Katibu Mkuu wa CC,Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe na kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa nyumba 60 za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),katika kijiji cha Inyonga ndani ya Wilaya Mpya ya Mlele mkoani Katavi mapema leo jioni.
  Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),mkoa wa Katavi,Bwa.Nehemia Msigwa akifafanua zaidi kuhusiana na mradi huo kwa katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana mara baada ya kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa nyumba 60 za Shirika hilo,katika kijiji cha Inyonga ndani ya Wilaya Mpya ya Mlele mkoani Katavi leo.
 Meneja Huduma kwa jamii wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),makao Makuu jijini Dar,Bwa.Muungano Sagaya akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Ujumbe wake  kwenye uzinduzi wa mradi wa ujenzi wa nyumba 60 za Shirika hilo,katika kijiji cha Inyonga ndani ya Wilaya Mpya ya Mlele mkoani Katavi mapema leo jioni.
 Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),mkoa wa Katavi,Bwa.Nehemia Msigwa akizungumza mbele ya mgeni rasmi,katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kabla ya kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa nyumba 60 za Shirika hilo,katika kijiji cha Inyonga ndani ya Wilaya Mpya ya Mlele mkoani Katavi mapema leo jioni.
 Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mh.Rajab Rutengwe akizungumza jambo kabla ya katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa nyumba 60 za Shirika hilo,katika kijiji cha Inyonga ndani ya Wilaya Mpya ya Mlele mkoani Katavi mapema leo jioni.
 Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),mkoa wa Katavi,Bwa.Nehemia Msigwa akizungumza jambo na Mkuu wa Mkoa wa Katavi,Mh.Rajab Rutengwe kabla ya katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa nyumba 60 za Shirika hilo,katika kijiji cha Inyonga ndani ya Wilaya Mpya ya Mlele mkoani Katavi mapema leo jioni.



 Katibu Mkuu wa CC,Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa na Meneja wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC),mkoa wa Katavi,Bwa.Nehemia Msigwa kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi la mradi wa ujenzi wa nyumba 60 za Shirika hilo,katika kijiji cha Inyonga ndani ya Wilaya Mpya ya Mlele mkoani Katavi mapema leo jioni.
========  ======  =====

KATIBU Mkuu wa CCM amelipongeza Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kwa kasi ya ujenzi miradi ya nyumba za makazi na biashara kwenye miji mbalimbali hasa makao makuu ya wilaya mpya.

Kinana aliyasema hayo katika mji wa Inyonga wilayani Mlele mkoa wa Katavi wakati akiweka jiwe la msingi la ujenzi wa nyumba 60 za shirika hilo.

Alisema uongozi mpya wa NHC umerudisha heshima na hadhi ya shirika hilo kwa kufanya kazi ambazo inapaswa kuzitekeleza.Kwa mujibu wa Kinana, katika kipindi cha karibuni NHC, imekuwa ikitekeleza kwa kazi miradi ya ujenzi wa nyumba za viwango mbalimbali ambazo ni muhimu na kimbilio la watu wa kipato cha chini.

"Hii ndio kazi inayopaswa kufanywa na shirika la nyumba ambalo ni tegemeo la wananchi. CCM inatambua kazi mnayoifanya inakupongezeni na kuungeni mkono katika kutekeleza majukumu yenu," alisema.

Akizungumza kuhusu kilio cha kutaka kupunguziwa kodi kwenye vifaa vya ujenzi vya shirika hilo, Kinana alisema hoja hiyo ni muhimu na inayopaswa kusikilizwa na kupewa kipaumbele kwa lengo la kuwasaidia watu wa kipato cha chini.

"Naona hapa kuna hoja ya msingi kwa kuwa hakuna sababu ya kutoza kiwango kibwa cha kodi kama nyumba zinazojengwa zinawasaidia watu wa kipato cha chini wakiwemo watumishi wa umma wenye mishahara midogo," alisema.

Kwa upande wake, Meneja wa NHC mkoa wa Katavi, Nehemia Msigwa, alisema nyumba hizo 60 zitajengwa kwa kipindi cha miezi minane.

Alisema zitakapokamilika, nyumba hizo zitauzwa kwa bei tofauti huku ya juu ikiwa ni sh milioni 54 na ya chini sh milioni 38.

Msigwa alisema nyumba hizo ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa NHC kujenga nyumba 15,000 kwa kipindi hadi mwaka 2015.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...