Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za CCM Mkoa wa Mwanza.Nape alisema kitendo cha wana CCM kushambuliwa ni kitendo cha kinyama na kinatakiwa kikemewe na kila mtu,pia alisisitiza Vijana wa CCM kuwalinda wapigaji kura wao siku ya kupiga kura.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisisitiza jambo wakati wa mkutano wake na waandishi wa Habari kwenye ofisi za CCM Mkoa wa Mwanza.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitazama picha ya X-Ray  ya Sebastian Masonga Katibu wa UVCCM kata ya Majengo Wilaya ya Kahama,Masonga amevunjika mkono wa kushoto baada ya kupigwa na wafuasi wa Chadema wakati walipokua wanarejea kwenye mikutano ya  kampeni za Udiwani.
Katibu wa NEC Itikadi na uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akimpa pole Afisa Mtendaji wa Kata ya Ubagwe wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga ambaye alipigwa na kutobolewa macho na wafuasi wa Chadema .
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoka nje ya jengo la hospitali ya Bugando akiongozana na baadhi ya viongozi wa CCM Mkoa wa Mwanza ambapo waliwatembelea na kuwajulia hali majeruhi walioumizwa na wafuasi wa Chadema mjini Kahama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Sasa kila mtu anaweza kusoma xray ya mgonjwa? Taaluma ya udaktari imeingiliwa.

    ReplyDelete
  2. Oh, it is so sad that people can actually inflict life-long pain on to other fellow Tanzanians! I am really sorry for the afflicted.
    Nape, that was so kind of you to visit the rank-and-file member who put their lives on line for what CCM stands for. I liked your sober statement. Let us trust in the law, and system.

    ReplyDelete
  3. Dr nape doing his thing

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...