Mkuu wa mkoa Rukwa Eng. Stalla Manyanya (kushoto) akimfariji msanii na taarab na malkia wa mipasho Tanzania,Khadija omar Kopa alipokua kwenye chumba maalum cha kupumzikia wageni kwenye uwanja wa ndege wa Mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leoa alfajiri kutokana na ugonjwa, Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani kitaifa yaliyoaadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana.
Baadhi ya viongozi na wananchi wa mkoa wa Rukwa na Mpanda wakimsindikiza kuapanda ndege msanii wa taarab na malkia wa mipasho Tanzania Khadija Omar kopa kwenye uwanja wa ndege wa mpanda baada ya kupewa taarifa ya kufiwa na mumewe Jafari Ali Yussuf aliyefariki Dunia leo alfajiri kutokana na ugonjwa, Bi Khadija Kopa alikua akitokea kwenye Maadhimnisho ya siku ya Mazingira Duniani kitaifa yaliyoadhimishwa Namanyere Mkoani Rukwa jana.
(Picha na ofisi ya Makamu wa Rais)
jamani...pole mamii
ReplyDeleteInnalillah wainna ilayhi rajiuun! Jamani huyo si ni kizuka tena, mbona yu waziiii?
ReplyDeleteHIVI HAO WABABA PEMBENI WANA AKILI KWELI? KWANINI HAWAWASAIDI WAMAMA KUMSHIKA KHADIJA HUONI WAMAMA WANATESEKA
ReplyDelete"Kullu nafsi dhaaikatul mawt" kila nafsi itaonja mauti. INNALILLAHI WAINNA ILAYHI RAJIUN.
ReplyDeleteWanamama wanamsaidia mwenzao,halafu lijamaa lenye kaunda suti linakenua, wajameni, ustaarabu upo wapi?
ReplyDeleteSipendi watu wanaocheka cheka ovyo misibani!
ReplyDeleteMdau wa 5 huyo anayekenua ukiona hivyo atakuwa ni Mtani wake Bibie Mfiwa Khadija Kopa.
ReplyDeleteSio rahisi mtu wa kawaida mwenye akili kukenua ktk tukio kama hilo.
Si unaona Khadija ni wa Pwani inawekena kwa kuwepo huko Rukwa jamaa Mtani anayecheka ni wa Bara analeta Utani Msibani!
Anayekenua huyo mwenye suti ktk tukio hilo la taarifa ya Msiba huenda ana ugonjwa wa kucheka!
ReplyDeleteHuyo anyecheka uko nyuma ana ubinadamu kweli?ana roho ya nyoka huyo suti kama anaenda kuiba ming'oko vile
ReplyDeleteDah! Yaani pole sana Dada Khadija. Nilisikitika sana niliposikia habari ya msiba wa mumeo. Yaani najua mlivyokuwa mnapenda. Mungu akutie nguvu dada. Mungu ailaze roho yake mahala pema mbinguni. Amen.
ReplyDeleteUNA MAJONZI WANGINE WANAFURAHIA MAJONZI YAKO.
ReplyDeleteHivi wadau mokoje? Mmemsikia jamaa akicheka? Kunonyesha meno au kufunua mdomo inawezekana anashangaa, analia, au labda kusikitika kwake ni kucheka. Remi Ongala aliimba "usione ninacheka, ukadhani ninayofuha moyoni...."! Msimlaumu baba sijui kaka wa watu. Kila mtu ana namna ya ku-react na certain circumstances! Na pengine hajui kinachoendelea! Yaani Wabongo ni lawama tu ndio maana hatufiki. Chukueni muda kutafakari
ReplyDeleteWakina baba Hawa wanatisha... Hata kutoa msaada kwa kina mama Hawa. Hiyo anaecheka hayawani tu.. Hata kama ni utani una muda wake, sio tu mara mfiwa anapotaarifiwa Msiba. Lakini pia, mpiga picha nae hovyo... Picha gani hiyo ku publish mtu yuko at the lowest point namna hiyo..
ReplyDeleteHawa waliomwambia nao hawakutumia akili si wangemwambia tu asitishe ziara yake mumewe mgonjwa sana na anahitajika mara moja Dar. Huko Rukwa sijui hata kama alipata usafiri wa ndege wa mara moja maana kendesha ni mpaka Dar ni siku nzima almost 18 hours? Sasa si kazi hiyo kwa mfiwa?
ReplyDeletePole sana msanii wetu
ReplyDeletePole Khadija Kopa. Jamaee hivi kufiwa afiwe mwingine ina maana life has to stop kwa wengine... je mnajuaje kama hata anajuana na kopa au ni msafiri yuko nazake??? Imetokea tuu bahati mbaya katokea kwenye picha anafurahia maisha yake na washikaji wake... dunia kila mtu na lake
ReplyDeleteHuyu anaecheka anadhani atamuowa Khadija!
ReplyDeletePole sana Hadija naona hata pole haitoshi msiba usikie tu kwa wengine usiombe
ReplyDeletehuyo anaecheka ana matatizo gani,tuwe tunajizuia jamani kwenye vitu kama hivi,mijitu mingine bwana
ReplyDeletePole sana Hadija. Ila mumeo alikuwa anaumwa amelazwa, vipi uliweza kumuacha kitandani na wewe kwenda Namanyere? Huoni kwamba amekosa faraja kutoka kwako katika muda wake wa mwisho wa maisha. Any way yote ni mipango ya Mungu.
ReplyDelete