Ankal akimtambulisha mwasisi wa Bongo Fleva nchini Saleh Jabir (kati) kwa msanii Ferouz wa Daz Nundaz jijini Dar leo. Saleh, anayeishi Uingereza, yuko nyumbani kwa vekesheni ya mwezi mmoja ya mfungo wa Ramadhani. yeye ndiye msanii wa kwanza wa kizazi kipya aliyeimba Hip Hop kwa Kiswahili na wimbo wake wa Ice Ice baby uliompa ushindi katika mashindano ya Yo Rap Bonanza yaliyoandaliwa na Kim & The Boyz , kabla ya vikundi vingine kama Kwanza Unit, Diplomatz na vinginevyo kufuatia.
 Mpiga picha wa Daily News na Habari Leo Fadhili Akida akila pozi na Saleh Jabir (kulia) na Ferouz wa Daz Nundaz

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 11 mpaka sasa

  1. Mkuu wa Rap Cartoon Naruka kama Ninja na Paa kama ndege dah zamani kweli.

    ReplyDelete
  2. Je hakutoa album hata moja huko jikoni ukerewe?

    ReplyDelete
  3. opipiiiii yeyunoliiii....ice ice bebiiiiiii, dah niko form two wakati huo dah!

    ReplyDelete
  4. Saleh Jabri,umenikumbusha mbali sana, enzi hizo za ...

    Kitu kimenikaa moyoni, sasa naamua kukitoa mdomoni
    Yooh, I do know, kusema mengine, naona choo
    To the stream nataka mike ya umeme, niko kwenye stage nayakata madebe

    Ngoma hii ya ajabu inawafanya watu wawe kama deadly,
    inapodunda redioni, tega sikio sikiliza kwa makini
    Ipende usiipende take your way, na mimi ninadunda kama kid & play
    Kama hunipendi yoo kaa pembe sitopenda wengi kama Maumba

    Ice Ice baby ..... too cold, too cold

    ReplyDelete
  5. Huyu akiwa mwasisi wa bongo fleva lile kundi la KWANZA UNIT chini yake marehebu Adili Kumbuka (Nigger One) na Marehemu Robert Mwingira (D-Rob) bila kuwasahau akina Ramson (Rhyme-Son) utawaweka wapi? KUMBUKUMBU YANGU INANIAMBIA KWAMBA, ADILI KUMBUKA NDIO MWANZILISHI NA KUNDI ZIMA LA KWANZA UNIT.

    ReplyDelete
  6. Album ya Saleh Jabil ilitwa Swahili Rap(1991). Na Kundi la Kwanza Unit lilianza 1993. Nakubaliana ni mwanzilishi wa bongo flava. Alipata umaarufu kwa sababu alikuwa anaimba kwa kutumia kiswahili.

    ReplyDelete
  7. Saleh Jabirni mwasisi wa Bongoflava kwa mantikiya kwamba ndiye alikuwa wa kwanza kurekodi kikamilifu wimbo mzima kwa kutumia Kiswahili.
    Enzi zile, wasanii karibu wote walikuwa wanarap kwa Kiingereza.
    Nakumbuka fika tamasha ambalo Saleh alirap kwamara ya kwanza na kushinda pale New Africa ghorofa la saba.Wasanii wengine waliduwaa, watu waliokuwepo walishangaa na baadaye kushangilia sana!
    Kwa kweli ilikuwa ni mapinduzi makubwa!
    Marehemu Adili alikuwa mkali nakubali, lakini kwa kweli, Saleh anastahili Taji maalumu la kukuza Kiswahili na kubadilisha kabisa mwelekeo wa rap Tanzania daima!
    Taji

    ReplyDelete
  8. AnonymousJuly 26, 2013

    sasa hizo nyimbo zako king fanya utaratibu uziingize kwenye mtandao kama vipi watu turuke majoka .

    ReplyDelete
  9. Namkubali sana huyo jamaa.Kuthibitisha kuwa namuenzi ni kuwa hadi leo hii tape ya album ya Swahili rap ninayo.N
    naitunza kama vyeti vya taaluma.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Mkuu ninashida na hiyo albamu. Ninafanya utafiti kidogo. Tafadhali naomba tuwasiliane kupitia barua pepe - kidojasper@gmail.com

      Delete
  10. Ntazipataje hizo nyimbo zake?mwenye nazo aniuzie kwa gharama yoyote ile

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...