Majeruhi akifikishwa hospitali ya Amana usiku huu baada ya kukumbana milipuko ya mabomu kambi ya jeshi Gongo la Mboto jijini Dar usiku huu. Bado haijulikani wangapi wameumia ama kupoteza maisha katika milipuko hiyo iliyotokea kwenye ghala ya silaha za jeshi huko Gongo la Mboto na kusikika kila sehemu ya jiji
Daktari hospitali ya Amana akimhudumia mmoja wa majeruhi wengi walioletwa hospitalini hapo
Mmoja wa majeruhi akipata huduma hospitali ya Amana

Deo rweyunga wa Radio One akiongea na
mmoja wa majeruhi hospitali ya Amana

Majeruhi wa milipuko ya mabomu
Watoto wakiwa na mama yao aliyejeruhiwa hospitali ya Amana
Huduma kwa majeruhi
Mdau baada ya kupata huduma ya kwanza hospitali ya Amana
majeruhi akifikishwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili
Gari la wagonjwa likiwasili Muhimbili usiku huu likiwa na majeruhi wa mabomu hayo
majeruhi wakiwa Muhimbili
Majeruhi akiwasili Muhimbili
Daktari akiwa na mtoto ambaye kapotezana
na wazazi wake hospitali ya Amana

Meya wa Ilala Mh. Jerry Silaa, ankal, askari na Deo rwedyunga wakiwa eneo la tukio kwenye geti la kuingilia kambi hiyo ya Gongo la Mboto ambako raia walizuiwa kuingia
Wakaazi wa Gongo la Mboto na maeneo ya
jirani wakitafuta pa kwenda

Kizaazaa Gongo la Mboto usiku huu
Wananchi wakihaha huku na kule Gongo la Mboto
Mbio mbio kuepusha maafa Gongo la Mboto

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 28 mpaka sasa

  1. Poleni jamaa wote kwa maafa yaliyowakuta.M/mungu awape nafuu ya haraka kila la heri tupo wote pamoja.

    ReplyDelete
  2. Sasa hapa sijui nani wa kulaumiwa kwani tukio kama hili limetokea miaka miwili iliyopita na bado tunashindwa kujifunza kutokana na makosa yaliyopita.Mwaka huu tunatimiza miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika tunashindwa hata kuwa na kikosi cha uokoji tunapopata maafa kama haya watu wa mekuwa wabinafsi kupita kiasi hamjali wala kuangalia thamani ya maisha ya binadamu wenzenu,kumbukeni mungu yupo na wote njia yetu ni moja.

    ReplyDelete
  3. Poleni sana jamani.Kaka Michuzi na team yako asanteni sana kwa kutufikishia habari hii.Inasikitisha sana kuona katika karne hii jambo kama hili linatokea, inakuwaje jamani mpaka mabomu yanalipuka na kudhuru watu?

    ReplyDelete
  4. Serikali itueleze kwa kina kwa nini mabomu yanalipuka???????? na hii mara ya pili wananchi wanapata maafa alafu mahali pakukaa hawana wananyanyasika hawapewi hata hela ya kujenga nyumba zao ambazo zimebomoka,ichunguzwe kwanini yalipuke kuna kitu hapo kabisaaaaaaa tutaendelea kuwa masikini tuu kwa wengine kujinufaisha

    ReplyDelete
  5. Jeshi na serikali lazima watupe maelezo kulikoni maana haya mabomu yamekuwa too much sasa.

    ReplyDelete
  6. kutenda kosa sio kosa kurudia kosa ni kosa kubwa sana

    ReplyDelete
  7. Kufanya kosa ni kurudia kosa. Serikali yetu na Jeshi ni nini kinaendelea? hali hii inaumiza sana maana tunapoteza ndugu zetu wengi na wengi kukosa makazi kabisa. Maisha haya mpaka lini jamani. Poleni sana wahanga. Tuko pamoja.

    ReplyDelete
  8. Kwa kweli hii sasa imekua tatizo, Lazima serikali itoe tamko sababu ya hii milipuko. Mbona inatokea Dar es Salaam tu???? Huko mikoani hakuna maghala ya silaha??? Au silaha zinauzwa kisha kuchoma kupoteza ushahidi kwa ma'auditor??? inashangaza sana serikali isiyomakini kama hii...!!!

    ReplyDelete
  9. I am definitely Speechless.

    ReplyDelete
  10. Tunaitaji vyombo vya habari vitukomboe, ili kujua kama bwawa lina ruba lazima utibue maji

    ReplyDelete
  11. kambi za jeshi, na sehem za kuhifadhia silaha zilitakiwa ziwe nje ya mji ( uraian) amabpo mbali na nyumba za raia, tukio bhilo lilishatokea karibuni na wtu wazima na watoto waliathirika na kupoteza maisha, pale ndio ilikuwa pa kujifunza na hatua zingechukuliwa, kwasababu kama sasa hivi limetokezea tena na aliathirika ni raia, kama kambi zingekuwa nje ya uraiani haya angeepukika. lakni viongozi hawakuliona hilo, wanaona kama wangehamishia hizo kambi itawacost, laki saa hivi mtanzania ndie anaelipa hizo costza maisha yake. kufanya kosa ni kosa na kurudia kosa ni uzoefu wa makosa. maisha ya naraha jaman na kila mtu napenda roho yake, hakuna mtu amabe anataka kufa kwa excident za ajabu ajabbu na kwa vitu vinavyoweza kuepukia

    ReplyDelete
  12. Mimi MOHAMED wa MUCE IRINGA: - Makambi ya jeshi yahamishwe mbali na makazi ya watu.Au wahamie Dodoma,haipendezi kuona Watanzania wakifanywa kuwa misitu ya kujaribia ubora au ubovu wa silaha.Najua si muda muafaka kuanza kulaumiana lakini kutokana na mabomu ya Mbagala tulijifunza nini? Na serikali ilituahidi nini? Mwaka huu wasiunde tume badalake wachukue hatua madhubuti dhidi ya matatizo kama haya.POLENI SANA WATANZANIA WENZANGU kwa wakati mgumu mlionao kwa sasa Mungu atawarehemu.

    ReplyDelete
  13. Waziri wa ulinzi Mwinyi na viongozi wa jeshi wajiudhuru hawawezi kazi. Watu wamekuwa kama wakimbizi ndani ya nchi yao?
    Poleni sana mliopatwa na maafa hayo. Serikali iwajibike kwa hili siasa pembeni

    ReplyDelete
  14. Ni vema na haki hili suala la mabomu kuweza kufanyiwa uchunguzi wa kina ili kupata ufafanuzi yakini. Nadhani jambo usiololielewa ni kama usiku wa giza. Binafsi sielewi ni nini hasa sababu ya milipuko hiyo na kama yaweza zuilika au la... sioni kama ni wakati wa kulaumiana lakini kutokana na ukubwa wa madhara yake inapotokea kwa niaba ya wananchi naomba serikali na vyombo vyote husika wafanye uchunguzi na kutoa ufafanuzi kwa wananchi. Ni muhimu sana wananchi ambao ndio waathirika wakubwa kulielewa hili jambo..Vinginevyo wananchi wanapokosa imani na serikali yao ni hatari kwa taifa zima. Mwisho nawapa pole wananchi wote walioathirika na shida hii last time mbagala na sasa gongo la mboto. Kikubwa tumtumaini Mungu lakini zaidi tushirikiane katika uwajibikaji wa kuzuia maafa kama haya.Shukrani.
    Mwananchi mzalendo,
    Agnes

    ReplyDelete
  15. POLENI SANA WALIOPATWA NA HAYA MAAFA. Ila serikali yetu na wahusika wake katika kila nyanja huwa hawako makini au serious kwa kila jambo. Nina uhakika bongo watu wanaishi kwa kudra za mwenyezi Mungu na si vinginevyo. SERIKALI INABIDI IWAJIBIKE HASA KATIKA HILI.

    ReplyDelete
  16. My Dear minister of defense i think its wise to resign now. Sympathise with the loss of lives. Accountability though not common in Tanzania, but this sounds too much.

    Please do something to show the public that you care for them.

    ReplyDelete
  17. yani wanajeshi wa tanzania ni wazembe kwanini hawachukuwi uangalifu maana ni mara ya pili yani kila siku nasoma blong hii lakini wala sicomment lakini leo nimepatwa na hasira lohhh mnatuvunja nguvu kurudi nyumbani poleni waliopatwa na maafa halafu sidhani hata kama serekali itajali kulipa fidia

    ReplyDelete
  18. NI VEMA RAIS AU PM WAKATOA TAMKO KWA WALALA HOI WENZANGU! IWEJE KILA SIKU MALOFA NDO WANAKUMBWA NA MABALAA?? MBONA HAYATOKEI SEE VIEW AU MASAKI??

    ReplyDelete
  19. Poleni wahanga wote.
    Tukumbuke kuwa haya ni mabomu ya ki-China - tena pengine ya miaka kama ishirini na mitano iliyopita!!!!!!!

    ReplyDelete
  20. Hakika serikali isipowajibika kupitia wizara husika, sidhani kama watanzania tutawaelewa. Hivi kweli pasipo aibu mnatuambia ni ajali tu, kwa hiyo ni kama vile bomba la maji kupasuka walio karibu hulowa na maji! Tuna tofauti gani na nchi zilizopo katika vita kwa sasa? kero zimezidi kupita kiasi, umeme shida, maji ni kitendawili na sasa mfululizo wa maafa ya mabomu, tuwaeleweje serikali iliyopo madarakani? Wahenga walisema ukila na kipofu usimshike mkono, sasa wamnyang'anya
    tonge mkononi?!!............madhara yake yaja hima.

    ReplyDelete
  21. Kwa kweli inasikitisha sana

    ReplyDelete
  22. Hii ni maafa ya kitaifa. Je, serikali itatoa tamko rasmi kuhusu tukio?
    Na ni kweli makambi ya jeshi yanatakiwa kuwa mbali na wananchi kuepeusha maafa ya kama hayo.

    Mungu alaze roho za waliopoteza maisha yao mahala pema mbinguni. AMEN.

    ReplyDelete
  23. Mohamed BilalFebruary 17, 2011

    we are very sory for the ones who are directly or inderectly affected by the tragedy..!! i think ministirial responsibility must take place now.. we expected that, after the mbagala bombing, then army would have taken steps forward to ensure they counter check the rest of the camps counetry wise.. but the recent bombing is evident that they didnt do so..!! we expect the resignation of the minister responsible..!!!

    poleni sana watanzania wenzangu..!!

    ReplyDelete
  24. MIMI MAFIKIRI KWA HILI SERIKARI HAINA CHA KUTUAMBIA INATAKIWA KUOMBA RADHI KWA WANANCHI NA KUWALIPA FIDIA ZA UKWELI SIYO MTU ANAKUFA AU ANAVUNJIKA MGUU ANALIPWA SHILINGI LAKI MBILI .INGEKUWA WALE WA MBAGALA WAMELIPWA IPASAVYO NADHANI SERIKALI ISINGEFANYA UZEMBE. HUU NI UZEMBE TU WALA SI KITU KINGINE NA WASISEME AJALI WASEME SERIKALI NI WAZEMBE NA WAWAOMBE WANANCHI MSAMAHA.

    NILIDHANI SERIKALI IMEJIFUNZA YALE YALIYOTOKEA MBAGALA.SERIKALI NI WAZURI KATIKA KUJITETEA LAKINI MUNGU ATAWASIMAMIA HAO WALIOPATA MATATIZO.
    NI VIZURI KUEPUSHA AJALI NA SIYO KUSUBILI YATOKEE NA WATU WAANZE KUUNGUA NA JUA NNA KUTOKWA NA JASHO KUFUATILIA VIJIHELA.

    ReplyDelete
  25. Like father, like Son. Dr Mwinyi tafadhali chukua hatua kama mzee mwinyi alizochukua alipokuwa waziri wa Mambo ya ndani.

    ReplyDelete
  26. inasikitisha sana,yaliyotokea mbagala haikua fundisho,na pia hata yaliyotokea mbagala ilikua ni uzembe,sasa kwa haya gongolamboto sijui hata tuseme nini,maana ni zaidi ya uzembe, kutojali maisha ya watu, kupuuzia kila kitu,ubinafsi, kutokuwajibika, kutokuipenda nchi na pia kutojali wananchi.maafa ni makubwa sana ingawa si rahisi kusema ukweli.wakipoteza maisha watu 200 tunaambiwa 2o.uongo kila sehemu,kweli Tanzania imeoza!tukizamia ughaibuni tunaomba msitulaumu,mambo kama haya yanachangi sana.
    mariam USA

    ReplyDelete
  27. Mwanzo kambi za jeshi zilikuwa mbali na uraiani. Lakini kila idadi ya watu mijini ikiongezeka, wananchi wanajenga karibu na kambi. Cha msingi ni kuwa jeshi la Tanzania halina tabia ya kuangalia usalama wa silaha kila kipindi fulani. Wakati umefika kufuata viwango vya kimataifa katika kila sekta nchini.

    ReplyDelete
  28. WANAJESHI WAMEKOSA UZALENDO JUU YA NCHI YAO NA WATANZANIA WENZAO.
    HIVI HII IMEKUSUDIWA AU NI BAHATI MBAYA? NI MARA YA PILI SASA WANANCHI WASIO NA HATIA WANAPOTEZA MAISHA. SERIKALI ITUJALI JAMANIIII!!!! TUTAISHI KWA WASIWASI KAMA TUPO DAFU MPAKA LINI?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...