Mhe. Hussein Kattanga, Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, akifungua mafunzo hayo rasmi jana, katika maneno yake ya ufunguzi Kattanga amewaasa Makarani kutokufanya kazi kwa mazoea bali kufanya kulingana na misingi ya maadili ya Mahakama iliyopo lengo likiwa ni kubadili taswira ya Mahakama kwa wananchi, (kushoto) ni Msajili wa Mahakama ya Ardhi, Mhe. Lameck Mlacha, kulia ni Naibu Mkurugenzi Mafunzo, Bi. Rehema Vyas.
 Mmoja wa Makarani kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, akipendekeza jambo mbele ya Mtendaji Mkuu kuhusiana na maboresho ya huduma ya utoaji haki kwa wananchi.
Baadhi ya Makarani wa Mahakama wakiwa katika Mafunzo hayo yanayofanyika katika Chuo cha Learnit kilichopo jijini Dar es Salaam.
 1.      Mhe. Hussein Kattanga akiwa darasani kushuhudia baadhi ya wanafunzi hao wakipewa somo kuhusiana na mfumo wa kuingiza taarifa za mashauri/kesi kwa kutumia kompyuta, aliye pembeni na Mtendaji huyo ni Bw. Machumu Essaba, Mkuu wa Kitengo cha ICT, Mahakama ya Tanzania, na wengine waliosimama kwa nyuma ni baadhi wa wakufunzi wa Mafunzo hayo ambao pia ni Watumishi wa Mahakama, Kitengo cha ICT. 
 Mtendaji akiendelea kushudia wanafunzi wakiwa katika mafunzo hayo. Lengo la Mahakama ni kuhakikisha kuwa huduma ya utoaji haki nchini inapatikana kwa urahisi kwa kutumia njia za teknolojia hususani katika kuingiza taarifa muhimu za kesi kwa kutumia kompyuta. Mafunzo hayo ambayo yatachukua jumla ya siku 21 yanajumuisha jumla ya Makarani 30 kwa kila wiki, ambapo kundi la kwanza litamaliza mafunzo yake siku ya Jumapili 02.03.2014.         
  Mgeni rasmi aliyefungua mafunzo hayo ya Makarani, Mhe. Hussein A. Kattanga, Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania (katikati), Mhe. Lameck Mlacha, Msajili wa Mahakama ya Ardhi (kushoto), pamoja na Bi. Rehema Vyas, Naibu Mkurugunzi Mafunzo, Mahakama ya Tanzania wakiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi (Makarani) wanaohudhuria katika mafunzo hayo na baadhi ya Wakufunzi wa mafunzo hayo. 
Picha na Mary Gwera, Mahakama ya Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...