
Niliangalia vitabu vya ki-Swahili, ambavyo ni vingi katika maktaba hii, nikavutiwa na vitabu vya Someni Kwa Furaha, tulivyosoma tulipokuwa shule ya msingi.
Nilijikumbusha kuhusu Bulicheka na mke wake Lizabeta, Wagagagigikoko na mfalme wao, Makari Hodari, Kalumekenge, na Pauli mwenye mikono michafu.
Tulibahatika, enzi za utoto wetu, kuwa na vitabu vya kusisimua, vilivyotupa motisha ya kusoma. Vitabu hivi viliandikwa kuzingatia umri wetu. Walimu walikuwa makini, katika kufundisha, kwa mbinu mbali mbali, kama vile nyimbo. Tuliimba alfabeti hadi orodha. Nawasifu na kuwashukuru waalimu wale.
Mtembelee Profesa Mbele BOFYA HAPA
Yaani Prof.umenigusa kweli..ni majuzi tu nilikuwa najaribu ku-recall maisha ya utoto wangu nikawa nakumbuka zile nyimbo za "Pauli/o usije kucheza na mimi..uuna mikoono michaaafu..!Sijui heee YAKOOBOO..heee YAAKOBOO amka twende shule..amka twende shule...haaya njoo,haaya njoo.!!!Elimu ya siku hizi"siyo".
ReplyDeleteDavid V
Thanks Prof kwa kuturudishia miaka yetu nyuma kwa miaka arubaini na ushei.
ReplyDeleteTumbo niache nimwachie Manenge uji....
ReplyDeletewadau kilikua kitabu gani hicho....