MWANAMKE mkazi wa kijiji cha Ikandamoyo, wilayani Katavi, Veronica Saleh ‘Mama Kaela’ (50), amefanya uamuzi adimu wa kuolewa na wanaume wawili ambao anaishi nao kijijini hapo.

Kijiji hicho kipo umbali wa takribani kilometa 30 kutoka mjini hapa katika Jimbo la Katavi linalowakilishwa na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

Pamoja na ndoa hiyo iliyowezeshwa na mume mkubwa kukubali kuishi na mume mdogo, imeelezwa kuwa mwanamke huyo ndiye ‘aliyewaoa’ wanaume hao kwa zaidi ya miaka saba sasa, huku akiwa na amri kuu katika nyumba, kama ilivyo katika ndoa za kawaida.

Wanaume hao ni Paulo Sabuni ‘Baba Kaela’ (60) ambaye ndiye mume mkubwa na Arcado Mlele (45) ambaye ni mume mdogo.

Taarifa za kuwapo kwa ndoa hiyo ya aina yake, ziliifikia Globu ya Jamii na kufanyiwa uchunguzi kwa zaidi ya wiki tatu, na hatimaye katikati ya wiki hii, wahusika walikubali wao wenyewe kuzungumzia suala hilo. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanamke huyo ambaye alionekana kuwa msemaji wa familia hiyo, yeye na mumewe mkubwa, walifika kijijini hapo miaka 24 iliyopita, wakitoka kijiji cha Usumbwa mpakani mwa Chunya, Mbeya na Tabora.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 24, 2013

    Hiyo ni kinyume na maumbile, au?.....

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 24, 2013

    This comment has been removed by a blog administrator.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 24, 2013

    Inafurahisha na inachekesha kidogo. Lakini sababu twashangaa kuona mwanamke kuolewa na wanaume wawili ambapo hatuoni jambo mwanamme akioa wanawake wawili.Wadhungu wasema..what is sauce for the goose is sauce for the gander.
    Incidentally I would appreciate if someone gave me tasir fasah ya msemo huo
    Ibrahim

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 24, 2013

    Kuna haja kuwaomba wanaharakati kushinikiza mfumo huu uwe rasmi. Kama wanapigania usawa wa kijinsia basi kila jinsia iwe na uhuru wa kuoa!!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 24, 2013

    Ohooo!

    Haya tena Mtoto wa Mkulima Mzee PM unatueleza nini kuhusu watu wako hao kwenye Jimbo lako?

    Inafahamika ya kuwa sisi Watanzania ni jamii yenye kujinafasi sana hasa kwa mambo adimu kama hilo!, pana uwezekano mkubwa wakatokea Wanawake hapa Tanzania wakaupendelea utaratibu huo.

    Je ikitokea Watanzania wakapendekeza Kikatiba KTK MCHAKATO WA KATIBA YA TANZANIA utaratibu huo Mtoto wa Mkulima unasemaje kuhusu hilo pia liingizwe kwenye Katiba?

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 24, 2013

    Haya Baba Pinda kazi kwako unasemaje kwa hilo?

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 24, 2013

    Ahhh!

    Sio siri mambo haya wanaweza wanawake, inawezekana hao wanaume wanazichapa ngumi na kupigana vikumbo kwa siri, sio rahisi zamu ya mwenzio wewe ume umejikunyata pembeni.

    Hiyo kwa wanaume inawezekana?

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 24, 2013

    hilo ndio jembe, mipini miwili halali? mingapi mafichoni? ila watoto lazima watakuwa wanaumia kisaikolojia.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 24, 2013

    Wanaume wawili mwanamke mmoja?

    Wanaume wanaweza hata kucheza mchezo wa Drafti au Bao kwa pamoja 'Dam dam' wakiwa nyumbani huku wakisubiri chakula!

    Yote 9 la 10 ni pale chakula kimesha liwa...NA SASA NI ZAMU YA MWANAMUME MWENYE ZAMU YAKE SIKU HUYO KUJINAFASI!

    OHHH HUYO MWANAMUME ATAKYEKUWA AMEAMURIWA KULALA CHINI YA MKEKA NA ''MWANAMKE-MUME'' MWENYE AMRI HAPO NDANI NADHANI PATAMBIMBIKA.

    INAWEZEKANA HUYO MWENYE ZAMU ATAONGEZA MADOIDO HAPO KTK JUKWAA AKIJINAFASI HADI ALIYELALA CHINI KWENYE MKEKA NAYE AKAPANDISHA MORI NA KUKAIDI AMRI NAYE ILI 'APEWE' AKAPANDA JUU!!!

    ReplyDelete
  10. afadhali ana wawili wale machangudoa wana wangapi?

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 24, 2013

    INASIKITISHA SANA

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 24, 2013

    Hii ndoa ni halali? Ya kanisani (dhehebu gani)?, ya msikitini au ya Mwenyekiti wa Kijiji?

    ReplyDelete
  13. Hongera sana Mama. Wewe ni shujaa wa mashujaa KuVunja Ukimya. Atakaye lima kando mpe talaka yake asonge mbali. Mdebedo, awe kipagazi kulima mashamba alite chakula kwa familia. Dunia Mbadala inawezekana!

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 25, 2013

    Wadau eleweni kwamba hatujajua kiini kikubwa cha hayo makubaliano,inawezakana kuna busara za hali ya juu kupita hata hizo haki za binadamu zinazoongelewa;Mfano,kama mume wa kwanza amepatwa na tatizo la JONGOo KUTOWEZA KUPANDA MTUNGI na ahadi ya ndoa yao ilikuwa kwa raha na shida,Lakini sio shida ya kukosa ngono.mume wa kwanza anaweza kukubaliana na mke ampate mtu wa kumtimizia shida yake ya ngono lakini huyo mume wa pili awe na wajibu mkubwa wakuitunza familia,inawezekana mume wa pili akawa kama mtumwa lakini kwamakubaliano!!AU mama huyu ni the main bread winner, anaweza kuwaambia ni kusuka au kunyoa.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 25, 2013

    Hii ni busara, ni makubaliana ya watu. Kama anony mmoja alivyosema inawezakana mme wa kwanza jogoo hawiki. Na kama ni vinginevyo basi ni sawa na sisi tuwaowe, maana mmetuowa kwa karne nyingi muno. Asante Mheshimiwa Pinda kwa kibari hiki.

    ReplyDelete
  16. hongereni wanawake kumbe na nyie mnaweza.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...