Rais mstaafu wa awamu wa tatu Mh Benjamin Mkapa leo(jumatatu) amefanya ziara kumtembelea Shule ya msingi ya Manyara Ranchi inayofadhiliwa na shirika la kimataifa la uhifadhi wa wanyamapori la African wildlife foundation wilayani Monduli.
Mzee Mkapa ni Makamu mwenyekiti wa shirika hilo lenye makao yake mjini Washington Marekani.picha mbalimbali zinamuonesha waziri mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akimuongoza Rais Mkapa kuzuru shule hiyo.
Rais mstaafu wa awamu wa tatu,Mh. Benjamin Mkapa (katikati) akimsikiliza kwa makini Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa wakati alipotembelea Shule ya msingi ya Manyara Ranchi inayofadhiliwa na Shirika la Kimataifa la Uhifadhi wa Wanyama pori la African Wildlife Foundation,wilayani Monduli.
Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akimueleza jambo Rais mstaafu wa awamu wa tatu,Mh. Benjamin Mkapa wakati walipokuwa kwenye moja ya madarasa ya shule hiyo.
Rais mstaafu wa awamu wa tatu,Mh. Benjamin Mkapa akiagana na Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...