Askofu Mkuu wa Kanisa la Kilutheri (KKT) dayosisi ya  Iringa  Dkt. OwdenburgMdegela
Wachungaji na  msaidizi wa Askofu kulia wakifuatilia salam za  pasaka zilizokuwa  zikitolewa na askofu Dkt. Mdegela
Waumini  wa KKKT usharika wa kanisa  kuu Iringa leo.
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA
Na  Francis Godwin, Iringa 

ASKOFU mkuu wa Kanisa la Kilutheri (KKT) dayosisi ya  Iringa  Dkt. OwdenburgMdegela ameitumia ibada  ya Jumapili ya Pasaka leo  kulaani vikali  wale wote  wanaowatukana waasisi wa Taifa  hili Sheikh Abeid Amani Karume  na Mwalimu hayati Julius Kambarage Nyerere.
Askofu Dkt  Mdegela amesema kuwa watu hao wanapaswa kuwaomba radhi  watanzania huku akisisitiza wajumbe umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA) kurejea bungeni ama  kufungasha  virago  vyao na kurudi nyumbani kwao na sio kuzunguka kupandikiza chuki kwa wananchi.
Askofu Dr Mdegela aliyasema hayo leo  wakati akitoa  salam za pasaka kwa  waumini  wa Dayosisi hiyo kupita washarika wa  kanisa  kuu.

Dkt. Mdegela asema "Watanzania tunataka  kuikataa lulu tuliyopewa na Mungu lulu ya amani na  kuanza  kutafuta kuvuruga amani  na utulivu  wetu ambayo ni lulu ya pekee inayogombewa na nchi  nyingine na  kuwa  wanaotaka lulu  hiyo ivurugike wasivumiliwe kamwe.
"Kinachofanywa  bungeni kwa  sasa ni mzaha wa hali ya juu na  Watanzania wanapaswa  kuwachunguza vema  wawakilishi wao hao wakiwemo wabunge wa vyama  vyote na  wale wanaoeneza mbegu ya  chuki  wasichaguliwe tena...."

Asema wajumbe wa bunge la katiba  hawana  sifa ya  kutengeneza katiba kwani  wametanguliza mzaha na matusi  yasiyo na tija  na kuwa hawa  wanaokwepa  bunge na kutaka kuzunguka kwa wananchi  wanapaswa kuzuiwa kufanya  hivyo na vyombo vya usalama kwani wanataka  kuipeleka nchi pabaya.
"Kama wamekula pesa za wananchi kwa muda  wote huo kwa ajili ya kuunda katiba iweje  leo  watoke bungeni na kudai  kuja kwa wananchi mikono mitupu??" amehoji.

"Wananchi tuwakatae wajumbe  wanaotaka  kuzunguka kupandikiza  chuki kwa wananchi kwa kujiita  wao wapo kwa ajili ya katiba ya  wananchi hali  wamekimbia bunge na kutaka  kutuwakilisha nje ya  bunge 
"....tunawakataa  wao na mawazo yao na pia kama wajumbe wa bunge  hilo  wameshindwa kazi tutaikataa rasmu ya katiba ambayo italenga  kutugawa  watanzania.
"Na niweke  wazi mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba Jaji Joseph Warioba mbali ya kazi  hiyo bado tunawajibu wa kumrekebisha pale  alipokosea kwani Wazanzibar wa Pemba wanataka serikali nne sio tatu mbona hajaeleza
" ....nasema serikali mbili ni  jibu kama haiwezekani bado tuwe na serikali moja itakayotuunganisha"
Hata  hivyo Dr Mdegela alisema  kuwa msimamo  wake na waumini  wa kanisa  hilo ni kuwa na serikali mbili na ikiwezekana  kuwa na serikali  moja  pekee na si vinginevyo na iwapo  wajumbe wa  bunge la katiba  wameshindwa kazi na kugeuza  bunge  hilo ni sehemu ya kuonyeshana ujuzi wa kutukanana ni  vema wakirudi katika mwelekeo mzuri ama kurudi majumbani kwao  ili viongozi wa dini mashekhe na maaskofu wakaifanya kazi hiyo ya kuunda katiba  bila kutukanana .

"Nimejizuia  sana kwa kipindi  hiki  cha bunge la katiba  nisiseme  chochote ila  kutokana na mambo jinsi yanavyokwenda uvumilifu  umenishinda nimelazimika  kusema na ninachosema nimekiandika ili  wale  wapotoshaji washindwe  kupotosha ninachosema....wayahudi  walikataa kuongozwa na Samweli kwa  sababu walisema  watoto wa Samweli wanatabia  mbaya ...walikataa kuongozwa na Mungu kwa madai  kuwa na  wao  wanataka mfalme wetu  uli tukienda  kupigana na watu  ili  tuwe kama mataifa  mengine  ila Mungu hakutaka wao  kuwa kama mataifa  mengine  ila  wao  wanataka  kuwa kama mataifa  mengine ....Samweli akaenda mbele ya Mungu akilia ....ila  Mungu akasema hawajakukataa wewe  wamenikataa mimi ...enyi  watanzania tukikataa lulu  tuliyopewa na Mungu ya kuwa nchi ya amani  tutakuwa hakuwakatai viongozi  wetu  tutakuwa tunamkataa Mungu"

Aliwataka  watanzania  kuyatazama mataifa  jirani kama Kenya ambao  walijipenda  wao na kushindwa  kuwapenda  majirani  sasa  Wasomari  wameingia wanawasumbua  ila tazameni pia Malawi ambao walimtaka rais  wao awe Joys Banda ila alipoingia tu Ikulu alitangaza ndoa za jinsia moja pamoja na nchi ya Kongo ambayo imesaidiwa na Tanzania kurudi katika amani ikiwemo nchi ya Burundi  ambayo Rais  wake amekuwa akishinda katika maombi kwenye kanisa lake na kuacha kuongoza nchi.

"Tunapaswa  kujiuliza amani  hii iweje  leo  ichezewe na  watu  wachache  wenye uchu wa madaraka na hata  kususa  bunge la katiba ...hatujifunzi  kutoka nchi  za majirani  zetu kama Uganda ,Rwanda kuna  vyama 10  vya upinzani na kuna  vikundi 10  vinavyotaka  kumpindua Rais huku Uganda kuna mtu anaitwa Kony yeye  siku  zote  kumshumbua Rais ....ninyi ni nani  Tanzania bara  na visiwani mkaa kwenye amani kiasi hiki na mnakataa umoja na kuanza kuwasikiliza  wanaopandikiza mbegu ya kuvuruga amani ya kutaka serikali tatu ....watanzania tunataka  kuikataa lulu tuliyopewa na Mungu lulu ya amani"

Dr Mdegela  alisema kuwa hadi  sasa mwenendo  wa  bunge la katiba unatia aibu kubwa kwa  Taifa na hata nje ya taifa   hili na kuwataka  wajumbe hao  kuwa wasikivu na kama  walisema  wanakwenda kuandaa katiba ya  wananchi iweje kabla ya  kuanza kwa  bunge  hilo walianza kwa kulilia posho kuongezwa hali  wakijua  walimu hawajalipwa malipo yao pamoja na  wafanyakazi  hawajaongezwa mishahara yao.

"Natamka  wazi  kuwa  mimi Dr Mgedela sina  imani hata  kidogo na  wajumbe wa  bunge la katiba .....kama  wanavyoonekana na  walivyo wana hadhi ya kutoridhika  watatuletea  katiba mbovu kwa  sasa na  wao  ni wabovu ..
"Natamka rasmi  kuwa  tume iliyoandaa rasmi ya katiba haukuandaa msaafu  wala Biblia  ili andaa kitu ambacho  mbacho  kinaweza  kuhojika na kukataliwa  ama kukubalika  wao  si Miungu ni  wanadamu kama  sisi madai kuwa wanavyeo vingi  serikalini hata mfagiaji anavyo ....sasa naiomba serikali hao  waliojitoa bungeni wanataka kuja kwa wananchi tunasema hatuwataki ....
"Hivi kama mtu ameshindwa  kujenga  hoja bungeni watakuja kutueleza nini nawaombeni usalama wa Taifa fanyini kazi ya kulinda amani yetu ....kama hawataki kurudi bungeni basi waende majumbani kwao"

Askofu Dr Mdegela  alisema kanuni za bunge  wametunga  wao na iweje leo  wanakimbia kanuni waliyoitunga hivyo kama  wanaona kanuni  ni mbaya  basi  watuombe Watanzania wenye akili tuwasaidie hata   yeye anaweza kwani  wajumbe hao ni walafi  wasiopenda amani ya nchi hii.

Katika  hatua  nyingine  askofu  huyo  alisema kwa  sasa  kinachoendelea na kuwa  kila kanda  itataka  serikali  yao iwapo  hoja  ya  serikali tatu  ikapitishwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. well said doctor Mgedela! Hawa ukawa wanachezea lulu tulioachiwa na waasisi wetu.. Ankal kama una video ya hii speech naomba uitupie humu jamvini tafadhari.

    mdau,
    ughaibuni

    ReplyDelete
  2. sawa baba askofu tumekusikia hayo ni mawazo yako na ni haki yako au kama ya kanisa lako pia ni haki yenu kuyatoa sharia za nchi hazikatazi fikra tofauti,sawa iwe za binafsi au taasisi.
    huku Zanzibar na sisi tuna shehe wetu wa msikiti mkuu wa kidongo chekundu nae anataka serekali tatu hayo pia ni mawazo yake au ya msikiti wetu na ni haki yetu kwa mujibu wa katiba na sharia ya nchi hii ya Zanzibar hakatazwi mtu au taasisi yoyote kutoa fikra zao.
    sasa twendeni tukawaulize wananchi wenyewe wanatka serekali ngapi?
    wanasiasa na viongozi wa dini wote tunajua misimamo yao hilo sio geni kilich kigeni ni wananchi wa nchi hii hawajaulizwa wanaogopwa nini?
    mdau.
    Zanzibar.

    ReplyDelete
  3. The mdudu,acheni kuwasemea wananchi coz wananchi wenyewe wanajua kinachoendelea kwasababu wao ndio wenye MATATIZO MAKUBWA KWENYE HII NCHI,nyie mnaosemea wananchi mkumbuke yakwamba mnafanya kazi na mnalipwa mishahara minono na wala kitu njaa kwenu hamjui ni nini,ndio maana sisi wananchi tunataka serikali 3 zenye kuwajibika na nidhamu pasipo na RUSHWA,serikali mbili za sasa zimeshindwa kuleta usawa kwa wote,ndio maana kuna gepu kubwa sn kati ya MASIKINI NA MATAJILI,matatizo ya sisi masikini haya hapa,Hatuna maji safi majumbani mwetu,Hatuna umeme,Hatuna shule za maana,Hatuna hosipital za maana,Hatuna kazi za maana hizo sababu tosha kabisa sisi makabwela kuzitaka hizo serikali 3,hayo matatizo niliyo ya sema hapo kwenu nyie hayapo hasa nyie viongozi na vyama vyenu ndio maana mnazitetea hizo serikali 2,ila sisi hatutaki tena hizo mbili.

    ReplyDelete
  4. Askofu mwenye akili timamu na asiye tumiwa na chama chochote hawezi kutoa kauli ya kuwa huo ni msimamo wa kanisa lake. Hilo ni kosa, sababu katika kundi la hao waumini wake pia kuna wanao penda serikali mbili, tatu au moja. Angesema hayo ni mawazo yake. Msimamo wa kanisa lake ni ile imani yao, sababu ndio iliyowaunganisha. Sasa wakitokea waumini wengine wa kanisa hilo wakasema wanataka serikali tatu atawafukuza katika hilo kanisa? Hayo ndio matatizo ya kuwa wachungaji kisha mnahudhuria mikutano ya ndani inayoongozwa na makada wa chama fulani, sababu mkutano uliitishwa na mkuu wa mkoa. Mnalamba posho na kupewa masharti ya kwenda kutoa tamko kwenye ibada zenu yanayo lingana na matakwa ya vyama hivyo. Shame on you. Mnachanganya mambo ya kaisari na Mungu. Na Shehe mkuu wa mkoa huo akitangaza msikitini kwake yeye na msikiti wake msimamo wao ni serikali tatu. Je hapo hamuja leta mgawanyiko mkubwa katika jamii?

    ReplyDelete
  5. bwana askofu nafikiri kazi yako ni kutuongoza sisi kiroho , hizi siasa tuziache kwa wanasiasa, na kuhusu serikali ngapi tunazitaka au muungano tunautaka basi waulizwe wananchi wa pande zote mbili kwa kura ya maoni , wewe huna haki baba askofu kutuambia chochote kuhusiana na serikali , na mikifanya hivyo mtawafanya na mashehe kule znz na hapa bara waanze kuzungumza siasa misikitini kuelimisha waumini wao ,

    ReplyDelete
    Replies
    1. Asante sana mdau. Wananchi ndio waamuzi wa mwisho katika kura ya maoni. Mengine yote msemayo ni mawazo yenu binafsi.
      Chonde ccm msilete uchakachuaji kwenye hili

      Delete
  6. Baba Askofu big up! Hao UKAWA ni wanafiki, wachochezi! Wanahubiri Utanganyika? Huo ni ukabila!! Hawana tofauti na Makaburu. Msikilize yule Toto Tundu Lissu, msikize mtoto si rizki Jussa chuki tupu, kejeli, matusi, dhihaka. Muungano wa aina gani wanaohubiri? Tuwakatae makanisani tuwakatae misikitini. Mungu ubariki Muungano wetu.

    ReplyDelete
  7. Duh Baba Askofu ulikuwa wapi siku zote? Hawa wana UKAWA Hawana lolote, wameshalaniwa. Leo wanamtukana Nyerere na Karume wana mwisho mwema hao? Hebu wadau angalieni Hansard, mtaona matusi ya Jussa, Abubakari Hamis na wengine . Hawana haja na Muungano . Wao uchochezi na kuhubiri chuki. Hawana nafasi katika Tanzania huru!

    ReplyDelete
  8. Bravo Baba! Muungano wa serikali mbili ndiyo utakaodumisha amani na umoja. UKAWA wana sema wametoka kwa sababu ya ubaguzi. Hivi kuwaita wenzao Intarahamwe siyo ubaguzi ? Wao wanapandikiza mbegu za chuki: Utanganyika , Uzanzibari, huu si ubaguzi? Kero zipo, zitatuliwe! Serikali Tatu, marais watatu, si ndiyo kero zitazidi? Mzigo huo atabeba nani? UKAWA Hawana sera warudi Bungeni wakatunge Katiba!

    ReplyDelete
  9. Mimi, naomba kuuliza swali. Endapo wananchi wanatata serikali tatu ni maana yake maraisi watakuwa watatu? au inakuwaje. Na kama maraisi watatu kwa serikali ya Tanzania mbona tutakuwa ni kama sehemu ya kukumbatia madaraka? Sawa, wananchi wanahitaji serikali tatu lakini hatujui madhala yatakayotokea baada ya serikali tatu. Tuongee na kupima mambo, tuamue jambo kwa busara. Mwenye ufafanuzi wa hili naomba anisaidie. Mdau

    ReplyDelete
  10. Mambo ya Katiba ni masuala ya kisheria. Ni masuala ya raia. Ni makosa watu kutumia nafasi za uongozi wa kidini kuingilia kati mchakato wa raia na mstakabali wa nchi yao.

    ReplyDelete
  11. Marekani wana serikali 52 za majimbo na serikali 1 kuu. Mbona hakuna shida. Watu wako selective sana kwenye kujenga hoja. Eti wanatoa mfano wa Urusi ya zamani, Senegal-Gambia etc. Kila nchi ni tofauti.

    ReplyDelete
  12. Uwepo wa serikali 3 sio matakwa ya wapinzani, bali hayo ni maoni ya wananchi kwa mujibu wa Tume ya Maoni ya Katiba. Hayo ni maoni ya wananchi hata sisi wa ughaibuni tulitoa maoni kwa njia ya mtandao. Iweje kuwasakama wapinzani wakati wao wako sambamba wanaunga mkono mawazo ya wananchi walio wengi, serikali 3 !!. Hawa wanachama wa chama tawala wanaolazimisha serikali 2 kinyume na maoni ya wananchi ndio wanaoleta fujo kwa sababu kuanzia hatua ya mwanzo ya kutoa maoni,maoni ya taasisi mbalimbali, maoni ya mabaraza hadi Tume ilipovunjwa rasmi waaliunga mkono michakato yote na mawazo ya wananchi, Iweje leo waje na mawazo tofauti ya kulazimisha serikali 2!!! wanatuyumbisha sisi wananchi. Basi nashauri mchakato wa maoni ya muundo upi wa serikali unaofaa, uanze upya na kila mwananchi apige kura ya maoni kwanza kujua ni aina ipi ya muundo inayotufaa, na maoni ya wananchi yaheshimiwe, ndipo baadaye tujadili katiba mpya.

    ReplyDelete
  13. Linalojitokeza hivi sasa katika duru za uchambuzi wa mchakato wa katiba mpya ni kuwa "HAKUTAKUWA NA KATIBA MPYA".Huu mvutano utaendelea hadi siku ya mwisho wa Bunge hili "utumbo". Maafikiano ya theluthi mbili juu ya tatu katu haitafikia na hata kama ikifikia na katiba to be ipigiwe kura na wananchi haitapa mandate ,matokeo yake basi Raisi wa Jamhuri hataitisha tena bunge la katiba na atatangaza TUENDELEE NA KATIBA TULIYONAYO.Ambapo itakuwa ni ushindi kwa warevu na ni ushindi kwa wajinga.Na wala hapatakuwa na malalamiko kuwa nchi inaongozwa unconstitutional maana katiba ya mwisho itakuwepo na itakuwa ikifanya kazi. Jee ni nani atakuwa mshindi na ni nani mshindwa?

    ReplyDelete
  14. Solution ya hili ni kuuvunja muungano tu, watanganyika kivyetu and wazanzibari Kivyao, na kila mtu arudi kwao, enough said.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...