Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bi. Sihaba Nkinga, akisisitiza jambo, leo Novemba 5, 2013, jijini Dar-es-salaam, alipokutana na ujumbe wa kampuni ya Symbion ya Marekani kujadili maandalizi ya ujenzi wa kituo kikubwa cha maendeleo ya mchezo wa soka nchini (Soccer Academy), ambayo itashirikiana na Club ya Sunderland ya Uingereza katika kuindesha Academy hiyo. Katika mpango huo, Kampuni ya Symbion pia itajenga viwanja vya michezo (sports courts) eneo la Kidongo Chekundu. Mazungumzo hayo yamehusisha pia ujumbe wa viongozi kutoka Idara ya Michezo (hawapo pichani)
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Symbion, Ndugu. Peter Gathercole akifafanua jambo, leo Novemba 5, 2013, jijini Dar-es-salaam, alipokutana na Uongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuelezea mikakati ya Maandalizi ya ujenzi wa Kituo cha Maendeleo ya mchezo wa soka nchini (Soccer Academy), pamoja na viwanja vya michezo (sports courts).
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Symbion, Ndugu. Peter Gathercole (kulia) akifafanua jambo, leo Novemba 5, 2013, jijini Dar-es-salaam, alipokutana na Uongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kuelezea mikakati ya Maandalizi ya ujenzi wa Kituo cha Maendeleo ya Mchezo wa soka nchini (Soccer Academy), pamoja na viwanja vya michezo (sports courts). Kulia kwake ni wajumbe alioongozana nao.
Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Ndugu. Leonard Thadeo (kushoto) akielezea jambo, leo Novemba 5, 2013, jijini Dar-es-salaam, wakati uongozi wa Wizara ulipokutana na Ujumbe wa Viongozi wa kampuni ya Symbion ya Marekani Kujadili Maandalizi ya Ujenzi wa Kituo Kikubwa cha Mchezo wa soka nchini (Soccer Academy), pamoja na viwanja vya michezo (sports courts). Kulia kwake ni Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo la Tanzania (BMT), Henry Lihaya na Afisa Michezo Mkuu, Charles Yasse Mattoke.
Viongozi wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakiwa katika mazungumzo na Ujumbe wa Viongozi wa Kampuni ya Symbion ya Marekani walipokutana, leo Novemba 5, 2013, jijini Dar-es-salaam kujadili maandalizi ya ujenzi wa Kituo cha Maendeleo ya Mchezo wa soka nchini (Soccer Academy), pamoja na viwanja vya michezo (sports courts). (Picha zote na Johary Kachwamba-MAELEZO)
|
Jamani mm naungana na nyie kuhusu huo mpango mzuri wa kimaendeleo,,lakini tujiulize je hiyo sehemu ni kubwa na inatosha ya kujenga hayo mambo mazuri? Mm naona tungelitanua jiji letu,tutoke nje ya jiji zaidi ili kupatikane eneo kubwa zaidi ya hapo,,naitwa mdudu kaka kuona,,nipo huku UINGEREZA
ReplyDeletePOLLUSION YOTE HIYO KATIKASTI YA JIJI HII INAONESHA NI JINSI GANI VIONGOZI WETU WASIVYO NA UPEO, KWANINI WASIENDELEZE KIJIJI CHA MICHEZO KILICHOTELEKEZWA KARIBU NA UWANJA WA TAIFA KILICHOPO BARABARA YA MANDELA? AMA KWELI SIKIO LA KUFA HALISIKII DAWA.
ReplyDelete