Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii
(NSSF), Crescentius Magori akifafanua
jambo wakati wa semina kuhusu mafao na utunzaji kumbukumbu kwa maofisa utumishi RAS, DED na Manispaa kutoka mikoa yaote ya Tanzania Bara. Semina hiyo imeandaliwa na NSSF na kufanyika leo Mkoani Morogoro. Wa pili kushoto ni Ofisa Rasilimali Watu na Utawala, Chiku Matessa.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii
(NSSF), Crescentius Magori akitoa mada kuhusu
mafao ya muda mrefu ya pensheni ya uzeeni, Pensheni ya ulemavu, pensheni ya urithi
pamoja na mafao ya muda mfupi ambayo ni mafao ya matibabu, mafao ya kuumia
Kazini, mafao ya uzazi na msaada wa mazishi. Semina hiyo iliandaliwa na NSSF
kwa ajili ya maofisa utumishi RAS, DED na Manispaa kutoka mikoa yote ya
Tanzania Bara.
Mshiriki wa semina ya maofisa utumishi wa manispaa akisoma kipeperushi cha taarifa za Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kabla ya kuanza kwa semina ya maofisa utumishi ilifanyika mjini Morogoro na kuandaliwa na NSSF.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...