Hatimaye bifu kali kati ya msanii aliyewahi kutwaa tuzo 5 nchini za KTMA na kuvunja rekodi TWENTY PERCENT (kushoto) na aliyewahi kuwa Producer wake na pia ni mshindi wa tuzo ya mtayarishaji bora wa muziki nchini KTMA  2012 MAN WATER (kulia) limemalizika rasimi leo kwa wawili hao kukutana nakumaliza tofauti zao.
Man Water na 20% walikutana leo katika studio za Magic fm na Channel Ten ambapo wawili hao wamekubaliana kufanya kazi tena pamoja na kusahau yaliyopita.
Akizungumzia kiundani kuhusu tofauti zao Man Water alisema tatizo lilikua ni kutoelewana au kupishana kidogo kwa kauli ambazo leo walizimaliza na hatimaye kuweka mikakati mipya ikiwemo ya kufanya kazi pamoja kwa makubaliano maalumu.
Kwa upande wake 20% amesema tofauti zao hazikuwa za msingi bali ni kupishana tu kwa kauli na sasa yuko tayari kufanya kazi pamoja na Man Water.
Inaaminika kwamba kufanya kazi pamoja kwa wawili hao kuna maana kubwa kutokana na kuwezana na kuelewana katika kazi zao mbalimbali walizowahi kufanya ikiwemo kazi ya Yanini malumbano,Tamaa mbaya,Mama Neema na nyinginezo.
Peace And Love

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Yap,huyu 20% kwa kweli nyumbo zake zina mengi yahusuyo jamii zetu.

    Basi tunawasubiri.

    ReplyDelete
  2. Saaaaaffffiiiii ssssaaaannnnaaaaa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...