Wahalifu mtandao wameendelea kubuni aina mpya za kufanikisha uhalifu wa mitandao hasa katika makampuni. Hili limeonekana kushika kasi katika maeneo mbali mbali na limeingia katika mijadala na kuwa ni moja ya maswala yaliyo onekana yana haja kufikiswhwa kwa jamii ili kuendelea kukuza uelewa wa makosa mtandao.
Kwanza kabisa, Faili lolote ambalo linasomeka na kiambatanishi .exe mfano: umoja.exe nifaili ambalo limedhamiriwa kuingizwa kuwa ni moja ya program za komputa hivyo kabla ya kubonyeza aina hii ya mafaili lazima uwe na ujuzi wa unacho kibonyeza ndicho mahitaji yako au la.
Aidha, kwa upande wa aina hii ya uhalifu umekua ukitumia vifaa kama USB, au CD na DVD ambazo muhusika anayetakiwa kudhuriwa anaweza kuvikuta aina hizi za vifaa kwenye ofisi yake na maranyingi vinakua vimekaa katika sura ya kushawishi muhusika avichukue.
Maara baada ya kufanya hivyo kinachofata ni muhusika kuwa na kutaka kujua nini kiko ndani, na ndipo muhusika atataka kufungua na hapo kunakua na faili/mafaili yenye majina mfano, Mishahara.exe (ambapo muhusika atajua ni faili litakalo onyesha mishahara ya wafanya kazi) na huwenda pia ika wa majina mengine mbali mbali.
Muhusika anapo bonyeza ili kutaka kuona hiyo mishahara, mhalifu anakua tayari kashaingia katika komputa yake na kuweza kuanza kuleta madhara punde tu anapo anaza kutumia mtandao. “mara unapo kua mtandaoni tayari unaongeza wigo la mhalifu kuweza kukudhuru na unapotoka mtandaoni mhalifu anakua hana tena nafasi ya kukudhuru.” – Yusuph Kileo.
Hili ni jambo muhimu sana kulifahamu yakua unapokua mtandaoni tayari unakua si salama sana na utokapo mtandaoni unakua salama kimtamtandao kutokana na madhara ya usalama mtandao yanaweza kuonekana na kujitokeza pale tu unapo kua umejiingiza mtandaoni.

Hivyo, unapo kuta kitu chochote kama CD, USB, DVD na vingine vyenye mfano wa hivyo ambavyo hujui vimefikaje au hukuwa umeagiza viletwe kwako eidha mlangoni mwa ofisi kwenye lift ya ofisi au hata mezani ofisini kwako yako unachopaswa kufanya ni kuviwasilisha maramoja kwa kitengo cha usalama mtandao “Computer security department” kwa hatua zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...