Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa a(BMT) Dionizi Malinzi (wapili kulia)akikabidhi kombe kwa kapteni wa timu ya sekondari ya Mugabe Laurian Didas baada yakuibuka mabingwa katika michuano maalumu ya Community Sports Cup ambapo walishinda jumla ya bao 1-0 dhidi ya shule ya sekondari ya Kawe,( wa pili kutoka kushoto) ni Meneja Uhusiano wa Nje wa Vodacom Tanzania, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Leonard Tadeo, Katibu Mkuu wa BMT Henri Lihaya (wakwanza kutoka kulia). Michuano hiyo imemalizika rasmi kwa udhamini wa kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania.
Mashabiki wa timu ya sekondari ya Mugabe wakishangilia baada yakuibuka mabingwa wa michuano maaalum ya Communnity Sports Cup baada ya kuichapa timu ya sekondari ya Kawe bao 1-0 katika fainali zilizopigwa kiwanja cha Turiani Sekondari. Michuano hiyo imemalizika rasmi kwa udhamini wa kampuni ya mawasiliano ya Vodacom Tanzania.
Meneja wa Uhusiano wa nje wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim (aliyevaa flana nyekundu) akiwa kwenye picha ya pamoja na timu ya Sekondari ya Mugabe kabla ya fainali hiyo ya mashindano maalum ya Community Sports Cup kuanza katika kiwanja cha Turiani Sekondari. Mashindano hayo yamewezeshwa na kudhaminiwa na kampuni ya Vodacom Tanzania.
Meneja wa Uhusiano wa nje wa Vodacom Tanzania Salum Mwalim (aliyevaa flana nyekundu) akiwa kwenye picha ya pamoja na timu ya Sekondari ya Kawe kabla ya fainali hiyo ya mashindano maalum ya Community Sports Cup kuanza katika kiwanja cha Turiani Sekondari. Mashindano hayo yamewezeshwa na kudhaminiwa na kampuni ya Vodacom Tanzania.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...