Abiria wapatao 60 waliokuwa wanasafiri na basi la Turu linalofanya safari zake kati ya mkoa wa Singida na Haydom mkoani Manyara, walilazimishwa kuteremka toka ndani ya basi hilo na wananchi zaidi ya mia mbili ( 200 ) wa vijiji vitatu, ambao baadae walilichoma moto basi hilo.
Taarifa toka eneo la tukio zinasema wananchi hao  wa vijiji vya Singa, Idabagadu. na Nkungi. mkoani Singida, ambao baada ya kuhakikisha abiria wote wameshuka, walilichoma moto basi hilo ambalo limetekea sehemu kubwa.  
Sababu ya wananchi hao kuchukua uamuzi huo ni kutokana na basi hilo kumgonga mwanakijiji mmoja na kufa wiki tatu zilizopita

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Kwani lililoua ni basi au dereva aliyekuwa analiendesha? Elimu vijijini ni muhimu.

    ReplyDelete
  2. Sasa wao wanadhani wamemkomoa mmiliki na siyo kampuni ya bima.

    ReplyDelete
  3. Hawa wanakijiji sheria za nchi zipo na zifuatwe sio kujichukulia sheria mkononi hata kama mwenzao kagongwa na kufariki

    ReplyDelete
  4. Chiki hizi ni zaidi ya mtu kugongwa tu! ina maana miaka tele tangia vijiji hivyo viwepo hakuwahi kufa mtu kwa kugongwa? Je walichoma gari husika pia?
    Huu ni umaskini wa kupindukia, unaozalisha hasira kiasi hiki. Serikali ifanye kweli "Maisha bora kwa kila Mtanzania"

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...