakazia macho

    ReplyDelete
  15. AnonymousJuly 30, 2009

    Kaka Michuzi ninashukuru kwa hii habari,kweli mambo bado kabisa Tanzania.

    How comes the speaker of the house of representatives is terrified and seeks additional security.Why do I think he does not feel safe?

    From what i know, some of the qualities of speaker are integrity which is straightforwardness and honesty in all his professional duties.Conducting house proceedings.

    He is supposed to be objective meaning he should not allow bias( "Tutashinda uchaguzi na nitakuwa speaker") and conflicts of interests.It seems from his words,he allowed bias presumably unfair favouring some people hence conflicts.

    The speaker has got to be independent which will avoid threats such as familiarity,and advocacy to one strong side( majority) hence rendering his obligation prone to attack then conflicts.Therefore he is fearing for his life.

    Thus why Mr Michuzi,from my incomplete leadership issues article,i stressed responses from executives to be scrutinized effectively and people to debate.

    I do not wish to compare TZ to UK but the above fundamental issues ought to be observed in houses where there are opposition to policies.Internal party issues and external.UK has another speaker after the expulsion of the other due to incompetence,bias,poor judgement on MP expenses skendo.

    So Mr Sitta has right to seek protection and I suggest,he should counter forces by observing fundamental principles of the house.From his words,Clearly,he is bias,unprofessional and advocating to one side.

    His deputy, as well,has same problems for being pro government for self interest knowingly that the general election is on horizon by protecting budget scrutiny by profihibiting nosy questions that are likely to stir up proper contention of issues.

    So kaka michuzi,it is vividly seen how political issues are undertaken in our country such that politicians are fearing for their lives.

    I could write endlessly on these issues and seek debate as I did on leadership issues article.Could I send you Part II?Anyway let others comment.Later

    Mdau ( John ) UK

    ReplyDelete
  16. HAYA NDIO MAMBO YA KUPOST KWAI NI YA KITAIFA NASIO KUTUPOSTIA MASHATI YA KIJANI KWENYE BLOG YETU YA JAMII.

    ReplyDelete
  17. AnonymousJuly 30, 2009

    Kwa kweli nimesoma hizo article kuhusu 6 na naona tangu alipoingia madarakani amekuwa akiiongoza ofisi ya bunge kidikteta. Lakini mimi lazima nataangukia kwenye upande wa habari zinazotoka kwa maana bado sijaona maaendeleo yetu sisi wantanzania na mapesa yanatumika tu mabilioni kwa manufaa ya nani???

    ReplyDelete
  18. AnonymousJuly 30, 2009

    yaani hiyo nyumba ni ya kuongelea mambo hayo. mbona anaweka hoja zake sehemu ngumu kujadiliwa na wengine. halafu ulinzi wa nini? mwanzoni nilimwona wa maana sana kumbe hamna kitu. hivi kweli watanzania tunachezewa kiasi hiki.

    naombeni kuuliza. check and balance kwa wabunge ni wapi? tofauti na sheria zao ambazo mahakama inaweza kucheki? nadhani kuna mwanya hapo ndo maana wanafanya watakavyo.

    ReplyDelete
  19. AnonymousJuly 30, 2009

    Mimi nasema huyu Spika ameanza kufanya Kampeni,tena anatumia jukwaa la Bunge,ningependa jambo hilo likomeshwe kabisa,kama kuna mtu huko anamuohofia kapeleka pikipiki na yeye awapelekee gari kwanza Watanzania tumechoka kuongozwa na watu masikini kama yeye anaeganga njaa!!,ohho unachafuliwa,unatungiwa,sisi tunajua nyinyi wote humo mna makundi na kila kundi lina magazeti yake.wewe Spika huwezi kusemwa hata siku moja katika magazeti ya Mzee Mengi kwa kuwa ndiyo kambi yako.

    Lakini magazeti hayo hayo kila siku yanataja mahisimu wenu kwa majina mabaya ya wezi,wahujuhumuna mafisadi kama vile hawana familia ndugu na jamaa wanaowaheshimu.

    Kuna Bwege mwingine aliwahi kutumia Bunge kuombea magazeti ya Bwana wake matangazo kwa Serikali sasa sisi siyo mafala tukomomeni kabisa.

    Acha magazeti yaandike wote ninyi humo ndani,mmezidi kubana habari tupate uapnde mmoja tu ya watu wasiyo na magazeti na nyinyi wenye magazeti tusipate upuuzi wenu.

    ReplyDelete
  20. huo ndio uwazi na uwajibishaji. ukiwa msafi uhandamwi. mbona hawajamsema Pinda au Shein? kwa nini wakuseme wewe? tujibu. Pikipiki wapi na wapi na uchaguzi? Ya richmond na epa yalianza hivi hivi na ukayabeza eti yanatoka kwenye internet. matokeo yake kila mtu anajua sina haja ya kuelezea. Bunge likuundie TUME

    ReplyDelete
  21. AnonymousJuly 30, 2009

    MICHUZI NAONA UMEKUA SASA!!! NAONA TARATIIBU NAWE UNAANZA KUBADILIKA. UNAANZA KUWA NA AKILI SASA!!! SAFI SANA, YALE MAMBO YA UCCM CCM TU NAONA UNAANZA KUYAWEKA KANDO BAADA YA WATU WENYE AKILI ZAO KUANZA KUIPONDA BLOG YAKO!!! HIVYO NDIVYO UNAVYOTAKIWA KUWA KWANI TANZANIA YETU ITAJENGWA NA SOTE UKIWAMO WEWE. WEWE UKIWA WA AJABUAJABU LEO WAKATI UNAANZA KUZEEKA UJUE UNAWAANDALIA NCHI MBOVU WANAO!!! THE TRUE MEANING OF BLOG YA JAMII NDO HII SASA. SIO ZAMANI MAONI YAKIWA CRITICAL TU UNAYATIA KAPUNI!!!
    UMEONA KATIKA MAONI 18 YA MWANZO KARIBIA 96% YA MAONI WAMEMPONDA SPIKA NA HOJA ZAKE. YEYE ANA UHAKIKA GANI KUWA NI LAZIMA ATASHINDA UCHAGUZI KAMA SIO YALEYALE MABAVU NA NGUVU ZA DOLA WANAZOTUMIAGA CCM KUPOLA KULA ZA WATANZANIA!!!!
    WAJUE MWISHO UPO NA UNAKARIBIA!!
    Mdau kutoka BIDII Forum + JF
    GA,USA

    ReplyDelete
  22. A third world country in a G8 media spin. With recent 'Fibre optic' internet boost in TZ this entails to more exposure of our govt leaders 'ufisadis' and I trust this would be in wananchi's favour. Developed countries would be exposed to 'ufisadi' prevailing in TZ and foreign funded projects would be closely monitored by the donors to the benefit of the intended recipients as opposed to the fisadi leaders hence the intended civilians continue to suffer.
    I commend the technological advancement in our country, Radio and TV stations have somewhat failed to shed more light on issues relating to our govt leaders due some strict rules set by 'them' so as to protect their interests to the eyes of the general public in favor of winning votes during general election.
    But time has come for our leaders to be 'striped' out in 'black and white' and the general public need to be alerted of the truth behind the people they've elected lest we end up developing individuals rather than developing the country as a whole. Internet rules, fibre optic optimise the connection and let the world know the truth...

    Mungu Ibariki Tz.

    ReplyDelete
  23. AnonymousJuly 30, 2009

    huyu mtu hatufai toka aingie yeye bunge limekuwa la majungu, makundi na lisiloelewa. Bunge sasa limekuwa kama nyumba ya majungu tu lakini mbona wakati wa msekwa kulikuwa hakuna hv vitu bunge lilikuwa na heshima yake anazungumzia maadui zake yeye c alichekelea wakati kina lowassa wanaondolewa kwenye madaraka akaacha hadi safari ya nje aliyokuwa naye ili awepo kwenye kikao cha kujadili ripoti ya richmond siku hazigandi mzee, yeye anataka kumkosoa kila mtu kwani yeye ni msafi. Uchaguzi wenyewe alitumia pesa nyingi sana yeye na mwenzie salim ahmed salim ilimradi akishinda akaibomoe serikali ya kikwete na kwa kiasi kikubwa kafanikiwa lakini sasa ndi mwish wake.naomba kuwasilisha hoja

    ReplyDelete
  24. AnonymousJuly 30, 2009

    Kuna mambo matatu yaliyonigusa katika maneno ya spika:
    1. Ametumia maneno "maadui zangu". Japo wahenga walisema Adui Mpende, kwa kawaida wanadamu huenda kinyume. Uadui wa Mmatumbi kwa Mmatumbi hauliletei taifa letu manufaa yoyote!
    2. Amesema wabaya wake "wako Dar es Salaam wanamsikiliza". Inaashiria kwamba anawafahamu hao watu ambao anawaita wazushi. Kama kweli kuna watu wanaoleta uzushi na kitendo chao ni kinyume cha sheria kuna vyombo vya dola vinatetea haki za kila mwananchi. Natumai spika amevipa vyombo vya dola taarifa na ombi lake la ulinzi kwa Waziri Mkuu linamaanisha kwamba angependa Waziri Mkuu atambue kwamba vyombo vya wizara ya mambo ya ndani vimepewa kazi.
    3. Ni kama amejihakikishia Uspika kama asipokumbwa na mambo yaliyo nje ya uwezo wa kibinadamu. Haya ni mambo ambayo Watanzania hawataki kuyasikia ya uongozi kuwa utawala wa kisultani. Kibaya zaidi wanapoenda watu Urambo na kusaidia kuleta maendeleo wanaonekana ni maadui wa Spika wanaotaka kuchukua kiti chake. Kile kiti sio chake, ni cha Watanzania. Kazi ya kuchochea harakati za maendeleo ya Urambo sio mpaka uwe mbunge tu, hata ukiwa Mtanzania mwenye nia na uwezo wa kufanya japo jambo dogo, uwepo wa mbunge haupaswi kukuzuia. Kina Mashaka waogope kutoa misaada kwenye hospitali kwa ajili ya kumwogopa mbunge ataelewaje???? Tutakuwa hatufiki!!!

    ReplyDelete
  25. AnonymousJuly 30, 2009

    Nilidhani SPIKA anachaguliwa, Kumbe kuna wengine wakiwa hai tu washakuwa maspika??? eti Mungu akiniweka HAI NTAENDELEA KUWA SPIKA...Huu ni ubaradhuli uliopita mipaka. SPIKA anasupport rushwa kwa kusema wakipewa PIKI PIKI wanaongezewa uchumi na kuondoa Umasikini??

    ReplyDelete
  26. AnonymousJuly 30, 2009

    Nyie mnaomponda spika inaonyesha ni kiasi gani hamjui siasa za nchi hii. Huyu ni spika wa kwanza kuruhusu mjadala wa kuiadhiri serikali kwa rushwa na kufanya waziri mkuu ajiuzulu. Spika wa kwanza kuruhusu marais wastaafu waelezwe ukweli bungeni kutokana na walivyotuibia. Mafisadi sasa hivi hawana raha sababu anaruhusu mijadala kwa kina kuliko spika yeyote aliyewahi kutokea nchi hii. sasa ukizingatia amewabania mafisadi ulaji, hivi ni kitu cha kushangza kuona hizo tuhuma za maji taka mitandaoni. Ana mapungufu ndio, lakini kwani nani hana?

    Ripoti ya CAG ambaye ofisi yake ina mamlaka ya ukaguzi na wataalamu wa hali ya juu wa auditing, wameipa ofisi ya spika clean report ya matumizi kwa mwaka ulioisha. Vitabu vipo in order.

    Sasa huko kukaa kwenu ulaya na kudhania habari za mtandao niza kuzichukulia jumla, mungeanza na wamarekani wanaosema Obama ni rais batili sababu alizaliwa kenya na kwenye internet hizo habari zimejaa...Mnasemaje?

    Acheni ujinga wa kudandia kila stori na kuimeza nzimanzima kama chatu, mkishaimeza ndo mnakua kama mazezeta sasa, mafisadi wanawang'ong'a!

    Watu wanapanga foleni sinza kuchukua bahasha za kuja kuwasafisha mafisadi na nyie wengine mdandania treni kwa mbele kama mandondocha.

    Michuzi usinibanie comment wapuuzi wanaibiwa nchi yao huku wanajiona halafu yanabaki ushabiki tu.

    ReplyDelete
  27. Nimeandika makala fupi kuhusu kuandamwa kwa spika. Nimejaribu kuuliza maswali ambayo ikiwa Spika ataweza kuyajibu kunaweza kuleta mwanga juu ya nini kinachoendelea. Inapatikana hapa: http://drfaustine.blogspot.com/2009/07/ya-spika-wa-bunge.html#links

    Mdau
    Faustine

    ReplyDelete
  28. nambawaniJuly 31, 2009

    MIMI NAFIKIRI KUNA KITU HAMJAKIELEWA AMBACHO AMEONGEA 6,NI KWAMBA KAOMBA ULINZI KWA MKUU,NI KWAMBA ULINZI ALOOMBA NI KUHUSU UCHAGUZI UJAO KUTOKA SERIKALINI WAKUWEZA KUMUWEKA TENA MADARAKANI NAFIKIRI MIMI NDIO ALICHOOMBA HICHO.MAANA KAMA ULINZI ANAO TAYARI,NINI ANATAKA KAMA SIO KULINDWA KTK UCHAGUZI?.NAWAKILISHA!

    ReplyDelete
  29. AnonymousJuly 31, 2009

    HAKUNA VITU VIPYA .TUWE WAWAZI UCHAGUZI KARIBU KUPAKANA MATOPE,KASHIFA NA SIASA CHAFU NDO MUDA WAKE HUU...SIX ULIHAMA KUNDI,AMBALO LILIKUWEKA HAPO..WANATAKA KITI CHAO...BLOG IWE
    HURU SIO GREEN TU...

    TANGANYIKA MZALENDO

    ReplyDelete
  30. AnonymousJuly 31, 2009

    Vita ni Vita Mr Sitta, Pambana ndo sihasa hiyo uliyataka mwenyewe, kwani ulimaliza mkataba Pal uwekezaji au mbio zako za kutaka makubwa, Ukubwa jaaa la taka unalalamika vipi? achia uspika na ubunge kama kuna mtu atakufuata urambo ukiwa unalima Tumbaku yako na kula michembe

    ReplyDelete
  31. AnonymousJuly 31, 2009

    NAUNGANA NA ANONYMOUS WA 11:29 KWAMBA WATANZANIA TUWE TUNAJARIBU KUCHAMBUA HOJA WA KUANGALIA PANDE ZOTE MBILI! SIKATAI SIX ANAMAPUNGUFU YAKE! LAKINI HATA SIKU MOJA SITA HAWEZI KUFANANISHWA NA MSEKWA! HUWEZI KUSEMA SIX NI DIKTETA KULIKO ALIVYOKUWA MSEKWA NA WENGI TUNALIJUA HILI! NI UKWELI USIOPINGIKA KUWA TUKIWEKA SIASA PEMBENI NI SPIKA WA KWANZA AMBAE AMELIFANYA ANGALAU BUNGE LIWEZE KUWAJIBIKA! NDIO TUNAWEZA TUKASEMA KUTOKANA NA MAKUNDI LAKINI SISI KAMA WANANCHI TUNACHOANGALIA NI MATOKEO! TUMEONA ANGALAU SASA HATA BAADHI YA WABUNGE WENYE UJASIRI WANAONGEZEKA! TOFAUTI ZA ENZI ZILE NI ALIKUWA MZINDAKAYA NA NJERU KASAKA TU! MIMI NIKIASHA PEMBENI MAPUNGUFU YA SIX LAZIMA NIKUBALI BUNGE LIMEBADILIKA ACHILIA MBALI MAKUNDI, MITANDAO, U-CCM NA UKANDA! NAPENDA KUSEMA TUTAFIKA TU

    ReplyDelete
  32. kaka asante kwa habari hii mimi nimeona waraka wenyewe kusema ni mbaya kwa wafanyakazi wote wa bunge si spika peke yake lakini baadhi ya maandishi ni uzushi mtupu hayana ukweli ndani yake alafu hakuna adress ya mwandikaji bali ni mambo ya kutunga na mengine ni kweli lakini nafikiri ni kwasababu ya 2010 uchaguzi kama keli anajihami aweke adress na ninani au ni akina na nani kaka michuzi mimi sio mtalaam sana wa computer ila naomba utuwekee hapa uwanjani kila mtu asome ili aone mambo yalivyo ya kungaunga ni hayo tu.

    ReplyDelete
  33. AnonymousJuly 31, 2009

    Hii kauli ya maadui wangu na kutaka aondoke katika cheo alichonacho iliwahi kuitoa Lowasa katika sakata la Richmond. Hivyo kama spika ni msafi basi iundwe kamati itafiti jaombo hili kisha iwajulishe watanzania. Asifanye mambo ya ajabu, wengine wakituhumiwa huwekwa ndani chini ya ulinzi ili wasikimbie, yeye baada ya kutuhumiwa anataka alindwe. Awekwe rumande kama wangine na habari hii ifanyiwe kazi asitufanyie ujanja.

    ReplyDelete
  34. AnonymousJuly 31, 2009

    Hoja hujibiwa kwa hoja...spika aache kuleta longolongo. Tuhuma zimeandika majina na namba za magari husika. Badala ya kujibu tuhuma anaingiza mambo ya kampeni za uchaguzi ujao. Kama anaona yanayodaiwa si halali, basi ajitoe kimasomaso kupangua kila tuhuma na si porojo. Inawezekana usemi wa Lowassa kuwa "hakuna kiongozi aliye msafi" ni sahihi.

    ReplyDelete
  35. spika anatoa ajira za kidini hivi karibuni ajira wapewe wakristu watupu bungeni toka NYEGEZI.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...