Mkurugenzi wa Idara ya Habari –MAELEZO akiongea na wadau wa sekta habari leo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano wa kujadili mwongozo wa maadili ya vyombo vya habari katika kutoa taarifa za uchaguzi mkuu 2010. Pamoja na mambo mengine amewataka kuheshimu Uhuru wa vyombo vya habari uliopo nchini kwa kuepuka kuandika habari za uchochezi na matumizi ya lugha zinazoweza kusababisha uvunjifu wa amani.Bw. Deogratias Mushi mdau katika sekta ya habari akiongoza majadiliano ya mkutano wa wadau wa sekta habari kujadili mwongozo wa maadili ya vyombo vya habari katika kutoa taarifa za uchaguzi mkuu utakaofanyika nchini mwezi Octoba, 2010 leo jijini Dar es salaam.Wadau wa sekta ya habari nchini wakipiga kura kupitisha baadhi ya maamuzi yatakayozingatiwa na vyombo vya habari kama mwongozo wa maadili kwa vyombo vya habari katika kutoa taarifa za uchaguzi mkuu utakaofanyika nchini mwezi Octoba 2010.Baadhi ya wadau wa sekta ya habari wakichangia masuala mbalimbali kuhusu Mwongozo wa maadili ya vyombo vya habari katika kutoa habari za uchaguzi mkuu wa 2010 leo jijini Dar es salaam ambapo pamoja na mambo mengine wamekubaliana kutoa habari zisizopendelea upande wowote ,zenye ukweli na zenye kujali uchunguzi wa hoja.

(Picha na Aron Msigwa -Globu ya Jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. hao wadau hawafungi? naona chupa za maji tupu hapo

    ReplyDelete
  2. atanzania na sisi! Hicho chumba cha mkutano utadhani ni cha maakuli!

    The atmosphere is incongruous, indeed

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...