
Na Ally Kondo, London
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe (pichani) ameainisha baadhi ya changamoto anbazo Serikali inakabiliana nazo tangu ilivyoanza mchakato wa kuwahamasisha Watanzania wanaoishi ughaibuni (Diaspora) kushiriki katika kuchangia maendeleo ya nchi yao.
Je wapigabox waliruhusiwa kuhudhuria na walifika?
ReplyDeleteMmoja ya Kitu cha msingi kwetu wa-TZ tunaishi nje ya nchi ni DUAL CITIZENSHIP. Wenzetu Kenya na Uganda wameisha pitisha.GOD BLESS TZ.
ReplyDeleteHASHIM SWDEN?
ReplyDeleteNASHUKURU KUPATA TAARIFA HII KWENYE MTANDAO WA BWANA MICHUZI, LAKINI HOJA NI KWAMBA JEE WATANZANIA WANAOHITAJIKA KATA KUCHANGIA MAENDELEO YA TANZANIA NI WALE WANAOISHI UK PEKEE AU NI WOTE WANAOISHI UGHAIBUNI? SSA SSIS WENGINE MBONA HATUKUALIKWA NA HALI TUMEJIANDIKISHA KWENYE BALOZI ZETU? BAADA YA KUSOMA HABARI HII NILIWASILIANA NA WADAU WENGINE NIKAWADOEZA HABARI HII, TUMESIKITISHWA SAAAAANA NA HALI YA KUTOOPEWA FURSA YA KUHUDHURIA MKUTANO HUUUUU. AKINA DIASPORA TUKO WENGI SANA HAPA EUROPE. NINGEOMBA WADAU WAANDAE UTARATIBU WA KUPEANA HABARI MAPEMA ILI TUWEZE KUHUDHURIA KWA WINGI NA UMOJA PIA MSHIKAMANO. MAANA MADA HII INATUHUSU WOTE,
AHSANTE.
Mdau uliyesema kwamba hukualikwa, sidhani kama unamaanisha ulitaka utumiwe barua binafsi ya mwaliko. Habari za kuhusu mkutano huu wa Diaspora zilikuwepo katika blog hii ya jamii kwa siku nyingi tuu kabla ya mkutano wenyewe.
ReplyDeleteKuhusu UK, ni kwamba wote tunaelewa historia ya nchi yetu na UK. Ingawa siyo historia nzuri, lakini bado ni historia. Historia hii ndiyo inayofanya UK iwe na watanzania wengi kuliko nchi zingine za Ulaya, na hivyo basi, "by default", UK imekuwa ndiyo kitovu cha watanzania walowezi wa Ulaya. Ingawa hii haina maana kwamba watanzania wa UK ni muhimu kuliko watanzania wa nchi zingine za ulaya.
MPEVU asante sana kaka UMESOMEKA fullstop.
ReplyDeleteKwa mara ya kwanza nimehudhuria London Diaspora 3, nimefurahishwa na conference nzima kwani ni moja ya chombo muhimu sana ambucho watu wanachangia hoja kwa uwelewa wa juu sana kwani haiangalii uchama bali ni kwa maendeleo ya nchi.
ReplyDeleteBinafsi ninashauri Serikali iangalie umuhimu wa kuunda Diaspora kama chombo kisichounga upande wowote wa kichama, na iwatumie wana Diaspora kuwa ni source for economic policies. Inasikitisha report iliyotolewa na mtu wa BOT is very biased haizingatii International Macroeconomic na hii ni kwa sababu BOT is not an independent institution! therefore every report must support country political situation. My suggestion is that we must have a further vision for Diaspora Unit and might have a big impact to our economy only if it wont be associated with any side politically.
Mmesikia BBC Swahili kuna nchi za kina burundi zinataka kugoma kupitisha mizigo pale dar kwa ajili ya utapeli?habari inakuja mkuu akizidi kuwahamasisha diaspora.kwa kweli ieleweke bandari na TRA ni sehemu nyeti kwa nchi hasa inapotuhitaji sisi diaspora.Tuige Rwanda jamani wenye dhamana wawe responsible.Kagame hamtazami mkwamisha maendeleo usoni mara mbili Bongo vipi tunatawaliwa na ujanja ujanja tu?binafsi mwaka jana nilipitia Rwanda maendeleo unayaona nje si kwenye mitandao.Tuweni wakali na wakwamisha maendeleo ya nchi yetu tumsupport Raisi wetu yuko seriouse ila aige kuwajibisha bila kutazama usoni otherwise tutakaa diaspora miaka dahari tunapigia ngoma majini
ReplyDeleteMimi sikuweza kuhudhuria Diaspora kwa sababu nilikuwa na udhuru kidogo. Ila napenda kutoa maoni yangu kidogo kwenye hili swala la Dispora na maendeleo ya Tanzania. Kwanza ningependa kuishauri Serikali chini ya muheshimiwa Rasi Kikwete kwamba huu sio wakati wa siasa na maneno yasioyokuwa na utekelezaji. Nakumbuka (kama kumbukumbu zangu zipo vizuri) rais alishawahi kusema wakati akiwa US miaka ya nyuma kwamba "watanzania walioko nje wanaonea wivu watanzania wa bong ndo maana wanataka uraia wa nchi mbili". Samahani kama nitakuwa nimenukuu vibaya ila tafsiri yake ndo hiyo. Sasa kama Tanzania kweli ipo serious kwa maendeleo yake ni bora ikaruhusu hili swala la uraia wa nchi mbili. Wenzetu Kenya wameshalipitisha hili na katika hii East African Community wao watakuwa wanabenefit zaidi kwa sababu wanayo access kwenye market ya Tanzania and at the same time Wakenya waliopo nje ya nje wanauhuru wa kufanya investment nchini kwao. Jamani viongozi wetu wa Tanzania, tusidharau wananchi walipo nje. Huku nje ya nchi (mfano UK nilipo mimi) hata mfanyakazi wa ndani anapata hela inayomwezesha walau kujenga kajumba ka kawaida bongo na kupangishia na serikali kupata mapato kupitia property tax. Naishauri serikali iharikishe mchakato wa kuwaruhusu watanzania kuwa na uraia wa nchi mbili au zaidi ili kupata mapato ya wanzania walio nje ya nchi. Kwa sasa inaonekana kama watanzania walio nje ya nchi wana tamaa lakini tuangalie mbeleni hili swala ni kwa ajili ya maendeleo ya Tanzania na Watanzania kwa ujumla wake. Tuambiane ukweli ni kwamba mwisho wa siku kama mimi naishi nje ya nchi na serikali hairuhusu uraia wa nchi mbili ili kuniwezesha kufanya investment popote Tanzania ninapotaka mwisho wa siku nitakuwa naifikiria familia yangu tu na ndugu zangu waliopo Tanzania. Lakini tukiangalia kwa mapana watanzania tuliopo nje tunaweza kufnaya investments kwa udogo wake ambazo zitaweza kutoa ajira kwa watanzania wenzetu. WAKUU WA SERIKALI EMBU LIANGALIENZI HIL KWA UPESI JAMANI...Hata kama Serikali itaendelea kuuzuia uraia wa nchi mbili, ukweli ni kwamba Tanzania haina Ajira za kutosha kuwashawishi watanzania waliopo nje kurudi. Alternative itakuwa kwa hao watanzania waliopo nje kujilipua(kuukana uraia wa Tanzania) na kuchukua uraia wa nchi walizopo. Hivyo basi serikali itafakari hili swala na kulifanyia maamuzi kwa haraka. Poleni kwa kuwachosha kusoma ila ni mtazamo wangu tu kwa maendeleo ya Tanzania.
ReplyDelete