Na Father Kidevu Blog, 

KAMATI ya Miss Tanzania imesema kuwa Mrembo Maggie Munthali hana pingamizi lolote katika kushiriki mashindano hayo kwa kutumia jina la Tanzania na badala yake  kufanya hivyo anatumia uzalendo wake kuitangaza nchi Kimataifa.

Ufafanuzi huo umekuja kufuatia malamiko yaliyotolewa na baadhi ya wadau wa Urembo hasa Watanzania waishio katika jiji la Washingtoni DC, Marekani juu ya Uhalali wa Mrembo Maggie Munthali kuvaa beji ya Miss Tanzania katika mashindano ya kumsaka Miss Afrika USA 2012.

Akizungumza na Blogu hii Msemaji wa Kamati ya Miss Tanzania Hidan Ricco amesema kuwa Kamati ya Miss Tanzania haina kipingamizi chochote kwa mrembo huyo kushiriki mashindano hayo, kwani shindano hilo linawahusu warembo waishio huko lakini wanatoka Tanzania.

Awali akitoa historia ya Mrembo huyo, Rico alisema kuwa Kamati inamfahamu vyema mrembo Maggie Munthali kwani aliwahi kushiriki mashindano hayo ngazi ya Vitongoji na kuishia ngazi ya kanda.

Tumesoma maoni yenu kupitia mitandao ya kijamii Blogs inaohusu taarifa ya mrembo Maggie Munthali kushiriki shindano la urembo la Miss Africa USA.

“Mrembo Maggie Munthali alishiriki mashindano ya urembo ya Miss Tanzania Kitongoji cha MZIZIMA mwaka 2005.” Alisema Ricco.

Pia aliendelea kwa kusema kuwa Mrembo Maggie alikuwa miongoni wa waliofanikiwa kuingia TOP 3 ya shindano hilo hivyo kupata nafasi ya kuwakilisha kitongoji hicho katika ngazi ya KANDA YA ILALA  kwa mwaka huo.

Mrembo huyo hakupata nafasi  ya kuingia katika Fainali za Taifa kwa mwaka huo 2005. aliishia ngazi ya Kanda ya Ilala.

Kanda ya Ilala kwa mwaka huo iliwakilishwa na FEZA KESSY, Perminda Raj na LILIAN MUSHI, na mshindi wa mwaka huo alikuwa NANCY SUMARI ambaye pia alitwaa taji la MISS WORLD AFRICA 2005.

Ricco amesema Kamati ya Miss Tanzania haijui ni vigezo vipi vinatumika katika shindano hilo, na maamuzi yakumpa jina Miss Tanzania na Kamati inaamini kuwa ni mrembo anayewakilisha Tanzania  japokuwa hakuingia  katika Fainali za Taifa.

Kamati inamtakia kila la heri mrembo huyo na wengine watakaojitokeza kutangaza jina la Tanzania katika fani ya urembo.
 
Father Kidevu Blog ilifanikiwa kufanya utafiti juu ya washiriki wa shindano hilo na kubaini kuwa sio Mamiss halisi wa nchi walizotoka kwani baadhi ya nchi walikuwa zaidi ya mmoja kama vile Kenya. 
Pia baadhi yao Umri unaonesha dhahiri kuwa umekwenda sana kwani washiriki wanapoaswa kuana miaka kuanzia 18 lakini isizidi 29 na hawaendani na vigezo halali vya mashindano ya Urembo yanayofanyika kila mwaka katika nchi husika kwaajili ya kushiriki Miss World.
  
Haya ni baadhi ya Masharti na Vigezo vya Mshiriki ambayo yapo katika mtandao huu   http://www.missafricaunitedstates.com/application/registration/


ELIGIBILITY

1.Applicant must have at least one parent from an African country.
2. An applicant with parents from two countries will choose to represent only one country of her choice.
3. Applicants must be at least 18 years old on or before the date of the pageant she wishes to compete in.
4.Applicants above 29 years of age will not be accepted
5.We accept Applications from students, professionals and girls wishing to develop themselves and improve their status.
6. Applicants are strongly encouraged to have a humanitarian platform and realistic project to uplift the community in need.
7. No Pageant Experience is required.
8. Applicants must be female at birth and never married.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. go Maggie..

    ReplyDelete


  2. SASA YULE "MDAU WA WASHINGTON" ALIKUWA ANAKURUPUKA KUTOKA USINGIZINI AU NDIO WALE WA RUSHWA ZA NGONO?

    MAANA KAPOST BILA KUFANYA KAUCHUNGUDHI ONA SASA KARUKA STIM

    ReplyDelete
  3. safi sana,yule bin adamu alikua anasambaza fitina akafie mbele

    ReplyDelete
  4. APPLICANT MUST NEVER MARRIED??

    ReplyDelete
  5. Mdau mtoa mada naomba urekebishe kuwa ni mtu mmoja tu aliyeuliza uhala wa huyo dada kishiriki. Tatizo limeonekana kuwa ni ukosefu wa elimu. Wasomi wengi wanaelewa kuwa kabla hujaandika, lazima ufanye research na kuelewa nini unakiandika.Nafikiri tumsamehe mtanzania mwenzetu na tumshauri aende shule. Natumaini ataupokea ushauri huu with positive attitude.

    ReplyDelete
  6. Alafu kapost hajui sheria na tarartibu za shindano. Maggie kakiuka nini pale? Au wivu?

    ReplyDelete


  7. hivi hata sisi watanzania tuliopo ughaibuni tunakua na wivu wa ajabu hvyo?? this is insane yaani wewe bala ya kumpigia kura ashinde unaleta umasikini wako humu ndani?? au ulitaka kwenda wewe??

    kweli wanao check eligibility ya nchi kua 3rd world walikosea Tanzania ilitakiwa kua 4th world country kabisaa coz naona hakili haziko sawa kabisaa am totally dissaopited with the person siamini kama anaishi huku huyo?

    Bado unamawazo ya 5th world wewe hata sio 4th world pumbavu kabisaa this is bad totally bad

    Go Magie tena nakuombea ushinde kabisaa

    ReplyDelete
  8. Duh!Nimesoma maelezo ya pande mbili kwa umakini sana,nimeelewa sasa.Yule wa post ya kwanza siyo kwamba anampinga huyu dada kuwakilisha Tanzania.Yeye,anapinga kujiita `Miss` Tanzania(Matumizi ya neno Miss-kama nilimwelewa vizuri).Kwenye huo mkanda angeweza kuandika tu TANZANIA (kwa maana kwamba ni mshiriki kutoka Tanzania).BTW,alishinda hilo shindano?

    David V

    ReplyDelete
  9. Ivi jamani Hebu muacheni hiyo binti apumue mbona mnamuandama hivyo.....ivi hao mnaowaita mamiss Tanzania mbona wana mambo makubwa wanafanya Julio hiyo binti.. Washirikina wengine wanatembea na dawa za kuweka midomoni ili wakiongea wakubalike au Sababu hatuwasemi...na kutwa mnawasifia..hivi lini mating a nacho nyingine za Africa Kuwa supportive yaani wengi ni wivu na inajionyesha wazi...she is beautiful,hard work na anajaribu kuwakilisha nchi please muacheni Je akishinda mtafanyaje?!tuweni na upends na tusche majungu ili tulete maendeleo nchini..mnataka nyinyi tu kwanini. Muacheni ni mtu kwenye upends,mtulivu....waandikeni hao watoto wenu kila kukicha kurudi nchini kurenew macaws...mkitiuzi tutawataja mamiss wenu washirikina

    ReplyDelete
  10. David V i'm with you! hoja ya majibu imeshindwa kueleza kama ni sawa kwa miss anayeshindana kuvaa mkanda wa/ulioandikwa MISS TANZANIA hata kabla ya kuwahi/kushinda taji hilo.

    ReplyDelete

  11. KAKA DAVID V, HIVI UNAELEWA MAANA YA MISS? BILA SHAKA UNAELEWA.
    HIYO NDIYO TITLE YAKE KAKA. ADULT WOMAN, NOT MARRIED.

    TITLE HAITUMIKI KWENYE MASHINDANO YA UMISI TUU, THE TITLE IS USED EVERYWHERE.

    KAZINI, HOSPITAL, CHUONI, KUJAZA FORM...THE LIST GOES ON!!! IT IS JUST A TITLE, SIO TITLE YA KWENYE BEAUTY PAGEANTS TU! YAANA HUJUI?

    KAZI IPO.

    ReplyDelete

  12. Anon wa TUE DEC 4th 01:54:00AM

    Marekani mwanaume ndio anaolewa, mwanamke ndio anayeoa. Bila shaka hiyo eligibility imetokea Marekani.

    In US the woman marries a man. Kama umeshawahi kusikia mwanaume asking a woman, "will you marry me"?

    "APPLICANT MUST NEVER MARRIED" yaani,

    LAZIMA AWE HAJAWAHI KUOA.

    ReplyDelete
  13. Huyo aliyelalamika ktk post ya mwanzo atakuwa ANABEBA MABOSKI tu. Anajua kula mikate na ugali tu ili apate nguvu ya kubeba MABOKSI. LAkini kichwani ni MTUPI.

    ReplyDelete
  14. Swali la kizushi: Je, na hao wengine waliondika MISS (ikifuatiwa na jina la nchi), walishinda taji la UMISS katika nchi zao? Mdau unataka aweke kitambaa kilichoandikwa Tanzania; duu! kwani huyo dada ndiyo nchi ya Tanzania. Well done Miss Tanzania for representing us. Nyie wengine mwendelee KUBEBA MABOKSI mpaka MABEGA yaende upande

    ReplyDelete
  15. Ohhh Maggie Munthali hastahili!

    Watanzania Majuu wenyewe kwa wenyewe mnabaniana sasa je kweli mtaweza kuijenga Tanzania?

    ReplyDelete
  16. DAVID V, DAVID V, DAVID V, Wacha hizo. Labda ujasoma vizuri, soma tena(rudi nyuma usome maoni ya posti ya awali, maana hii ya pili). Nilishasema nyie ndiyo mnachochea ugomvi kati ya WaTanzania wa Ughaibuni na nyumbani. Nilishasema unachuki binafsi. Angalia unavyodanganya, umesoma maoni pande mbili zipi? Hapa maoni ni pande moja tu, asilimia 98 yanasema jamaa amekosea(hata hizo Miss kamati zote 2 zimejibu) na bila hata hivyo unaona kabisa jamaa ameongea madudu. Labda ni wewe ulieandika, ulikuwa unapima? Umeona sasa, usirudie kuandika madudu. Siye wote ni ndugu. Na jamaa walioko Ughaibuni wana uchungu sana na Taifa lao. Wapo wengi wanafanya mambo mengi kusaidia ndugu na Taifa, lakini hatujitangazi tu kwani siyo tabia yetu sisi wabongo.

    ReplyDelete
  17. JAMANI KUWA MISS TANZANIA C O MPAKA USHIRIKI UKIWA TZ KAVAA TAJI HILO KUWAKILISHA VYEMA UTAMBOLISHO WAKE HAWAKUTAKA JINA KWANI NI MISS AFRIKA USA SO KINACHOTAKIWA NI JINA LA NCHI KWA HIYO WEWE MVUTA MADUDE TULIZA WENGE KWA MAMBO YA MAENDELEO YA WENZIO WANAOJUA KWANINI WAKO HAPO DC mdau stockholm sweden

    ReplyDelete
  18. Anon wa Tue Dec 04, 01:54:00 AM 2012
    na
    Anon wa TUE DEC 4th 01:54:00AM

    Kweli lugha gongana. Na kama ni ujanja (kejeli)wa kujifanya mnajua zaidi, naona mmepotea na hapa mnaonyesha aibu jinsi msivyoelewa lugha, lakni mnajiona Poa. Mungu awasadie mpate hekima ya kuelewa. Na kama kweli hamuelewi lugha, samahani, basi ulizia kwa watu wanaojua.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...