Wazee wa kabila la Kihehe, kata ya Kalenga mkoani Iringa wakimpa heshima ya kichifu  alipokuwa Mkurugenzi wa Vodacom Tanzania Kanda ya Kusini Jackson Kiswaga ambae  leo anapigiwa  kura  za maoni  za  kusimamakugombea  ubunge  kupitia  CCM jimbo la Kalenga

Bw Kiswaga  akiwashukuru  wana kalenga
kwa maombi  na imani  yao kwake.

Na Francis Godwin, Iringa
Wakati  leo  wajumbe wa Halmashauri  kuu ya CCM jimbo la Kalenga  wanakutaka  katika ukumbi wa Siasa ni Kilimo mjini Iringa  kumteua  mgombea  ubunge  kupitia  CCM katika  jimbo la Kalenga  wana Kalenga  wasema isingekuwa demokrasia  kwa  kila mmoja kugombea basi  wangempitisha moja kwa moja  Jackson Kiswaga  kuwa mbunge  wao

Wamesema jitihada zake  za kimaendeleo  katika  jimbo la Kalenga na mkoa  wa Iringa ni kubwa na hakuna mgombea  hata mmoja kati ya  tisa  waliojitokeza ambae anaweza kumfikia  Kiswaga katika  kujitolea  kwa shughuli za kimaendeleo jimbo la Kalenga na  mkoa wa Iringa .

Wameongezea kuwa  Samson Kalinga  kuwa  hata  wakati  wa uhai  wake  mbunge wa  jimbo  hilo Dr  Wiliam Mgimwa alipata  kumpongeza  kwa  kuonyesha ukeleketwa wa kweli wa maendeleo ya wana Kalenga kwa  kuchangia shughuli mbali mbali  za kimaendeleo .

Hata  hivyo  alisema imani ya  wana kalenga  ni kuona  wana CCM hao  leo  wanamchangua mtu  mwenye  malengo ya kweli  ya  kuwakomboa wana Kalenga  kama  ilivyo kwa Kiswaga na  si vinginevyo .

Kiswaga  amepata  kujitolea  kuchangia  sekta  ya elimu kwa kujenga madarasa katika  shule ya  sekondari Lipuli, kununua  vitanda  vya  kujifungulia  wakina mamaa Hospital ya Ipamba , kuchangia  madawati na umeme shule ya msingi Tanangozi ,kuchangia madawati shule ya msingi Lulanda na maeneo mengine  mengi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...