TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 07.02. 2014.


·         WATU 03 WA FAMILIA MOJA WAFARIKU DUNIA BAADA YA KUANGUKIWA NA UKUTA MKOANI MBEYA.

·         WATU 07 WAKAMATWA NA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA WAKIWA NA POMBE HARAMU YA MOSHI.


WATU 03 WA FAMILIA MOJA WAFARIKU DUNIA BAADA YA KUANGUKIWA NA UKUTA MKOANI MBEYA.

watu watatu wa familia moja waliotambulika kwa majina ya steven mwaijombe (35) baba wa familia, ester kibona (25) mama wa familia na mtoto wao edgael steven mwaijombe (02) wote wakazi wa sogea walifariki dunia baada ya kuangukiwa na ukuta wa nyumba yao wakiwa wamelala. tukio hilo lilitokea mnamo tarehe 07.02.2014 majira ya saa 04:45hrs usiku wa kuamkia leo huko eneo la sogea kata na tarafa ya tunduma wilaya ya momba kufuatia mvua kubwa zinazoendelea kunyesha mkoani mbeya. miili ya marehemu imehifadhiwa katika kituo cha afya tunduma. kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi ahmed z. msangi anatoa pole kwa ndugu na majirani wa familia hii kutokana na janga hilo. 

WATU 07 WAKAMATWA NA JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA WAKIWA NA POMBE HARAMU YA MOSHI.


jeshi la polisi mkoa wa mbeya linawashikilia watu 07 wakiwa na pombe haramu ya moshi [gongo] ujazo wa lita 11/2. katika msako uliofanywa mnamo tarehe 06.02.2014 majira ya saa 19:30hrs usiku huko mwanjelwa na mafiata jiji na mkoa wa mbeya emanuel mbwete (27) mkazi wa makunguru akiwa na wenzake 05 walikamatwa wakiwa wanakunywa pombe haramu ya moshi. pia katika msako mwingine hamasha paulo (25) mkazi wa forest mpya alikamatwa akiwa anakunywa pombe ya moshi. taratibu za kuwafikisha mahakamani watuhumiwa zinafanyika. kamanda wa polisi mkoa wa mbeya kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi ahmed z. msangi anatoa wito kwa jamii hasa vijana kuacha matumizi ya pombe haramu ya moshi kwani ni kinyume cha sheria na ni hatari kwa afya ya mtumiaji.


Signed by:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Nimesikitishwa na hiyo taarifa, haijakaa kiumakini, haijawa edited, taarifa ni ya kiswahili lakini imechanganywa na kiingereza...this is not professional kwa kweli

    ReplyDelete
  2. na wewe mdau wa namba moja umechanganya kiingereza na kiswahili. unakosoa nimi na unafanya nini? ni kweli taarifa iandikwe kwa kiswahili fasaha nakuunga mkono mdau. ni jukumu la wahusika kuliangalia hilo. kazi njema

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...