Mbunge Kabati akikabidhi  mipira  kwa mratibu wa mashindano Rashid Bilo 'Shungu' katika makabidhiano yaliyofanyika katika uwanjwa wa Ipogoro.
 Mbunge kabati  akifunga mashindano ya Rita Kabati Vijana Cup yaliyofanyika katika Kata ya Ruaha mjini Iringa 
  Mbunge  wa viti maalum mkoa  wa Iringa Ritta Kabati akionyesha uwezo wake  kisoka huku mkuu wa wilaya ya Kibonde Venance Mwamoto kulia akishangaa utaalam wa mbunge huyo.

00000000  0000000 0000000

MASHINDANO YA MBUNGE YAMALIZIKA

Na Denis Mlowe,Iringa

MASHINDANO  ya kombe la mbunge yanayojulikana kwa jina la ‘Rita Kabati Vijana Cup’ yanayodhaminiwa na mbunge wa Viti maalum kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM),Rita Kabati, yamefikia  ukingoni juzi katika kata ya Ruaha jimbo la Iringa mjini huku mbunge huyo akiahidi makubwa kwa wanamichezo jimboni hapo  ikiwa ni pamoja na kuifikisha bungeni  timu itakayofanya  vema .

Akizungumza  juzi  wakati  wa  fainali  ya  kombe  hilo mchezo uliofanyika uwanja  wa  shule ya Msingi Ipogolo na kuzikutanisha timu za Jamaica Fc na News Boys ,Kabati  alisema  kuwa ameamua  kuanzisha mashindano  mbali mbali ya soka kwa  vijana kama  njia ya kuinua soka katika mji  wa Iringa na vitongoji vyake.

Alisema kuwa  mbali ya mashindano hayo kumalizika anakusudia  kuanzisha mashindano mengine ambayo  mbali ya mshindi  kupewa  zawadi mbali mbali bado timu bingwa  ataipeleka  bungeni mjini Dodoma ili kutambulishwa na kuhudhuria kikao kimojawapo  cha bunge.

Kabati  alisema kuwa katika ilani ya CCM inasisitiza  jinsi ambavyo  itakavyoendeleza sera  ya  michezo kwa  vijana na  tayari  utekelezaji  huo  umeanza katika mkoa  wa  Iringa na maeneo mbali mbali ya nchi.

Aongeza kuwa kama mbunge  wa mkoa  wa  Iringa atahakikisha vijana wanaanzishiwa mashindano ya mara kwa mara  ili  kuwaepusha na vishawishi mbali mbali kama utumiaji wa  madawa ya kulevya pia  kuifanya  michezo 

"Nina mpango  wa  kuendeleza  vijana  kimichezo  na ikiwezekana ligi kuu kuanzwa  kuchezwa mkoa  wa Iringa iwapo timu zetu zitafanya  vema katika mashindano mbali mbali kama ilivyo mikoa mingine ambayo imeendelea  kisoka zaidi" alisema Kabati

Katika fainali hiyo News Boys ilifanikiwa kuchukua ubingwa kwa kuwafunga Jamaica kwa penati 5 – 4 baada ya dk 90 kufungana goli moja kwa moja.

Katika mechi hiyo wafungaji walikuwa  Hasan Peng’e kwa upande wa Jamaica Fc na Michael Kalinga kwa upande wa News Boys.

Kwa upande  wake mratibu wa mashindano hayo Katibu Mkuu wa Chama cha Soka Manispaa ya Iringa, (IMFA) Rashid Shungu alisema  kuwa mbunge  huyo ameonyesha  jitihada  kubwa katika kuendeleza soka mjini Iringa na kumuomba  kuendelea  zaidi  kusaidia soka Iringa.

Shungu  alisema mashindano hayo yameleta  chachu  kubwa ya soka katika kata ya Ruaha ambapo  vijana wengi  wamehamasika na  kuonyesha  uwezo  wa hali ya juu katika soka na  kuwa lazima kuweka mkakati wa  kudumu wa  kuendeleza  vijana hao kisoka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...