Na Abdulaziz Video,Masasi.

Barabara ya Ndanda kwenda Masasi eneo la Kijiji cha Mkalapa,limekuwa ni majanga matupu kama inavyoonekana katika picha hapo chini,kwani barabara hiyo imeharibika vibara kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha matika maeneo mbali mbali hapa nchini.

Abiria wanaofanya safari katika maeneo hayo,inapaswa wajiandae kwa kupoteza masaa kadhaa katika eneo hilo,kwani mambo hayajakaa sawa.

Hivyo wakala wa Barabara Mkoa wa Mtwara (TANROADS),wanapaswa kulishughulikia swala hili haraka iwezekanavyo ili kuwaepusha watumiaji wa barabara hiyo kuondokana na hadha hii inayowaathiri wasafiri waendao Newala,Masasi,Nachingwea,Nanyumbu na Tunduru.
Magari yakipishana kwa shida katika eneo hilo la Kijiji cha Mkalapa,Mkoani Mtwara kutokana na kuharibika kwa barabara hiyo.
Wakazi wa kijiji hicho pamoja na Abiria wanaosafiri kwenda Newala,Masasi,Nachingwea,Nanyumbu na Tunduru wakiwa wamesimama bila kujua cha kufanya wakati magari yakiwa yamekwama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. barabara ya masasi-ndanda si ya lami kweli? lami imeenda wapi?

    ReplyDelete
  2. Hapa panahitajika barabara inayopitika wakati wote.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...