Mkuu wa Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Prof. Mjema akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam kuhusu habari za upotoshaji zilizoandikwa na gazeti moja la kila siku na baadhi ya mitandao ya kijamii kuhusu chuo hicho, leo jijini Dar es salaam.

Na. Aron Msigwa – MAELEZO.

Mkuu wa chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) kampasi ya Dar es salaam Prof. Emanuel Mjema amesema kuwa habari zilizoandikwa na kuchapishwa na gazeti moja la kila siku na baadhi ya mitandao ya kijamii hapa nchini zililenga kukidhalilisha chuo na kuipotosha jamii kufuatia chuo hicho kuendelea kufanya vizuri katika kulinda maadili na viwango vya taaluma hapa nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam mkuu wa chuo hicho amesema kuwa habari zilizochapishwa kuhusu kuwekwa kwa mfumo wa kamera za kisasa madarasani na taarifa ya kufukuzwa kwa mwalimu mmoja wa chuo hicho akihusishwa na vitendo vya ngono na wanafunzi zimepotoshwa na vyombo hivyo kwa kukosa weledi wa kushindwa kupata uhalisia na usahihi wa habari husika kutoka mamlaka za chuo hicho.

Prof. Mjema amesema kuwa Chuo cha Elimu ya Biashara ni Chuo cha Serikali ambacho kimekua kikitoa Elimu ya Biashara kwa miaka 49 na kuongeza kuwa chuo hicho kinaajiri wakufunzi wake kupitia utaratibu wa serikali wa kutangaza nafasi za kazi kupitia Tume ya Ajira iliyopo chini ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa umma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...