Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Ghalib Mohamed Bilal akipata maelezo ya Historia, Muundo, Kazi na Utendaji wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kwa Afisa Habari wa Bunge Bw. Prosper Minja wakati kiongozi huyo alipotembelea banda la Bunge lililopo katika Viwanja vya Mnazi Mmoja leo lijini Dar es Salaam. Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni miongoni mwa washiriki wa maonesho ya maadhimisho ya Miaka 50 ya Muungano. Taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi zinashiriki katika kuonesha mafanikio makubwa yaliyofikiwa katika kipindi cha Miaka 50 Muungano.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Maalim Seif Shariff Hamad (kulia) akisaini Kitabu cha Wageni Mashuhuri alipotembelea banda la Ofisi ya Bunge lililoko katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Jijini Dar es Salaam wakati wa maonesho ya maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano. Picha na Prosper Minja - Minja

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...