Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony Mtaka , akizumgumza na Waandishi wa Habari mjini Morogoro kutoa pongezi na kumshukuru Waziri Membe .
Na John Nditi, Morogoro
RAIS wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT), Anthony Mtaka amemshukuru Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe kwa kuanzisha diplomasia ya michezo na nchi za nje pamoja na kufadhili maandalizi ya wanariadha 40 na makocha sita.
Wanamichezo na makocha hao wanapelekwa nje kwa ajili ya kujinoa ili kuwa tayari kwa ajili ya Mashindano ya Jumuiya ya Madola yanayotarajiwa kufanyika kuanzia Julai 23 hadi Agosti 3, mwaka huu , Glasgow , Scotland.
Rais huyo wa RT alimshukuru Waziri Membe, alipozungumza na waandishi wa habari Mjini Morogoro , Februari 21, 2014 na kusema kitendo cha kuanzisha diplomasia ya mchezo na nchi za nje kimetoa majawabu kwa wanamichezo na viongozi wa Tanzania wanalodeni la kurejea na medali za kutosha kutoka kwenye mashindano hayo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...