KaTtibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Maji wa MCAT (Millenium Challenge Acount Tanzania,Bwana William Christian kuhusianana namna maji yanavyokusanywa na kusambazwa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Pwani na Jiji la Dar,kati ni Mkuu wa Mkoa wa Dar,Mh.Mecky Sadicky akisikiliza.
 KaTtibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akiwaongoza viongozi wa CCM Wilaya ya Kinondoni kutembelea mitambo mipya baada ya upanuzi wa mitambo ya maji ya Ruvu Chini, wilayani Bagamoyo, kufanyika. Ujenzi wa mitambo hiyo umegharimu sh. Trilioni 1.6. Mradi huo unaotarajia kukamilika mwaka huu utapunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la maji katika Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam. Kinana amemaliza ziara yake jijini Dar,wilayani Kinondoni pia kwa kutembelea kituo cha mabasi ya mjini kilichopo sinza na kufungua tawi jipya la vijana wakereketwa Kawe.
 Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akiendelea kupata Maelezo kutoka kwa kutoka kwa Mkurugenzi wa Maji wa MCAT (Millenium Challenge Acount Tanzania,Bwana William Christian,juu ya mitambo hiyo mipya ya kuchujia maji.Ndugu Kinana alieleza kuwa ameridhishwa na namna ya kazi ya upanuzi wa mitambo mipya ya maji Ruvu chini inavyoendelea,ameeleza kuwa kazi hiyo ya upanuzi ikikamilika basi jiji la Dar na maeneo mengine mbalimbali tatizo la maji litapungua kwa asilimia kubwa. 
Ndugu Kinana na Ujumbe wake wa CCM kutoka Wilaya ya Kinondoni wakiangalia sehemu ya kuchanganyia dawa za maji kabla ya kusambazwa kwa matumizi mbalimbali.
 upanuzi wa mitambo ya maji ya Ruvu Chini, wilayani Bagamoyo, ukiendelea.

  KaTtibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana pamoja na  viongozi wa CCM Wilaya ya Kinondoni wakipata maelezo mafupi kuhusiana na usambazaji wa maji maeneo mbalimbali sambamba na namna ya upanuzi wa mitambo mipya ya maji ya Ruvu Chini, wilayani Bagamoyo, a Ujenzi wa mitambo hiyo umegharimu sh. Trilioni 1.6. Mradi huo unaotarajia kukamilika mwaka huu utapunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la maji katika Mkoa wa Pwani na Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...