Baraza la madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni limepitisha bajeti ya sh.bilioni 121 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo ya halmashauri kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015.


Akitoa taarifa hiyo Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Mheshimiwa Yusuph Mwenda alisema fedha hizo zimetokana na makusanyo ya vyanzo vya mapato , pesa kutoka ruzuku serikali kuu,Tamisemi,pesa za makusanyo ya ndani ya Halmashauri .Kwa sasa Halmashauri ina uwezo wa kujiendesha kwa asilimia 30 tofauti na hapo nyuma ambapo ilikuwa ikijiendesha kwa asilimia 20 tu.

Bajeti ya mwaka 2014/2015 ina lengo la kutekeleza mipango ya maendeleo na kuwaondolea umaskini wakazi wa kinondoni na kuboresha maisha yao.Imetolewa na Manispaa ya Kinondoni.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Ingependeza km hao Halmashauri ya Kinondoni wangefafanua mfano ktk hizo bil 121 bilioni kadhaa ni kwa ajili ya kitu fulani.

    hii inasaidi hata wakazi wa eneo husika kujua kuwa kuna mpango kazi wa kitu fulani mwaka huu.

    mfano. mwaka huu tunaamua kujenga barabara inayo toka sehemu fulani mpaka sehemu fulani.

    pia tunatarajia kuiboresha hospitali fulani labda kuwawekea huduma ya X-Ray hivyo wakazi wa eneo hilo hawatakua na haja tena ya kwenda Mwanamala kwa ajiluli ya kupata huduma.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...