Katibu tawala wa mkoa wa Mtwara,Yusuf Matumbo akizungumza na wajumbe wa jumuiya ya serikali za mitaa(Alat)mkoa wa Ruvumna wakati wa ziara ya wajumbe hao kutembelea mkoani humo kujifunza namna ya kilimo cha korosho na mazao mengine ya biashara.
Mtafiti wa zao la korosho kutoka kituo cha kilimo Naliendele mkoani Mtwara,Ramadhan Bashiru (kulia) akiwaonesha mche wa korosho baadhi ya wajumbe wa jumuiya ya serikali za mitaa(Alat)wa mkoa wa Ruvuma walipotembelea katika kituo hicho kujifunza kilimo cha kilimo bora cha korosho hivi karibuni.
Wajumbe wa jumuiya ya serikali za mitaa(Alat)mkoa wa Ruvuma wakimsikilimza mtaalamu wa kilimo cha korosho kutoka kituo cha kilimo cha Naliendele mkoani Mtwara,Bi Joan Kasuga (kushoto) juu ya kilimo bora cha korosho,kufuatia ziara ya wajumbe hao kutembelea kituo hicho kwa lemngo la kujifunza kilimo bora cha zao hilo.
Mtafiti wa zao la muhogo kutoka kituo cha kilimo cha Naliendele mkoani Mtwara Abdala Nyapuka (kulia) akiwaonesha wajumbe wa Alat mkoa wa Ruvuma aina moja wapo ya muhogo unaozalishwa katika kituo hicho.kufuatia ziara ya mafunzo ya wajumbe hao mkoani Mtwara kujifunza namna ya kilimo bora cha korosho na mazao mengine ya biashara.
Katibu wa jumuiya za serikali za mitaa(Alat)mkoa wa Ruvuma Musa Zungiza akiazungumza na wajumbe wa jumuiya hiyo juzi katika u8kumbiu wa halmashauri ya wilaya Tunduru mkoani humo,kushoto ni mwenyekiti wa jumuiya hiyo Oddo Mwisho.
Mwenyekiti wa jumuiya ya serikali za mitaa(Alat) mkoa wa Ruvuma Oddo Mwisho akiangali chupa yenye wadudu waharibifu wa korosho katika kituo cha kilimo cha Naliendele mkoani Mtwara,alipoongoza ujumbe wa wajumbe hao kutembelea mkoani Mtwara hivi karibuni.Picha na Muhidin Amri wa Globu ya Jamii,Ruvuma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...