Malkia
wa mipasho nchini, Khadija Kopa, kutoka T.O.T akiwapagawisha mashabiki
waliohudhuria Mitikisiko ya Pwani Dar Live Jumamosi.
MALKIA
wa mipasho nchini, Khadija Kopa, juzi (Jumamosi) alifunika vilivyo
katika Tamasha la Mitikisiko ya Pwani lililofanyika ndani ya ukumbi wa
kisasa wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar.
Tamasha hilo lilipambwa na makundi mbalimbali ya taarab yakiwemo Jahazi,
Coastal, TOT na mengineyo. Watangazaji mahiri kutoka Times Radio
wakiongozwa na Gardner G Habash na Khadija Shaibu 'Dida' walinogesha
tamasha hilo na kulifanya liwe la kipekee.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...