Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John M. Haule (kushoto) akiwa pamoja na Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Mhe. Lu Youqing wakati wa mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari maelezo siku ya Jumanne tarehe 25 Machi, 2014. Mkutano huo ulizungumzia maadhimisho ya miaka 50 ya ushirikiano wa kidiplomasia  kati ya Tanzania na China na mafanikio ya ziara ya Rais wa China aliyoifanya nchini ambayo imetimiza mwaka mmoja.
Sehemu ya waandishi wa habari walioshiriki mkutano wa waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari maelezo. 
Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki (kushoto) akiteta jambo na Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Msemaji wa Serikali, Bw. Assah Mwambene wakati wa Mkutano wa Pamoja na waandishi wa habari kati ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Balozi wa China.
Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bibi Mindi Kasiga akisikiliza kwa makini hotuba zilizokuwa zikitolewa. wengine ni maafisa wa Ubalozi China.
Baadhi ya maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje walioshiriki mkutano huo. 
Picha ya pamoja, kutoka kulia ni Balozi wa China, Mhe. Lu Youqing; Katibu Mkuu, Bw. John M. Haule; Mkurugenzi Msaidizi katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Nathaniel D. Kaaya; Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje, Bibi Mindi Kasiga na Afisa kutoka Ubalozi wa China.

KUSOMA HOTUBA YA  KATIBU MKUU WA WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...