Muwakilishi wa Kudumu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akizungumza mwanzoni mwa Mkutano wa Mwezi mmoja wa Wajumbe wa Kamati Maalum ya Usimamizi wa Operesheni za Ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa, (C-34). Katika baadhi ya mambo aliyosititiza ni pamoja na kuangaliwa upya kwa posho ya kila siku wanayolipwa walinzi wa amani ambayo ni dola 1.28, posho ambayo imedumu kwa miaka 20 bila ya kufanyiwa mabadiliko. Mkutano huo unafanyika hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York, Marekani. Aliyeketi nyuma kwa Balozi, ni Lt. Kanali Wilbert Ibuge Mwambata Jeshi katika Uwakilishi wa Kudumu.
Baadhi ya Waambata wa Kijeshi wanaoziwakilisha nchi zao Katika Umoja wa Mataifa, wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi kabla ya ufunguzi wa Mkutano wa Mwezi mmoja wa Kamati Maalum ya Usimamizi wa Operesheni za Kulinda Amani. Katika Mkutano huu wajumbe ambazo ni kutoka nchi ambazo zinachangia walinzi wa amani watajadili sera zote zinazohusu ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...