Arsene Wenger jana alipatwa na majanga mawili ya mwaka baada
ya kula mweleka muda mfupi baada ya timu yake ya Arsenal kupigwa 5-1 na Liverpool.
Meneja huyo wa washika bunduki wa Uingereza alikuwa
anawahi treni kurudi London katika mtaa wa Lime jijini Liverpool akiwa na
wachezaji wake alipoteleza na kuanguka pwa!
Meneja huyo mwenye umri wa miaka 64 anaokenana
pichani akiwa anaburuta begi lake wakati akiingia stesheni, lakini mara tu
baada ya kuvuka mlango wa kuingilia, anateleza na kula mweleka.
Mfaransa huyo aligumia kwa maumivu wakati askari
polisi wawili walipofika kumsaidia. Msemaji wa Arsenal alinukuriwa baadaye
akisema kuwa mzee mzima hakuumia na hajambo.
Pole masikini, sifikiri kama wenye nyumba walikuwa wapo, maana akili zake zote zilikuwa
ReplyDeletezafikiri, hivi kichapo hiki ni kweli ama ni ndoto tu.