Raia wa  Ugiriki, Alexamdrios Atanasios, amekamatwa maafisa wa usalama wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam Jumapili usiku Februari 24, 2014, akiwa na kilo tano za madawa ya kulevya.
 Habari zinasema mzungu huyo alikamatwa wakati wa upekuzi, akijiandaa kupanda ndege ya Swiss air kueleke jijini  Zurich, Uswisi. 
Madawa hayo yalikutwa yakiwa yamefichwa kwenye “sakafu” ya begi lake baada ya mitambo ya kisasasa yaupekuzi, kugundua kuwa kulikuwa na ‘mzigo’.
Habari zinasema, kwa sasa mtuhumiwa anashikiliwa kwenye kituo cha polisi cha uwanjani hapo  akisubiri taratibu za kisheria ili afungukliwe mashtaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 13 mpaka sasa

  1. Kautoa wapi? Again hatuwezi kuua mmbuyu kwa kukata matawi.lazima kuongoa mizizi.Hawa punda wanaoshikwa kwenye Airports kunawanao wamiliki.

    ReplyDelete
  2. Hiyo Henellic ni nchi gani wajameni?

    ReplyDelete
  3. Good work to the airport personnel in finding the 'unga wa kulevya'. You deserve a bonus. Hili lijamaa must have thought that atapita tu maana wafanyakazi wa airport wapo wapo tu. But he was not so lucky THIS time eh!!

    ReplyDelete
  4. hiyo nchi ndio kwanza naisikia

    ReplyDelete
  5. Kwanini mmetoa picha yake hadharani?Si mtaaribu upelelezi wenu au?(Utani.....)?.Kama alivyosema mwana blog ya jamii hapo juu,aliutoa/nunua soko gani?

    David V

    ReplyDelete
  6. Jamani tumechoka kuonyeshwa wanaokamatwa kisha hatusikii mwisho wa hiyo taarifa, yule mke wa kigogo aliekamatwa na kete kaziweka kichani kaishia wapi na wengine wengi. Mdau wa hii blog hebu fanya uchunguzi utuhabarishe kinachoendlea katika hizi kesi za madawa ili hata hawa wanaotaka kuendeleza waogope kwa kigezo cha hao walio kamatwa

    ReplyDelete
  7. Kule Oman yule Zahoro matelephone kesi yake ilikwenda siku 5 tu , hapa kwetu kesi za unga zinachukuwa miaka na miaka tokea mtoto amezaliwa mpaka anaanza shule ya msigi kesi hazijahukumiwa lengo lake hasa silijui ni Hongo au nini? nchi imeoza kweli hii

    ReplyDelete
  8. isije kuwa ulikuwa wa matumizi yake binafsi

    ReplyDelete
  9. Afadhali ulikuwa unatoka kwenda nje ya nchi kuliko kuingia nchini! lol

    ReplyDelete
  10. tusubiri tuone hii issue itaishia wapi

    ReplyDelete
  11. Jamani isije kuwa kabeba kwa matumizi yake binafsi

    ReplyDelete
  12. Haya mambo ya unga yamezidi kabisa. Ukiangalia athari zake zinatisha.

    ReplyDelete
  13. hukumu ya sembe kiasi hicho huko kwao ugiriki ni kifungo cha maisha nayeye apewe hocho hicho hapo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...