wasanii wa kike watatu wanao tamba katika tasinia ya muziki nchini shaa, mwasiti na khadija omari kopa wanatalajia kupamba tamasha la jukwaa la wanawake lijulikanalo kama familia kitchen part gala litakalo fanyika jijini dar es salaam siku ya kesho katika ukumbi wa diamond jubilee chini ya women in balance chini ya udhamini wa shirika la psi tanzania.
mratibu wa jukwaa hilo vida mndolwa amesema jukwaa hilo limelenga kutoa elimu mbalimbali hususani uzazi wa mpango na upimaji wa saratani ya mlango wa kizazi ili mafunzo yanayo fundishwa yaingie vizuri lazima yaendane na burudani.
vida ameongeza kuwa jukwaa hilo litaanza mapema saa 6 na anategemea kuwa litakuwa zaidi ya yale ya mwanza na dodoma kutokana na mwamko uliopo jijini dar es salaam
aidha wawakilishi wa psi wakizungumza kuhusu jukwaa hilo wamesema pamoja na burudani pia shirika hilo litatumia jukwaa hilo ambalo limekwisha fanyika dodoma na mwanza na kufanikiwa kwa kiasi kikubwa kuendesha zozi la upimaji afya hususani saratani ya mlango wa kizazi.
Daktari bingwa mshauri wa PSI dakta Joseph mashafi akisisitiza jambo katika mkutano na waandishi wa habari hawapo pichani kuhusu jukwaa la FAMILIA KITCHEN PARTY GALA TOUR 2014 ambayo inatalajia kufanyika jijini dar es salaam siku ya jumapili katika ukumbi wa diamond jubilee (kulia) mwanzilishi wa jukwaa hilo Vida Mndolwa anaye fuatia ni Mratibu wa mawasiliano kanda ya pwani PSI Bwana Mohamed Mziray wakimsikiliza kwa makini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...