Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Amantius C. Msole akifuatilia kwa jambo kwa makini wakati wa mkutano wa Kisekta Baraza la Mawaziri wa Afya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaoendelea katika ukumbi wa Zanzibar Beach Resort mjini Unguja Zanzibar. Mkutano huo unaendelea katika ngazi ya Makatibu Wakuu.
Wajumbe wa Mkutano wa Kisekta wa Baraza la Mawaziri wa Afya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiendelea na majadiliano ya Mkutano huo unaoendelea katika ukumbi wa Zanzibar Beach Resort mjini Unguja Zanzibar. Mkutano huo unaendelea katika ngazi ya Makatibu Wakuu.
Wajumbe wa Mkutano wa Kisekta wa Baraza la Mawaziri wa Afya wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unaondelea katika ngazi ya Makatibu Wakuu wakiimba wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki mara baada ya kufunguliwa kwa Mkutano huo katika ukumbi wa Zanzibar Beach Resort mjini Unguja Zanzibar. Mkutano huo unaendelea katika ngazi ya Makatibu Wakuu.

Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa kisekta wa Afya wa Jumuiya ya Afrika umekamilika katika ngazi ya wataalamu Zanzibar.

Mkutano huu ambao ulianza tarehe 14 Aprili, 2014 na umekuwa ukiendelea kwa siku mbili na sasa unaingia ngazi ya Makatibu wakuu na utaitimisha na Mawaziri wa Afya tarehe 17 Aprili, 2014.

 Pamoja na mambo mengine Mkutano huu umepitia taarifa ya utekelezaji wa maamuzi na maagizo mbalimbali ya Mikutano iliyopita na pia kujadili masuala ya kukamilisha kwa Mpango Mkakati wa Sera ya Afya ya Jumuiya ya Afrika Mashariki,Itifaki ya Afya ya Jumuiya ,kujenga sekta ya rasilimali watu ya Afya ya magonjwa yanayoambukiza na yasiyoamabukiza, haki, jinsia na afya ya uzazi.

 Mkutano huo ulifunguliwa na Bi. Asha Ali Abdallahi, Katibu Mkuu ,Wizara ya Uwezeshaji, Jamii, Vijana na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambaye alizitaka Nchi Wanachama wa Jumuiya kuweka pamoja na kuimarisha sera muhimu kwa ajili ya kuendeleza na kukuza hali ya maisha kwa wananchi wa Afrika Mashariki.

 Naye Mkurugenzi wa Sekta za Kijamii wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki akiongea na wataalamu wa Mkutano huo alisema kuwa Sekretarieti ya Jumuiya inatumbua Juhudi za wataalamu hao kwa mchango wao mkubwa katika kuendeleza mtangamano wa Afrika Mashariki.

 Aidha Kiongozi wa ngazi ya wataalamu kwa upande wa Jamuhuri ya Muungano waTanzania Dkt. Elias M. Kwesi aliwakikishia ujumbe wa mkutano namna Tanzania ilivyo makini katika utekelezaji na uendelezaji wa Mtangamano na kuwataka wajumbe wa mkutano kwa pamoja kutekeleza sera na mikakati ya kupambana na magonjwa yayoibuka hususani ikiwemo kitisho cha magonjwa yasiyo ambukiza.

 Mkutano huu kwa sasa unaendelea katika ngazi ya makatibu wakuu na utaitimishwa katika ngazi ya Mawaziri.
 IMETOLEWA NA WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...