Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony Mtaka , akizumgumza na Waandishi wa Habari mjini Morogoro kutoa pongezi na kumshukuru Waziri Membe .

Na John Nditi, Morogoro

RAIS wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony  Mtaka  amemshukuru Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe  kwa kuanzisha diplomasia ya michezo na nchi za nje pamoja  na kufadhili maandalizi ya wanariadha 40 na makocha sita.

Wanamichezo  na makocha hao wanapelekwa nje kwa ajili ya kujinoa  ili kuwa tayari kwa ajili ya Mashindano ya Jumuiya ya Madola  yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Julai 23 hadi Agosti 3, mwaka huu , Glasgow , Scotland. 

Rais huyo wa RT alimshukuru Waziri Membe, alipozungumza  na waandishi wa habari Mjini Morogoro , Februari  21, 2014 na kusema  kitendo  cha kuanzisha diplomasia ya mchezo  na nchi za  nje  kimetoa  majawabu kwa wanamichezo na viongozi wa Tanzania wanalodeni  la kurejea na  medali za kutosha kutoka kwenye  mashindano hayo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...