Mradi wa kuunganisha sekta za Wazalishaji matunda, mbogamboga na wenye hoteli (SECO) unaofadhiliwa na Serikali ya Switzerland umezinduliwa Jijini Arusha.

Mradi huo ambao lengo lake kuu ni kuboresha maisha ya watanzania wanaojihusisha na sekta hizo kwa kuongeza uzalishaji wao na uhakika wa masoko ya ndani nan je ya nchi, unaanza utekelezaji wake mara ,moja ukiwa na thamani ya jumla ya Dola za Ki marekani milioni tatu na nusu.

Uzinduzi wa Mradi huo umeshuhudiwa na Katibu Mtendaji wa UNCTAD Dkt Mukhisa Kituyi, Balozi wa Uswizi nchini Tanzania BwOlivier Chave na Mkurugenzi wa Idara ya Mtangamano wa Biashara katika Wizara ya Viwanda na Biashara Bw Lucas Saronga.
Katibu Mtendaji wa UNCTAD Dkt Mukhisa Kituyi (Kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Mtangamano wa Biashara wa Wizara ya Viwanda na Biashara Bw Lucas Saronga( Katikati) na Balozi wa Uswizi nchini Olivier Chave(Kulia) wakisaini hati za makubaliano ya utekelezaji mradi wa SECO.
Picha ya pamoja ya wafadhili na wawakilishi wa Serikali ya Tanzania walioshiriki uzinduzi wa mradi wa SECO uliofanyika Jijini Arusha.
Picha ya pamoja ya Washiriki wote wa Mkutano na uzinduzi wa mradi wa SECO uliofanyika mjini Arusha.
Baadhi ya Washiriki wa uzinduzi wa mradi wa SECO uliofanyika Jijini Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...