JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA WAZIRI MKUU
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MKOA WA RUKWA

Anuani ya simu:”REGCOM”                          Simu Na:(025)-2802138/2802144

Fax Na. (025) 2802217

Baruapepe: rasrukwa@yahoo.com


             OFISI YA MKUU WA MKOA,
     S.L.P. 128,
     SUMBAWANGA.



Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Eng. Stella M. Manyanya (Mb) kwa masikitiko makubwa anapenda kuwajulisha juu msiba mkubwa ulioukumba Mkoa wetu wa Rukwa wa kuondokewa na Mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mhe. Moshi Mussa Chang’a (62) aliyefariki jana jioni terehe 20 April, 2014 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa Shinikizo la Damu na Kisukari.

Mwili wa Marehemu Mhe. Chang’a unategemewa kusafirishwa kesho jioni kutoka Jijini Dar es Saam hadi nyumbani kwao Mkoani Iringa ambapo mazishi yake yatafanyika keshokutwa siku ya Jumatano tarehe 23 April, 2014.

Marehemu Mhe. Chang’a alizaliwa Mkoani Iringa Januari Mwaka 1952 na amewahi kushika nafasi mbalimbali Serikalini na katika Chama cha Mapinduzi (CCM). Katika nafasi ya Ukuu wa Wilaya amewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Mbeya, Tabora, Mkalama na Kalambo Mkoani Rukwa ambapo mauti yake yamemfika.

Katika Ngazi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) amewahi kuwa Katibu wa CCM Wilaya ya Njombe na Iringa Vijijini na Katibu Mwenezi wa CCM Mkoa wa Iringa.

Marehemu Mhe. Chang’a ameacha watoto watano (5) na Mjukuu Mmoja (1).Watoto wa kiume 3 na Wakike 2.
Kwa niaba ya Wananchi wa Mkoa wa Rukwa tunatoa pole kwa ndugu, jamaa, marafiki, na wote walioguswa na msiba huu mkubwa. Tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu awape nguvu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Sisi tulimpenda lakini Mungu kampenda zaidi.

Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi “AAAMIN”


Imetolewa na:

OFISI YA MKUU WA MKOA
RUKWA
Tarehe 21 April, 2014.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...