Mkuu wa wilaya ya Lindi,Dr Nassor Ally Hamid akifungua mafunzo kwa wanahabari na waratibu wa NHIF/CHF wa mkoa wa Lindi,Kushoto ni Meneja Nhif Lindi,Bi Fortunata Kullaya na kutoka kulia ni Bw Faustine Nzota,Mshauri wa Mfuko wa Afya na anaefuata ni Mwenyekiti wa Bodi ya Afya Wilaya ya Nachingwea,Christopher Lilai.
Meneja wa NHIF Mkoa wa Lindi akitoa taarifa fupi kuhusiana na mfuko huo katika mafunzo ya wanahabari na waratibu wa Mifuko ya CHF na NHIF Lindi.
Mratibu wa CHF wilaya ya Liwale akichangia kuboresha mfuko huo katika mkutano wa mafunzo kwa wanahabari na waratibu.
Washiriki wa Mkutano huo.

Na Abdulaziz Video,LINDI

MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) pamoja na Mfuko wa Afya ya jamii (CHF) mkoani Lindi,imeanza kutoa mafunzo kwa waandishi wa Habari na waratibu wa Mifuko hiyo,ili kuboresha utendaji kazi ili kutatua changamoto za Afya kwa jamii ya wakazi wa mkoa huo.

Akimkaribisha Mgeni Rasmi katika Mafunzo hayo,Meneja wa (NHIF) mkoani hapa, Fortunata Raymond Kullaya ameeleza kuwa mafunzo hayo yaliyojumuisha waandishi wa habari na waratibu kutoka Halmashauri zote sita za mkoa huo yamelenga katika kuboresha utendaji wa kazi na kubaini changamoto mbalimbali zinazokwamisha jamii kujiunga na mifuko hiyo ukiwemo wa Afya ya Jamii(CHF).

Aidha alibainisha kuwa wanahabari wanashiriki vizuri katika kuhamasisha na kuwapa wananchi taarifa muhimu, zikiwemo za kujiunga na Mifuko hiyo ya (NHIF na CHF) ili kuwaondolea usumbufu pale wanapokwenda kupata huduma za matatibabu pale wanapougua.

Kullaya pia alisema kuwa Ofisi yake imeona upo umuhimu wa kuwapatia mafunzo hayo ili wanahabari waweze kuielimisha jamii iweze kubaini fursa zitakazowezesha utatuzi wa Changamoto hasi na chanya za huduma sanjari na kubadilishana uwezo wa kiutendaji baina yao na watumishi wa mifuko hiyo.

Kullaya akataja sababu nyingine ni pamoja na kuwapa elimu ya mabadiliko yaliyotekelezwa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya afya pamoja na maboresho yaliyokwishatekelezwa hivi karibuni na kuwa na kauli moja. "Kama mjuavyo ugonjwa unapokwenda kwa mwanadamu haupigi hodi,hivyo muda unapokujia huna pesa za kujitibia,Bima yako itakusaidia kukuwezesha kupata matibabu sehemu yeyote hapa nchini kwetu"Alisema Kullaya.

Akifungua Mafunzo hayo,Mgeni Rasmi ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Lindi,Dr Nassor Ally Hamid aliwataka Waratibu wa Mifuko hiyo kuhakikisha dawa zinapatikana na Wahudumu wa Afya wanakuwa na Lugha Mzuri kwa wagonjwa wanaowahudumia ambapo pia aliitaka ofisi ya NHIF Pia kutumia viongozi mbalimbali wa Serikali katika kuhamasisha kutokana na Idadi ndogo ya Jamii kujiunga na mfuko wa Afya ya Jamii ambapo kwa mkoa wa lindi ni asilimia 6.6 tu ndio iliyojiunga na mfuko huo.

Katika kupunguza makali ya Tiba katika hospital za Binafsi licha ya kuwa na gharama ndogo za Uchangiaji kwa kaya ambapo unalipa mara moja kupata huduma za Tiba kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Nae Mwenyekiti wa Klabu ya waandishi wa Habari mkoa wa Lindi,Abdulaziz Ahmeid ameahidi kushirikiana na ofisi hiyo ili wanahabari watumie kalamu zao katika kuhakikisha Jamii inapata huduma stahiki ikiwemo kushauri pale ambapo kuna changamoto zinazochangiwa na watoa huduma sambamba na kutoa wito kwa Wanahabari kujiunga na mifuko hiyo badala ya wao kuhamasisha tu.

Mafunzo hayo ya siku moja yaliyoratibiwa na Ofisi ya Mkoa ya NHIF pia wito umetolewa kwa zahanati,Vituo vya Afya vilivyopo mkoani humo kutumia fursa ya kukopa Vifaa tiba kwa mikopo na nafuu Kupitia katika mfuko huo ambapo malipo yake yatakatwa kupitia madai mbalimbali wanapowahudumia wagonjwa wa Mfuko wa NHIF

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...