Nashukuru sana kwa msaada wako.Wiki iliyopita niliweka tangazo langu humu nikiomba msaada wa kumpata dada aliyesahau simu yake ndani ya gari langu,wadau walitoa mawazo mbalimbali ya namna ya kumpata huyo dada.
Kuna mdau alinishauri nitoe line yake(iliyofungwa) na niweke line nyingine,nimefanya hivyo na nikampata rafiki yake akanieleza wapi mama yake anapatikana.
Bahati nzuri namfahamu mama huyo,hivyo nimeomba namba ya huyo mama kwa watu ,na nimeongea naye na wakati wowote nitaikabidhi simu hiyo kwa mama wa binti huyo.
Asanteeni sana kwa msaada wenu.
Mdau
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...